Dark City
JF-Expert Member
- Oct 18, 2008
- 16,252
- 11,649
Jana nilikuwa naongea na jamaa fulani kutoka UK ambao kwa namna fulani wanakabiliwa na changamoto za muungano zinazokaribia kufanana na zetu. Waliniuliza kwamba, endapo muungano ungefikia ukomo leo, wananchi wa bara wangependa kuendelea kuitwa Tanzania au kurejea jina la awali la Tanganyika?
Nilitoa maoni yangu nitayawasilisha hapo chini.
Wewe je ungependa jina lipi?
Binafsi ningependa tuendelee kuitwa Tanzania. Maoni yangu ni kama ifuatavyo.
1. Mimi ni miongoni mwa watu wengi waliozaliwa Tanzania. Siijui Tanganyika na itakuwa kama nabadilisha uraia ukubwani.
2. Katika matumizi ya kawaida, Tanzania imekuwa ikiwakilisha Tanzania bara na kwa hiyo itakuwa nimwendelezo wa kile kilichopo sasa.
3. Zanzibar wanaonekana kuridhia na kuridhika kuitwa hivyo badala ya Tanzania visiwani. Sidhani kama watakuwa na matatizo ya sisi kutumia tanzania ambayo ina neno Zanzibar ndani yake.
4. Sina hakika ila sidhani kama kutakuwa na matatizo ya kikatiba na kisheria endapo katiba itakayoundwa baada ya tukio hilo itatoa fursa hiyo kwa yeyote atakayetaka kuendeleza jina la Tanzania baada ya muungano kufikia ukomo wake!
Nilitoa maoni yangu nitayawasilisha hapo chini.
Wewe je ungependa jina lipi?
Binafsi ningependa tuendelee kuitwa Tanzania. Maoni yangu ni kama ifuatavyo.
1. Mimi ni miongoni mwa watu wengi waliozaliwa Tanzania. Siijui Tanganyika na itakuwa kama nabadilisha uraia ukubwani.
2. Katika matumizi ya kawaida, Tanzania imekuwa ikiwakilisha Tanzania bara na kwa hiyo itakuwa nimwendelezo wa kile kilichopo sasa.
3. Zanzibar wanaonekana kuridhia na kuridhika kuitwa hivyo badala ya Tanzania visiwani. Sidhani kama watakuwa na matatizo ya sisi kutumia tanzania ambayo ina neno Zanzibar ndani yake.
4. Sina hakika ila sidhani kama kutakuwa na matatizo ya kikatiba na kisheria endapo katiba itakayoundwa baada ya tukio hilo itatoa fursa hiyo kwa yeyote atakayetaka kuendeleza jina la Tanzania baada ya muungano kufikia ukomo wake!