Tani 20 za Pamba zataifishwa Bariadi

Tani 20 za Pamba zataifishwa Bariadi

Hii pamba inaonekana ilinunuliwa ki machinga kipindi mabank hayajaamuliwa kutoa pesa kwa wanunua pamba,
unakuta mkulima anashida mfano ana mgonjwa inabidi auze pamba kwa chinga ili apate pesa ya kutatua shida zake,
ila chinga nao wana roho ngumu sana maana mzigo kama huo kukamatwa ni hasara sana na kama mtu amekopa bank ndo mwanzo wa kushindwa kulipa deni,
hawa chinga ni wale wenye mitaji midogo mfano milioni 100,kwahiyo wao wananunua kwa mkulima mfano Tsh 800 na kwenda kuuza kwa mfanyabiashara mkubwa,wale wenye Ginnery kwa Tsh 1000,
anakula 200 kila kilo,
kiufupi hawa pia ni kagomba (walanguzi)
Ananunua Tani 20 = Tshs 16m
Anauza kwenye ginnery 20m
Faida ni 4m hii ni 25% ya capital
Is very good return!!
 
Hii pamba inaonekana ilinunuliwa ki machinga kipindi mabank hayajaamuliwa kutoa pesa kwa wanunua pamba,
unakuta mkulima anashida mfano ana mgonjwa inabidi auze pamba kwa chinga ili apate pesa ya kutatua shida zake,
ila chinga nao wana roho ngumu sana maana mzigo kama huo kukamatwa ni hasara sana na kama mtu amekopa bank ndo mwanzo wa kushindwa kulipa deni,
hawa chinga ni wale wenye mitaji midogo mfano milioni 100,kwahiyo wao wananunua kwa mkulima mfano Tsh 800 na kwenda kuuza kwa mfanyabiashara mkubwa,wale wenye Ginnery kwa Tsh 1000,
anakula 200 kila kilo,
kiufupi hawa pia ni kagomba (walanguzi)
Na kama wenye Ginnery ndio wanunuzi kupia ndugu zao. Risk ya kukamatwa na kutaifishwa ni ndogo!

Mfano, akitumia watu kinunua kwa Tshs 600 ni 12m
Lakini akinunua kwenye vyama vya ushirika atalipa zaidi ya 24m. Akifanikiwa trip moja hata nyingine akikamatwa bado haija affect mtaji wake!
 
Wasamehewe kwa kulipa bei halisi kwa wakulima,kutaifisha ni kuwadhulumu wafanyabiashara walioelewana na wakulima.
Taratibu zifuatwe ili mkulima apate fedha zake kwa wakati bila kuathili bei elekezi,wafanyabiashara nao wasijifanye wanyonyaji ni heri wapate faida ya 25-75/= kwa kilo ili waweze kukidhi gharama za usafiri na mishahara kwa wanunuzi wao.
 
Bora hiyo 800 ya papo kwa papo kuliko hiyo 1200!!ya baada ya miezi nane!! Toka mwezi wa tano wakulima walivuna pamba wakakataa kulipwa hiyo 1000,wakitaka walipwe 1200!!wakaiweka ndani wakati huo gunia la mahindi (katavi) lilikuwa likiuzwa elfu 25! Leo wanakopwa kwa 1200,gunia la mahindi ni elfu 55!!hapo nani bwege? Nfra wananunua mahindi kwa kilo shilingi500!! Nani akakopwe bora mtu auze kilo kwa shilingi 400!!ya hapo hapo.
Serikali siyo kitu cha kubebembeleza mtu! Tatizo ni hao wafanyabiashara. Tunawategemea wawe ni watu wa kiwango fulani cha ufahamu. Wana leseni na ni wataalamu wa masoko ya zao hilo. Kwa nini wajiingize kwenye biashara haramu wakati wana leseni. Let them suffer. Hatuhitaji kuhesabu shida za wakulima kwa manufaa ya wafanyabiashara.

Upuuzi huu ndo unapelekea watu duni kututawala miaka yoote. Tunawaruhusu wapate pesa za wizi halafu wanaanza kutupangia maisha yetu.
 
Serikali siyo kitu cha kubebembeleza mtu! Tatizo ni hao wafanyabiashara. Tunawategemea wawe ni watu wa kiwango fulani cha ufahamu. Wana leseni na ni wataalamu wa masoko ya zao hilo. Kwa nini wajiingize kwenye biashara haramu wakati wana leseni. Let them suffer. Hatuhitaji kuhesabu shida za wakulima kwa manufaa ya wafanyabiashara.

Upuuzi huu ndo unapelekea watu duni kututawala miaka yoote. Tunawaruhusu wapate pesa za wizi halafu wanaanza kutupangia maisha yetu.
Umezoea kushika rungu,na kutisha nalo watu ukadhani ni akili ya uongozi.
Wenye akili hawatumii nguvu wanatumia akili kuendesha nchi
 
Serikali haina pesa ya kununua Pamba ndiyo sababu walanguzi wamejitokeza kwa wingi msimu huu wa kununua Pamba katika mikoa mbali mbali nchini kuwalalia Wakulima. Halafu bado anajiita Rais wa wanyonge!!! Si ajabu mazao yote haya mawili makubwa ya biashara yakajifia na wa kulaumiwa ni nduli na sera zake MUFILISI za kutumia trillions kwenye mambo yasiyo na tija kwa Taifa na kushindwa kufanya yale ambayo ni vipaumbele kwa Taifa kama kuhakikisha kununua mazao ya wakulima nchini iwe ya biashara au ya chakula.

cd0d582c66482e5b0d2486177a9e816c

Gari aina ya scania iliyokamatwa na pamba hiyo
Derick Milton, Simiyu

Zikiwa zimepita siku kumi tangu Mkuu wa Wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu Festo Kiswaga, ataifishe tani 26 za pamba iliyodaiwa kununuliwa kwa njia ya machinga, leo Jumamosi Agosti 24, Mkuu huyo wa Wilaya ametaifisha pamba nyingine tani 20.

Akiongea na waandishi wa habari Kiswaga amesema kuwa pamba hiyo imekamatwa katika kijiji cha Igegu kata ya Sapiwi majira ya saa 5 asubuhi ikiwa imepakiwa kwenye gari aina ya scania yenye namba za usajili T 729 ARN.

Amesema kuwa kupitia kikosi kazi ambacho alikiunda cha kupambana na watu wanaonunua pamba kwa njia ya machinga, gari hilo baada ya kukamatwa dereva aliweza kukimbia kusikojulikana.

“Kikosi kazi hiki baada ya kukamata, kilikuta pamba haina kibali chochote na haikujulikani wapi inaenda, nani mmliki wake, na hata gari halijajulikana ni mali ya nani,” amesema Kiswaga.

cd0d582c66482e5b0d2486177a9e816c-1

Amesema kuwa ilibainika kuwa pamba hiyo ilikuwa inanunuliwa kwa njia za machinga, ambapo wakulima walikuwa wakinunuliwa kwa sh.600 hadi 800 kutoka katika kijiji hicho.

“Baada ya kubaini hivyo nimeamua kuitaifisha pamba hii na tutaenda kuiuza leo kwenye kiwanda cha kuchambua pamba chochote na pesa yote ambayo itapatika tutaipeleka katika kukamilisha ujenzi wa vyumba vya madarasa shule ya msingi Igegu,” amesema Kiswaga.

Aidha amewaonya viongozi wa Vyama vya Msingi vya Ushirika (Amcos) ambao wamekuwa wakishirikiana na makampuni kununua pamba kwa njia ya umachinga kuwa watakamatwa na kuchukuliwa hatua.
 
Umezoea kushika rungu,na kutisha nalo watu ukadhani ni akili ya uongozi.
Wenye akili hawatumii nguvu wanatumia akili kuendesha nchi
Tulia bhana!! Ukitulia utajifunza, ukijidai unazo hutaelewa.
Serikali gani duniani haina Jeshi na polizi? Ipo?? umewahi sikia wapi? Akili, akili wapi? Akili kwa watu wapuuzi!
 
Na bado uchaguzi umekaribia hapo ndipo napojua wabongoo ni binadamu wa aina gani
 
Hii ni dhambi kubwa sana, mkulima aliuza pamba yake hata kwa bei ndogo baada ya kukubaliana na mnunuzi kwa hiari yao wenyewe ili mkulima akamalize shida zake, yeye anapotaifisha pamba na gari ya mnunuzi aliyemsaidia mkulima kwa kununua pamba yake ili akamalize shida zake, yeye kama yeye aliyetaifisha pamba na gari ndo amewasaidia wakulima?.
 
cd0d582c66482e5b0d2486177a9e816c

Gari aina ya scania iliyokamatwa na pamba hiyo
Derick Milton, Simiyu

Zikiwa zimepita siku kumi tangu Mkuu wa Wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu Festo Kiswaga, ataifishe tani 26 za pamba iliyodaiwa kununuliwa kwa njia ya machinga, leo Jumamosi Agosti 24, Mkuu huyo wa Wilaya ametaifisha pamba nyingine tani 20.

Akiongea na waandishi wa habari Kiswaga amesema kuwa pamba hiyo imekamatwa katika kijiji cha Igegu kata ya Sapiwi majira ya saa 5 asubuhi ikiwa imepakiwa kwenye gari aina ya scania yenye namba za usajili T 729 ARN.

Amesema kuwa kupitia kikosi kazi ambacho alikiunda cha kupambana na watu wanaonunua pamba kwa njia ya machinga, gari hilo baada ya kukamatwa dereva aliweza kukimbia kusikojulikana.

“Kikosi kazi hiki baada ya kukamata, kilikuta pamba haina kibali chochote na haikujulikani wapi inaenda, nani mmliki wake, na hata gari halijajulikana ni mali ya nani,” amesema Kiswaga.

cd0d582c66482e5b0d2486177a9e816c-1

Amesema kuwa ilibainika kuwa pamba hiyo ilikuwa inanunuliwa kwa njia za machinga, ambapo wakulima walikuwa wakinunuliwa kwa sh.600 hadi 800 kutoka katika kijiji hicho.

“Baada ya kubaini hivyo nimeamua kuitaifisha pamba hii na tutaenda kuiuza leo kwenye kiwanda cha kuchambua pamba chochote na pesa yote ambayo itapatika tutaipeleka katika kukamilisha ujenzi wa vyumba vya madarasa shule ya msingi Igegu,” amesema Kiswaga.

Aidha amewaonya viongozi wa Vyama vya Msingi vya Ushirika (Amcos) ambao wamekuwa wakishirikiana na makampuni kununua pamba kwa njia ya umachinga kuwa watakamatwa na kuchukuliwa hatua.
wakulima waliouza pamba walilalamika kuwa wameibiwa?au ni kiherehere tu cha kujipendekeza?.
 
Kuna mdg wangu alilima pamba nadhani hatarudia, kwanza vitu vingine ni kujitakia tu unatumia 120000 kwa heka unakuja kuuza 200000 faida 80000 plus mateso ya kuamka sa11 kwa almost 5 months
 
Back
Top Bottom