Uzalendo wa Kitanzania
JF-Expert Member
- Mar 8, 2020
- 2,207
- 4,703
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar zimesaini mkataba wa makubaliano ya kuunganisha visiwa vya Pemba na Unguja na Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano
Utiaji saini huo umefanywa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Waziri Kindamba kwa upande wa Bara na Mhandisi Shukuru Awadh Suleiman, Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Miundombinu ya Tehama Zanzibar (ZICTIA) kwa upande wa Zanzibar
Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Mawasiliano), Dkt. Zainabu Chaula amesema Serikali ya Tanzania imejenga Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano kwa gharama ya zaidi ya shilingi bilioni 700 na kuunganisha kwenye mikoa yote 26 ya Tanzania Bara na kwenye nchi jirani za Congo, Zambia, Rwanda, Burundi, Kenya, Uganda na Malawi ambapo maunganisho haya yanaenda kufungua fursa za wawekezaji na watumiaji wa huduma za mawasiliano wa ndani na nje ya nchi
Naye Dkt. Mustafa Aboud Jumbe, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar amesema kuwa haya ndio matunda ya mapinduzi yanayopatikana katika nchi yetu.Amesema Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imetumia zaidi ya shilingi bilioni 30 kuunganisha mikoa na wilaya zote za Unguja na Pemba licha ya changamoto zilizokuwepo.
Utiaji saini huo umefanywa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Waziri Kindamba kwa upande wa Bara na Mhandisi Shukuru Awadh Suleiman, Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Miundombinu ya Tehama Zanzibar (ZICTIA) kwa upande wa Zanzibar
Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Mawasiliano), Dkt. Zainabu Chaula amesema Serikali ya Tanzania imejenga Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano kwa gharama ya zaidi ya shilingi bilioni 700 na kuunganisha kwenye mikoa yote 26 ya Tanzania Bara na kwenye nchi jirani za Congo, Zambia, Rwanda, Burundi, Kenya, Uganda na Malawi ambapo maunganisho haya yanaenda kufungua fursa za wawekezaji na watumiaji wa huduma za mawasiliano wa ndani na nje ya nchi
Naye Dkt. Mustafa Aboud Jumbe, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar amesema kuwa haya ndio matunda ya mapinduzi yanayopatikana katika nchi yetu.Amesema Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imetumia zaidi ya shilingi bilioni 30 kuunganisha mikoa na wilaya zote za Unguja na Pemba licha ya changamoto zilizokuwepo.