Tanzania ina kodi zaidi ya 52, ipi inakukera tuijadili!

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
84,036
142,131
Nchi yetu ina aina ya kodi na tozo zaidi ya 52, na hivi ndio vyanzo vikuu vya mapato ya serikali.

Wewe kama mlipa kodi una maoni gani juu ya mfumo wa ulipaji kodi ktk nchi yetu?

Ni kodi ipi unayoiona kama kero kwa jamii, tutajie tupate fursa ya kuijadili.Mfano wa kodi maarufu ni kama Vat, Paye, custom duties, property taxes, ada za leseni nk, nk.

Paye ndio kodi pekee inayotozwa na kulipwa kwa usahihi zaidi, nyinginezo zimetawaliwa na figisu za hapa na pale.

Karibuni kwa mjadala ili wanasiasa wetu pale bungeni waweze kusikiapo sauti zetu.
 
Nilifikiri nitakuta list iliyojipanga kumbe!!!

Ni tag ukiiweka nami nikujibu.
 
Nimeanda kulipia kodi ya ardhi imepanda kutoka sh 12000 mpaka 105000 kwa mwaka very very amazing.
 
Nchi yenyewe masikini wanajaza mikodi kibao badala ya kuangalia multiplier effect ya kuwepo hiko kiwanda au biashara.
Wanadhani wakiweka hizo bureaucratic process wataifanya Tanzania kuongeza mapato mengi ilihali wanapunguza mengi sana.
Urais wa kufanya biashara Tanzania ni mbovu kupindukia, ila waziri yupo bize kuhubiri viwanda bila kuangalia wapi Tanzania inakosea kwenye kuvutia viwanda.
Viongozi wa Tanzania ni kama vifaru wanaojiendea bila kuwa na mission na vision.
 
Kukwepa kodi ni jinai
Je, first, second, & third families zetu wanalipa PEYE na kodi za mapato ya biashara zao ikiwa ni pamoja na mijumba ya serikali waliyojibinafsisha?
Kwa mfabo, kila ikifika msimu wa kuwasilisha ulipaji kodi nchini Marekani, first family ndio huwa ya kwanza kuwasilisha na taarifa zake huanikwa hadharani!
 
Kodi ya kichwa au service development levy.
SDL= Kodi ya Kichwa, ilibadilishwa tu jina ila dhana ni ile ile.
 
Je, first, second, & third families zetu wanalipa PEYE na kodi za mapato ya biashara zao ikiwa ni pamoja na mijumba ya serikali waliyojibinafsisha?
Kwa mfabo, kila ikifika msimu wa kuwasilisha ulipaji kodi nchini Marekani, first family ndio huwa ya kwanza kuwasilisha na taarifa zake huanikwa hadharani!
Isipokuwa Hii first family ya Mpenda masifa(trump)
 
Kodi ya kuingiza gar pale bandarin... Utafikir huku ndan tuna kiwanda cha magar. Co kwa Kodi hiyo aisee
 
Nchi yetu ina aina ya kodi na tozo zaidi ya 52, na hivi ndio vyanzo vikuu vya mapato ya serikali.

Wewe kama mlipa kodi una maoni gani juu ya mfumo wa ulipaji kodi ktk nchi yetu?

Ni kodi ipi unayoiona kama kero kwa jamii, tutajie tupate fursa ya kuijadili.Mfano wa kodi maarufu ni kama Vat, Paye, custom duties, property taxes, ada za leseni nk, nk.

Paye ndio kodi pekee inayotozwa na kulipwa kwa usahihi zaidi, nyinginezo zimetawaliwa na figisu za hapa na pale.

Karibuni kwa mjadala ili wanasiasa wetu pale bungeni waweze kusikiapo sauti zetu.
Naumia sana Payee huwa siielewi kabisa.
 
Back
Top Bottom