Tangazo kwa UKAWA wote



Usiwatafutie Ban watu bure!
Mie nilidhani tangazo la maana kumbe porojo!
Angalia picha kubwa na siyo hesabu hizi za akina S.Sita,wacha wafanye lao,hujui kuwa hawajaanza leo kuiba kura?

Ubungo,Kawe,Arusha,Mbeya,Iringa,n.k watu walilinda kura zao na matokeo huhitaji Mganga wakienyeji kukutabiria.

Wito wangu kwa UKAWA; Andaeni Kijitabu,na kuisambaza Kila Kata kuhusiana na Uchakachuaji huu wa Rasimu ya Warioba ambayo msingi wake ni Maoni ya Wananchi.Na baada ya hapo uhamasishaji kupitia mikutano ya hadhara ufuatie nyuma yake;Ukombozi hauko mbali na ni suala la muda tu.


Mfano.Kijitabu.


Rasimu ya Warioba;c/o Maoni ya Wananchi
Bunge maalum la CCM;imebakiza au Kufutwa Rasimu ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba/Maoni ya Wananchi
Rasimu ya Chenge na Kamati yake C/O Sita wanapendekeza
Ibara 1..............................................
1. Imefutwa
......................................
2.;.........................................

2.Imefutwa
...................................



CC. UKAWA Kurugenzi ya Habari

 
Last edited by a moderator:
Hapa ninachosema ni ukweli mtupu hata kama mchungu, kwetu Tanzania kura ya HAPANA na ndiyo yote sawa. Nani atalinda kura nchi nzima wakati wameshindwa kulinda za watu wao 67, tell me, Mie nasema UKAWA wanyamaza kimya
 
UKAWA wameshindwa kusoma picha ndogo ya watu 67, wataweza kusoma picha kubwa ya watu mioni tano na zaidi. Bora upigwe Ban, lakini leo nitawapa ukweli UKAWA, wakitaka wameze, wakitaka wateme shauri yao. Tena nasema waufyate.
 
Nikisemaga nchi hii wapinzani mtasubiri saaaana mnanikoromea hizi ni enzi za money power zama za people's power zilishapitaga
 
Nikisemaga nchii wapinzani mtasubiri saaaana mnanikoromea hizi ni enzi za money power zama za people's power zilishapitaga
There you are. Wao wanajua watu wao wanatafutwa, it was very simple, kuapa kisheria na kutangaza hadharani kuwa hakuna atakayepiga kura, na kuwa wote hawaungi mkono katika ya CCM. Sasa wao walisubiri wapewe kwenye sahani katiba ya wananchi wakati CCM wanasema wanataka kutawala Tz hadi wahakikishe wamekomba raslimali zote za nchi.
 
Mkuu pole ila relax.
 
Mkuu pole ila relax.
Wacha niwaambie ukweli UKAWA, labda nita-relax. Kiukweli wamekera mno, wameudhi kwa kutokuwa strategic kulinda kura zao 67. Habu fikiria, wameshindwa kulinda kura za wajumbe wao 67, kisiasa na kisheria, watawezaje kulinda kura za HAPANA za mamilioni ya watanzania. Hakuna mantiki yoyote hapa, wanyamaze tu, hiyo ya kusubiri kura za wananchi ni very low idea, it is not an option, wameshindwa tayari.
 

Hivi kila kitu wafanye Ukawa? wewe na mimi jukumu letu ni lipi? Ukawa wamefanya walichoona kufanya kwa wakati ule, sasa swali kwako umefanya nini kuhakikisha unapata katiba bora? Kumbuka hii ni Tanzania yangu na wewe sio ya Ukawa tu.....Watanzania tuache mawazo mgando kila kitu ni Ukawa, Je wewe umefanya nini?
 


Hivi ni nani aliyekwambia kura 67 za Ukawa zimeibiwa? tuanze hapo kwanza
 
mmhh! Mie siamini kama kuna kitu ambacho UKAWA wangefanya eti kizuie Katiba kupita. Mnawonea bure UKAWA, wamejitahidi kadri ya uwezo wao. Mie nilifikiri sasa mtaelewa kwanini walitoka bungeni badala ya kubaki wakipambana humo humo!!
 
Hivi ni nani aliyekwambia kura 67 za Ukawa zimeibiwa? tuanze hapo kwanza
Amavubi usiukimbie ukweli. Bila kuibiwa kura za ukawa hakuna 2/3 ya kutoka Zanzibar. CCM wamefanikiwa kuiba kura za UKAWA ndiyo wametangaza kupita kwa rasmu, iko wazi mbona. Nimeshasema hapo juu kuwa kama UKAWA wangechukua kiapo cha kisheria ambacho wangefanya kirahisi tu, na kutangazia umma kuwa kiapo walichochukua ni kuwa hawatapiga kura kwa sababu hawaiungi mkono, na kiapo kingeeleza kuwa kama wangepiga kura ni HAPANA. Haujui kuwa kura za UKAWA zimetumika kuchakachua kupitisha katiba ya CCM?
 
mmhh! Mie siamini kama kuna kitu ambacho UKAWA wangefanya eti kizuie Katiba kupita. Mnawonea bure UKAWA, wamejitahidi kadri ya uwezo wao. Mie nilifikiri sasa mtaelewa kwanini walitoka bungeni badala ya kubaki wakipambana humo humo!!
Hivi ni ngumu kuelewa kuwa kiapo cha kisheria kingesaidia kueleza kuwa hawatapiga kura na kama wangepiga ni hapana. Walifanya hili? Ilikuwa ni lazima UKAWA kuwa strategic na kuzuia loop hole yoyote ya kuchakachua kura. Sasa wanatuambia wanasubiri kura za wananchi, watalinda kura za hapana za wananchi wakati wameshindwa kulinda kura zao 67
 

Kwani ukawa waliopiga kura wametajwa majina kwa sababu sheria ni kwamba kila mjumbe anaitwa jina na anapiga kura ya siri au wazi
 

UKAWA walijua anything can happen kwa hiyo acha kujikomba. Walijua waliobaki bungeni ndio marefa na ndio wachezaji.
 
ni muda gani watakuwa na fikra hizo? wao wanataka siasa za kusifiwa na kuonekana itv. toka mwanzo sikukubaliana na uamuzi wa kutoka mle ndani,nadhani kuna udikteta kwa wenyeviti na makatibu wakuu waliolazimisha jambo hili la kutoka,kama kuzomea na matusi wote walifanya,kama kauli ya lukuvi hata wao wana kauli mbovu nyingi tu zaidi ya wanawaita intarhamwe,ni upuuzi tu huu
 
TE=Stabilaiza;10769483]Hivi ni ngumu kuelewa kuwa kiapo cha kisheria kingesaidia kueleza kuwa hawatapiga kura na kama wangepiga ni hapana. Walifanya hili? Ilikuwa ni lazima UKAWA kuwa strategic na kuzuia loop hole yoyote ya kuchakachua kura. Sasa wanatuambia wanasubiri kura za wananchi, watalinda kura za hapana za wananchi wakati wameshindwa kulinda kura zao 67[/QUOTE]

Sasa niambie ni wapi na lini mwana ukawa amepiga kura na zikaibiwa?

Halafu nimekuuliza hii ni katiba ya watanzani ukiwemo na wewe au ni kjatiba ya ukawa?
Na kama ni katiba ya watanzania wewe umefanya nini kuakikisha unapata katiba bora?
Na ni wapi na Lini uliambiwa jukumu la kulinda kura ni la Ukawa?
 

Mimi nilipoona Mbatia kajiunga na UKAWA nikajua basi atawavuruga tu..na kawavuruga kweli
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…