Tanzania hakuna umoja wala mshikamano. Unafiki umetujaa vifo vya marubani chipukizi Serengeti vinaakisi

haszu

JF-Expert Member
Oct 10, 2017
837
1,550
Imagine, ajari ya ndege imeua wawili ila ndege ya serikali imebeba mwili wa mtu mmoja na mwengine atabebwa na ndege nyingine kwa uchunguzi zaidi,

Vyombo vya habari na mitandao ya kijamii habari sasa imebadilika kutoka ajari ya ndege haki kua Mabeyo afiwa na mwanae na viongozi wanaenda kutoa pole huko.

Watanzania tuna double standard sana. Na yeye aliekufa pia ni binadam kama uyo wa mku wa majeshi,

===================================

Baada ya ajali kutokea ilitangazwa kuwa waliofariki ni rubani na abiria mmoja. Baadaye ikatangazwa kuwa rubani aliyefariki ni mtoto wa Mkuu wa Majeshi Gen. Mabeyo. kuanzia hapo vyombo vya habari vyote vikajaa habari na picha za mtoto wa CDF kufa ajalini.

Muda si muda tukaanza kuona viongozi mbali mbali kuanzia rais wakimininika nyumbani kwa CDF kumpa pole. Viongozi mbali mbali wa upinzani nao hawakukosekana katika msafara huo. Baadhi ya taasisi na mashirika yakaanza kutoa salamu maalumu za pole kwa CDF kwa kuchapisha magazetini na kwenye mitandao ya jamii.

Yule aliyeitwa abiria baadaye tukaambiwa alikuwa ni rubani mwanafunzi/msaidizi. Vyovyote iwavyo hakuna aliye hangaika na habari zake katika mlolongo wa nilio wataja hapo juu. Vyombo vya habari na mitandao mingi ya kijamii imejaa habari za kifo cha mtoto wa CDF tu huyu mwingine kutoka katika familia ya wanyonge ambao rais huwa anajitambulisha kuwa ni rais wao, hasikiki kabisa na unaweza weza kudhani katika ajali ile alikufa mtoto wa Mabeyo tu.

Hakika hii ni aibu. Walikufa pamoja sasa imekuwaje mmoja anaonekana ndiye marehemu zaidi ya mwenzake? Hii ni aibu kubwa kwa vyombo vyetu vyote vya habari kwa kutoa coverage kubwa kwa mtu mmoja wakati walioathirika walikuwa wawili. Viongozi nao kuanzia namba moja wajithamini namna walivyolichukulia suala hili



View attachment 1215690

View attachment 1215691



View attachment 1215693

Wakamsahau mnyonge!

Pumzika kwa AMANI mnyonge mwenzetu nasi tupo nyuma yakoo😭😭😭😭
Vigogo mtupishe kidogo nasi tumfariji mnyonge mwenzetu😭😭😭😭
Image may contain: 1 person

RIP bro naona wanamkumbuka wa mabeyo tu kwa kuwa baba Ni mkuu wa wajeda😠
Image may contain: 1 person, selfie

View attachment 1215683
 
Kabla ya kuhitimisha kwa hayo ulosema nazani ni vema tutafute kufahamu ukweli wa mambo ukoje?

Before reaching a conclusion of yours we have to establish the facts first!

Je hali ya upande wa pili ikoje? Je ndugu zake wamesemaje?
Walishaamua mwili upelekwe wapi?
Kumbuka ajali imetokea mkoa wa Mara na asili ya jina la huyo mwingine iko kama ya kijaluo kama sijakosea, ambapo ni karibu na eneo la tukio hata kama ni wa nchi ya Kenya bado kutokea huko ni karibu kuliko angeletwa Dar es salaam,
Na wajaluo hupenda kuzika kwao, sasa mwili ubebwe kuletwa Dar halafu urudishwe tena Ujaluoni?

Hiyo gharama itakuwaje?!

Ndege haisimami popote kama gari hivyo haingeweza kusema ipitie mahala pengine kuupeleka huo mwili mwingine unless u assume kwamba kama huo mwili nao ungetakiwa kuja Dar es salaam!

Jukumu la kubeba mwili wa mtu wa watu siyo kitu rahisi sana, unaweza tenda Jema ukaishia kulaumiwa,

Zoezi lote limefanyika watu wakiwa wamechanganyikiwa,

Kabla ya kumlaumu tutafute kupata ukweli wa mambo kwanza,

Tukijiridhisha kuwa ridhaa ya kubeba mwili kuleta Dar es salaam ilikuwepo lakini walikataa basi hapo tutaweza kuhoji kwanini? Wameamua hivyo? Na pengine kuanza kuwalaumu!

Tafuta kupata taarifa sahihi toka kwa watu sahihi wakiwemo wana familia wa karibu sana wa ule mwili ukoachwa kule kabla ya kulaumu kisha ulete mrejesho!

Ikithibitika kuwa waliombwa kusaidia kuuleta mwili Dar na wakakataa bila sababu ya msingi hapo nitakuunga mkono ktk kuwalaumu!
 
Kabla ya kuhitimisha kwa hayo ulosema nazani ni vema tutafute kufahamu ukweli wa mambo ukoje?
Before reaching a conclusion of yours we have to establish the facts first!
Je hali ya upande wa pili ikoje? Je ndugu zake wamesemaje?
Walishaamua mwili upelekwe wapi?
Kumbuka ajali imetokea mkoa wa Mara na asili ya jina la huyo mwingine iko kama ya kijaluo kama sijakosea, ambapo ni karibu na eneo la tukio hata kama ni wa nchi ya Kenya bado kutokea huko ni karibu kuliko angeletwa Dar es salaam,
Na wajaluo hupenda kuzika kwao, sasa mwili ubebwe kuletwa Dar halafu urudishwe tena Ujaluoni?
Hiyo gharama itakuwaje?!
Ndege haisimami popote kama gari hivyo haingeweza kusema ipitie mahala pengine kuupeleka huo mwili mwingine unless u assume kwamba kama huo mwili nao ungetakiwa kuja Dar es salaam!
Jukumu la kubeba mwili wa mtu wa watu siyo kitu rahisi sana, unaweza tenda Jema ukaishia kulaumiwa,
Zoezi lote limefanyika watu wakiwa wamechanganyikiwa,
Kabla ya kumlaumu tutafute kupata ukweli wa mambo kwanza,
Tukijiridhisha kuwa ridhaa ya kubeba mwili kuleta Dar es salaam ilikuwepo lakini walikataa basi hapo tutaweza kuhoji kwanini? Wameamua hivyo? Na pengine kuanza kuwalaumu!
Tafuta kupata taarifa sahihi toka kwa watu sahihi wakiwemo wana familia wa karibu sana wa ule mwili ukoachwa kule kabla ya kulaumu kisha ulete mrejesho!
Ikithibitika kuwa waliombwa kusaidia kuuleta mwili Dar na wakakataa bila sababu ya msingi hapo nitakuunga mkono ktk kuwalaumu!
kasome bandiko lililowekwa JF, pili umesikia uyo mwingine akizungumzwa ?
 
Kama huna kipato ata kanisani hutopata heshima unayo staili... kikubwa tuzichange pesa wakuu ,
we unashangaa hii kuna wale wa ramba ramba tv wao walibebwa na ndege waka muacha dereva wa kosta adi daftari lipite kijiweni kwake
Acha urongo kijana, unaushahidi na uyasemayo au ulibeba lile watu walikua wanasema hapa.
Punguza mihemko
 
Imagine, ajari ya ndege imeua wawili ila ndege ya serikali imebeba mwili wa mtu mmoja na mwengine atabebwa na ndege nyingine kwa uchunguzi zaidi,

Vyombo vya habari na mitandao ya kijamii habari sasa imebadilika kutoka ajari ya ndege haki kua Mabeyo afiwa na mwanae na viongozi wanaenda kutoa pole huko.

Watanzania tuna double standard sana. Na yeye aliekufa pia ni binadam kama uyo wa mku wa majeshi,
Je unaijua vizuri familia ya huyo mtu mwingine ikoje ,Mimi naamini pia wao wako vizuri sema hawana umaarufu tu na huyo mwingine amekua maarufu kwa sababu tu ya cheo cha Baba yake!!
 
Aisee wanabodi kilichobaki ni kutafuta hela tu ili uthaminiwe katika jamii hii ya kitanzania.

Imetokea ajali ya vijana wetu wawili(mungu azilaze roho zao panapostahili) Nelson Venance Mabeyo na Nelson Olutu
Kuna kitu nilitaka ninyamaze ila kila nikifikiria najikuta naongea mwenyewe na maswali yanakuwa mengi kuliko majibu yake.

Hivi Watanzania tumefikia huku? Au kuna mahali tunakwama na uwezo wa kufikiria unapungua? Naomba kuwauliza ndugu zangu, au mimi ndo nimeanza kuchoka kichwani?

Jana vyombo vyote vimeripoti tukio la ajali ya ndege ndogo ya Auric Air na kusababisha vifo vya watu wawili akiwemo mtoto wa mkuu wetu wa Majeshi nchini, aitwaye Nelson Mabeyo na mwingine nikaambiwa anaitwa Nelson Olutu, hapo hapo nikaona helkopta ya JWTZ ikibeba mwili wa Nelson kumsafirisha kuurejesha kwao kwa hatua za mazishi.

Nimeona viongozi wengi pia wakitoa Pole na salamu za rambirambi kwa familia ya Mkuu wa Majeshi, ila sijaona kiongozi yeyote akihani msiba au salamu za rambirambi kwa familia ya yule marehemu aliyepata ajali na mtoto wa mkuu wetu wa majeshi.

Mwaka juzi niliwahi kuandika kwamba kuna watu huwa wanafariki na wengine wanafariki zaidi yaani wanakufa tuu.
Wanaofariki wanawafariji wengi, utaona kila mtu anaelekeza salamu na miguu huko ila anaekufa hakuna anaejali wala kuguguswa na msiba huo, ndugu yangu naomba ukazane kuhudhuria misibani, utaiona thamani ya uhai wako.
Hadi muda huu sijui yule mwingine aliyefariki ni wa wapi, ndugu wamempokea au bado! Haijulikani.

Nimeona niwashirikishe hili, Utanzania wetu unatokana na Udugu, Umoja na ushirikiano wetu, hawa marehemu wote walikuwa kwenye ndege moja, wakiendesha wote na kuongea na kufurahi pamoja, ila mmoja anapewa kipaumbele zaidi kuliko hata mwingine, sijui familia yake inajisikiaje, hata kampuni ya ndege husika sijui wanajisikiaje pia.

Nimefadhaika sana, najua wengine hawatanielewa katika hili ila ipo siku tutaelewana, tunajengeana mgawanyiko wa Udugu, Umoja na ushikamano wetu kwa vitu vidogo mno. Mnayoyaona leo yakifanyika Ulaya na kwingineko ya familia kuzikana wenyewe kwa wenyewe yalianzishwa na hii kitu, kwamba familia fulani zinakuwa bora zaidi kuliko familia fulani.

Nawatakia marehemu wote walale mahali salama, wote kwa majina ni Nelson isipokuwa mmoja ni Mabeyo na mwingine ni Olutu.

Mtakaokwazika, naomba mnisamehe mimi mkosefu nisiokuwa na adabu.labda niulize maswali je mtoto wa Mabeyo analiliwa sana kwa kuwa aliandaliwa aje aendeshe Bombadier? Kwahyo taifa limemkosa rubani wake aliyeandaliwa?
Tuseme Amen.
 
Umeonga suala la msingi sana,Mimi hata Jina rubani wa pili nimelijua leo baada ya kusikia redioni,hata ukifuatilia mada humu JF msisitizo ilikuwa mtoto wa CDF,huyu mwingine hata jina alikuwa hatajwi,tunahitaji kubadilika

Swali;Huyo alieandaliwa kuendesha Bombardier aliandaliwa na nani?
 
Nimebakiza kusafisha dining room, men and women toilet bathroomsna changing room. Kuna backside area corridor na vyoo vyake viwili karibu na service line. Halafu naenda kutupa kwenye trashbin takataka zote nilizolundika halaf faster kwenye kazi nyingine sehemu nyingine .

Nani aliwadanganya nyie binadamu wote ni sawa?

Fanyeni kazi
Kumbuka kwenye katiba ya TANU Binaadamu wote ni sawa!
 
Msiba wa Azam Media pia Mwili wa Dereva wa Coaster haukupewa nafasi wala kusafirishwa.
Msiba wa Lucky Vicent, Dereva Je?
Msiba wa Kibonde vs Ruge Je?
Dunia haina Usawa pambana.
 
Back
Top Bottom