Salaam JF.
Sasa kuna huyu shemeji yenu na wifi yenu hapa ambaye ana ujauzito wa miezi 7 sasa hivi.
Sijamuoa ila naishi nae na natarajia kumuoa panapo majaaliwa.
Tatizo lililofanya nije kwenu ni kwamba huyu mpenzi kwa kweli amekuwa na kiburi sana, na hataki kabisa tufanye mapenzi, yaani mpaka kwa mbinde tena mara moja kwa mwezi tangu amebeba ujauzito na nikipiga moja tu hataki kabisa kuendelea tena wakati mwingine hata kabla sijashusha yeye hataki visingizio vingi mara utamuumiza mtoto etc, wakati ana miezi miwili alipata kajitatizo akaambiwa apumzike kwa wiki moja sasa ndio imekuwa sababu kwa kweli, hataki nimguse kabisa tukilala yaani yeye kule mimi kule, nilianza kuishi nae miezi miwili kabla hajabeba ujauzito na kwa kipindi hicho tulikuwa tunafanya kila siku karibia.
Sasa nashindwa kuelewa kwamba ujauzito ndio ufanye akose namna ya kuishi ki romantic na mimi? Yaani mpaka natamani nighairi kumuoa ingawa nishatoa mahali kwao tayari maana naogopa isije ikawa ndivyo maisha nitakayokuwa nikiishi baada ya kumuoa.
Nikipata nafasi ya kufanya huwa namuandaa kabisa mpaka nahakikisha anaililia mwenyewe lakini kwa sasa ndio hivyo hataki nimsogelee, anachowaza yeye ni shela zuri na ukumbi mzuri na sherehe nzuri ya harusi, mambo ya nyumbani ukimwambia kisingizio ni ujauzito alio nao, hapiki wala kufua wala kufanya kazi za nyumbani, mara moja moja mpaka nimseme ndio ataanza kufanya kazi ndogo ndogo, wazoefu naomba mniambie, huyu ni huu ujauzito ndio unasababisha haya au anawezekana anasingizia ujauzito?
Maana kazini anaenda na anafanya kazi kama kawaida, na mimi kila siku nampekeka na gari langu na kumuonesha kuwa namjali kwa pale niwezapo, yaani nikimwambia nina ugwadu hataki anasema kwa sasa kwa kweli utanisamehe, na hata siku moja alishawai kuniambia nikapige puli kama nimezidiwa.
Nishaurini wakuu kabla sijafanya maamuzi magumu.