Tanzania, from an elephant to a bedbug!

Sijali

JF-Expert Member
Sep 30, 2010
2,589
1,679
'Tanzania, kutoka kuwa ndovu kuja kuwa kunguni'.

Hakika Tanzania katika ushawishi wa kidiplomasia Afrika, duniani, imekuwa si chochote. Jana, mkataba muhimu wa amani baina ya Ethiopia na wapiganaji wa TPLF wa Tigray ulitiwa saini huko Afrika ya Kusini. Nani alikuwepo huko? Kenya, Afrika Kusini yenyewe na Nigeria!

Siku hizi si ajabu Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa nchi kubwa duniani akaamua kutembelea Afrika, akaanza ziara yake Uganda, kisha akaruka kwenda Rwanda, Kenya na kisha kurudi alikotoka!

Tanzania inarukwa tu kama doa jeusi. Kinachonitia wasi wasi ni kwamba kila nikichunguza sioni dalili kwamba jambo hili linawakera walio na dhamana ya diplomasia.

Wasi wasi wangu mkubwa ni kuwa Wizara hiyo, hasa baada ya rais Mkapa, imekuwa , kama nyinginezo, ikikabidhiwa watu kwa misingi ya ukaribu wa kisiasa na hata urafiki binafsi, na si juu ya misingi ya taaluma na uweledi wa kusuka diplomasia na mahusiano.

Najua kuna wale walionyweshwa maji ya uzalendo bandia watakaosema 'ah, acha tujali mambo yetu tu!' Hawa hawafahamu, maskini!

Kuwa diplomasia inachangia katika kila kitu, hata uchumi wa nchi. Tena wakati diplomasia yetu ilipokuwa kilele wakati wa Mwalimu, kulikuwa na faida nyingine kuwa Watanzania walikuwa na uwelewa mkubwa wa mambo ya dunia, kuliko sasa.

Kabla sijamaliza, kwa vile nimefananisha kipindi hiki na cha nyuma, hasa cha Mwalimu, huenda ikadhaiwa ningependa kuona diplomasia ile ile ya kipindi cha Mwalimu. La hasha! Kipindi hicho nimekiishi na nikaona jinsi gani diplomasia ya nje ilikuwa ikichukua muda wote wa siasa zetu, hata kusahahu kutatua matatizo ya ndani.

Kibaya zaidi, ilitumika kwa kuwachagulia wengine jinsi gani waendeshe nchi zao. Tukawa twawaunga mkono 'Wajamaa' akina Mugabe dhidi ya Abel Muzorewa na Nkomo, Neto dhidi ya Holden Roberto, Samora Machel dhidi ya Andre Matsangaisa na Afonso Dhlakama n.k.

Baya zaidi, diplomasia hiyo haikuwa na malengo ya kuleta faida za kiuchumi, isipokuwa kui 'bleed' tu Tanzania.

Hapana! Ninachokikusudia ni kuwa tuwe na diplomasia ya kuitangaza nchi yetu na kuwa shina la utatuzi wa matatizo ya Waafrika wenzetu. Kwa nini hatuanzi kwa kusuluhisha mgogoro wa Rwanda/Uganda, Rwanda/ DRC?

Unapojulikana Kimataifa, inakuwa rahisi pia kuwa na mahusiano ya kiuchumi, kibiashara, kiutalii, kitaaluma, kiutamaduni n.k.
 
Umemaliza kwa kutupa jina kunguni au chawa. Sasa kunguni yeye hawezi kuwa na msimamo na kusimamia anachokiamini.
 
Diplomasia kuubwa huku wananchi wako wanakufa njaa ni upumbavu
Enzi za Nyerere tulikuwa tunatumia asilimia 40 ya bajeti kusaidia Uhuru wa nchi tele Kama Mozambique Hadi South Africa halafu walivyopata Uhuru wanapiga na kuwachoma Moto watanzania huko...Bora tutulie tufanye yetu..

Sisi hatukwepeki...Rwanda anategemea Bandari ...chakula na mafuta kupitia kwetu...Sisi ndo nchi pekee iliyo zungukwa na nchi karibu 10...
We are giant hata tukiwa tumesinzia
 
'Tanzania, kutoka kuwa ndovu kuja kuwa kunguni'.

Hakika Tanzania katika ushawishi wa kidiplomasia Afrika, duniani, imekuwa si chochote. Jana, mkataba muhimu wa amani baina ya Ethiopia na wapiganaji wa TPLF wa Tigray ulitiwa saini huko Afrika ya Kusini. Nani alikuwepo huko? Kenya, Afrika Kusini yenyewe na Nigeria!

Siku hizi si ajabu Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa nchi kubwa duniani akaamua kutembelea Afrika, akaanza ziara yake Uganda, kisha akaruka kwenda Rwanda, Kenya na kisha kurudi alikotoka!

Tanzania inarukwa tu kama doa jeusi. Kinachonitia wasi wasi ni kwamba kila nikichunguza sioni dalili kwamba jambo hili linawakera walio na dhamana ya diplomasia.

Wasi wasi wangu mkubwa ni kuwa Wizara hiyo, hasa baada ya rais Mkapa, imekuwa , kama nyinginezo, ikikabidhiwa watu kwa misingi ya ukaribu wa kisiasa na hata urafiki binafsi, na si juu ya misingi ya taaluma na uweledi wa kusuka diplomasia na mahusiano.

Najua kuna wale walionyweshwa maji ya uzalendo bandia watakaosema 'ah, acha tujali mambo yetu tu!' Hawa hawafahamu, maskini!

Kuwa diplomasia inachangia katika kila kitu, hata uchumi wa nchi. Tena wakati diplomasia yetu ilipokuwa kilele wakati wa Mwalimu, kulikuwa na faida nyingine kuwa Watanzania walikuwa na uwelewa mkubwa wa mambo ya dunia, kuliko sasa.

Kabla sijamaliza, kwa vile nimefananisha kipindi hiki na cha nyuma, hasa cha Mwalimu, huenda ikadhaiwa ningependa kuona diplomasia ile ile ya kipindi cha Mwalimu. La hasha! Kipindi hicho nimekiishi na nikaona jinsi gani diplomasia ya nje ilikuwa ikichukua muda wote wa siasa zetu, hata kusahahu kutatua matatizo ya ndani.

Kibaya zaidi, ilitumika kwa kuwachagulia wengine jinsi gani waendeshe nchi zao. Tukawa twawaunga mkono 'Wajamaa' akina Mugabe dhidi ya Abel Muzorewa na Nkomo, Neto dhidi ya Holden Roberto, Samora Machel dhidi ya Andre Matsangaisa na Afonso Dhlakama n.k.

Baya zaidi, diplomasia hiyo haikuwa na malengo ya kuleta faida za kiuchumi, isipokuwa kui 'bleed' tu Tanzania.

Hapana! Ninachokikusudia ni kuwa tuwe na diplomasia ya kuitangaza nchi yetu na kuwa shina la utatuzi wa matatizo ya Waafrika wenzetu. Kwa nini hatuanzi kwa kusuluhisha mgogoro wa Rwanda/Uganda, Rwanda/ DRC?

Unapojulikana Kimataifa, inakuwa rahisi pia kuwa na mahusiano ya kiuchumi, kibiashara, kiutalii, kitaaluma, kiutamaduni n.k.

Palikuwa na uzi wenye maudhui kama yako:

Lililokuwa taifa la kupigiwa Mfano halipo tena

Wanapoitishwa kujiuzuru wanaanza kutafuta wachawi wakati wachawi ni wao wenyewe.
 
Mijitu mingine hata haisomi, yataka tu isomwe yoo. Si nimesema wazi sipendi kuona diplomasia kama ile ya wakati wa Mwalimu?
 
Ethiopian na TPLF inawahusu nini Bongonyoso...
Mkae kwa kutulia na kuhakikisha maji yanatoka kwenye kila bomba na umeme unawaka kila kwenye kila taa.....baada ya hapo ndio halafu ndio mfikirie kunusanusa kila umbea wa nchi zingine....
 
Diplomasia kuubwa huku wananchi wako wanakufa njaa ni upumbavu
Enzi za Nyerere tulikuwa tunatumia asilimia 40 ya bajeti kusaidia Uhuru wa nchi tele Kama Mozambique Hadi South Africa halafu walivyopata Uhuru wanapiga na kuwachoma Moto watanzania huko...Bora tutulie tufanye yetu..

Sisi hatukwepeki...Rwanda anategemea Bandari ...chakula na mafuta kupitia kwetu...Sisi ndo nchi pekee iliyo zungukwa na nchi karibu 10...
We are giant hata tukiwa tumesinzia
Sasa hivi hakuna maji wala umeme.


Ng'ombe wewe stand up

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
 
Diplomasia kuubwa huku wananchi wako wanakufa njaa ni upumbavu
Enzi za Nyerere tulikuwa tunatumia asilimia 40 ya bajeti kusaidia Uhuru wa nchi tele Kama Mozambique Hadi South Africa halafu walivyopata Uhuru wanapiga na kuwachoma Moto watanzania huko...Bora tutulie tufanye yetu..

Sisi hatukwepeki...Rwanda anategemea Bandari ...chakula na mafuta kupitia kwetu...Sisi ndo nchi pekee iliyo zungukwa na nchi karibu 10...
We are giant hata tukiwa tumesinzia

Haufahamu kua Burundi na Rwanda kuna mizigo yao hupitia Mombasa? Unachotakiwa kufahamu Bandari hata kenya wanayo na wanapata mapato mengi kuliko sisi hivo hatuna uspecial wowote wa kuringa kivile, Ushawishi kwenye siasa za Kikanda ziliisha na Mkapa zaidi ya hapo hatuna jipya, Uchumi imara ndio unakufanya uwe na ushawishi sasa nchi iko kundi la nchi maskini duniani pamoja na rasilimali zote hizo unadhani nani atakuheshimu? Kwa akili za viongozi wako nchi ingekua jangwa ingekuaje? Bahari, mito, maziwa na maji ni shida, gesi yote iliyopo na umeme ni shida hao watu utasema wana akili sawa sawa? Bajeti asilimia 40 hadi 50 ukazungushe bakuli unahisi utaheshimika?
 
'Tanzania, kutoka kuwa ndovu kuja kuwa kunguni'.

Hakika Tanzania katika ushawishi wa kidiplomasia Afrika, duniani, imekuwa si chochote. Jana, mkataba muhimu wa amani baina ya Ethiopia na wapiganaji wa TPLF wa Tigray ulitiwa saini huko Afrika ya Kusini. Nani alikuwepo huko? Kenya, Afrika Kusini yenyewe na Nigeria!

Siku hizi si ajabu Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa nchi kubwa duniani akaamua kutembelea Afrika, akaanza ziara yake Uganda, kisha akaruka kwenda Rwanda, Kenya na kisha kurudi alikotoka!

Tanzania inarukwa tu kama doa jeusi. Kinachonitia wasi wasi ni kwamba kila nikichunguza sioni dalili kwamba jambo hili linawakera walio na dhamana ya diplomasia.

Wasi wasi wangu mkubwa ni kuwa Wizara hiyo, hasa baada ya rais Mkapa, imekuwa , kama nyinginezo, ikikabidhiwa watu kwa misingi ya ukaribu wa kisiasa na hata urafiki binafsi, na si juu ya misingi ya taaluma na uweledi wa kusuka diplomasia na mahusiano.

Najua kuna wale walionyweshwa maji ya uzalendo bandia watakaosema 'ah, acha tujali mambo yetu tu!' Hawa hawafahamu, maskini!

Kuwa diplomasia inachangia katika kila kitu, hata uchumi wa nchi. Tena wakati diplomasia yetu ilipokuwa kilele wakati wa Mwalimu, kulikuwa na faida nyingine kuwa Watanzania walikuwa na uwelewa mkubwa wa mambo ya dunia, kuliko sasa.

Kabla sijamaliza, kwa vile nimefananisha kipindi hiki na cha nyuma, hasa cha Mwalimu, huenda ikadhaiwa ningependa kuona diplomasia ile ile ya kipindi cha Mwalimu. La hasha! Kipindi hicho nimekiishi na nikaona jinsi gani diplomasia ya nje ilikuwa ikichukua muda wote wa siasa zetu, hata kusahahu kutatua matatizo ya ndani.

Kibaya zaidi, ilitumika kwa kuwachagulia wengine jinsi gani waendeshe nchi zao. Tukawa twawaunga mkono 'Wajamaa' akina Mugabe dhidi ya Abel Muzorewa na Nkomo, Neto dhidi ya Holden Roberto, Samora Machel dhidi ya Andre Matsangaisa na Afonso Dhlakama n.k.

Baya zaidi, diplomasia hiyo haikuwa na malengo ya kuleta faida za kiuchumi, isipokuwa kui 'bleed' tu Tanzania.

Hapana! Ninachokikusudia ni kuwa tuwe na diplomasia ya kuitangaza nchi yetu na kuwa shina la utatuzi wa matatizo ya Waafrika wenzetu. Kwa nini hatuanzi kwa kusuluhisha mgogoro wa Rwanda/Uganda, Rwanda/ DRC?

Unapojulikana Kimataifa, inakuwa rahisi pia kuwa na mahusiano ya kiuchumi, kibiashara, kiutalii, kitaaluma, kiutamaduni n.k.
Kipaumbele cha mama sasa hivi ni 2025! Ameisha onja utamu wa kuwa Raisi wa Muungano, na Tanganyika ni tamu sana, sasa hivi hawazi chochote ni 2025 tu
 
'Tanzania, kutoka kuwa ndovu kuja kuwa kunguni'.

Hakika Tanzania katika ushawishi wa kidiplomasia Afrika, duniani, imekuwa si chochote. Jana, mkataba muhimu wa amani baina ya Ethiopia na wapiganaji wa TPLF wa Tigray ulitiwa saini huko Afrika ya Kusini. Nani alikuwepo huko? Kenya, Afrika Kusini yenyewe na Nigeria!

Siku hizi si ajabu Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa nchi kubwa duniani akaamua kutembelea Afrika, akaanza ziara yake Uganda, kisha akaruka kwenda Rwanda, Kenya na kisha kurudi alikotoka!

Tanzania inarukwa tu kama doa jeusi. Kinachonitia wasi wasi ni kwamba kila nikichunguza sioni dalili kwamba jambo hili linawakera walio na dhamana ya diplomasia.

Wasi wasi wangu mkubwa ni kuwa Wizara hiyo, hasa baada ya rais Mkapa, imekuwa , kama nyinginezo, ikikabidhiwa watu kwa misingi ya ukaribu wa kisiasa na hata urafiki binafsi, na si juu ya misingi ya taaluma na uweledi wa kusuka diplomasia na mahusiano.

Najua kuna wale walionyweshwa maji ya uzalendo bandia watakaosema 'ah, acha tujali mambo yetu tu!' Hawa hawafahamu, maskini!

Kuwa diplomasia inachangia katika kila kitu, hata uchumi wa nchi. Tena wakati diplomasia yetu ilipokuwa kilele wakati wa Mwalimu, kulikuwa na faida nyingine kuwa Watanzania walikuwa na uwelewa mkubwa wa mambo ya dunia, kuliko sasa.

Kabla sijamaliza, kwa vile nimefananisha kipindi hiki na cha nyuma, hasa cha Mwalimu, huenda ikadhaiwa ningependa kuona diplomasia ile ile ya kipindi cha Mwalimu. La hasha! Kipindi hicho nimekiishi na nikaona jinsi gani diplomasia ya nje ilikuwa ikichukua muda wote wa siasa zetu, hata kusahahu kutatua matatizo ya ndani.

Kibaya zaidi, ilitumika kwa kuwachagulia wengine jinsi gani waendeshe nchi zao. Tukawa twawaunga mkono 'Wajamaa' akina Mugabe dhidi ya Abel Muzorewa na Nkomo, Neto dhidi ya Holden Roberto, Samora Machel dhidi ya Andre Matsangaisa na Afonso Dhlakama n.k.

Baya zaidi, diplomasia hiyo haikuwa na malengo ya kuleta faida za kiuchumi, isipokuwa kui 'bleed' tu Tanzania.

Hapana! Ninachokikusudia ni kuwa tuwe na diplomasia ya kuitangaza nchi yetu na kuwa shina la utatuzi wa matatizo ya Waafrika wenzetu. Kwa nini hatuanzi kwa kusuluhisha mgogoro wa Rwanda/Uganda, Rwanda/ DRC?

Unapojulikana Kimataifa, inakuwa rahisi pia kuwa na mahusiano ya kiuchumi, kibiashara, kiutalii, kitaaluma, kiutamaduni n.k.
NCHI IMEJICHOKA ILE MBAYA
 
Usifikiri Tanzania haina akili kutokwenda huko SA!
Hizo nchi ulizo zitaja ni wanafiki walio na degrees za utapeli mkubwa !
Kama kimekuudhi sana hamia katika hizo nchi na utuwache na Mama Tanzania wetu!
Midubwasha mingine bwana ni hovyo kabisa walahi!
 
Usifikiri Tanzania haina akili kutokwenda huko SA!
Hizo nchi ulizo zitaja ni wanafiki walio na degrees za utapeli mkubwa !
Kama kimekuudhi sana hamia katika hizo nchi na utuwache na Mama Tanzania wetu!
Midubwasha mingine bwana ni hovyo kabisa walahi!
Haya mambo ya kuambiana 'hamia huko' kila mtu anapotoa hoja ya kuonesha nchi nyingine zifanyavyo....yamekithiri mno. Nishaambiwa zaidi ya mara kadhaa.
Sijui Yarabbi Watanzania wana complex gani. Ukisema Kenya yafanya hivi, jitu litakwambia hamia huko!
Kwa kweli nadhani ni kukiri subconsciously kwamba ' basi tumeshindwa, hatuwawezi' halafu uvivu wa Kitanzania unaingia hapo na kuunganisha!
Hata Waziri aliwahi kuwaambia watu wahamie nchi nyingine! Na......akaachiwa!
 
Back
Top Bottom