TANESCO yalia ukata na madeni. Yaomba serikali (walipa kodi) wawabebe deni la tril 1.39 wanalodaiwa na IPTL, Songas na TPDC

Serikali imeombwa kubeba deni la shilingi trilioni 1.39 ambalo Shirika la Umeme nchini(Tanesco), linadaiwa na taasisi mbalimbali ikiwamo watoa huduma wake na mabenki. Katika deni hilo, shilingi bilioni 950, zinadaiwa na watoa huduma ikiwamo kampuni ya IPTL, Songas Pan Africa na TPDC, huku shilingi bilioni 442, zikiwa ni za mkopo wa benki kwa matumizi mbalimbali.

Mkurugenzi wa Tanesco, Dk.Tito Mwinuka, amesema shilingi bilioni 408 zilizokopwa kutoka benki zilitumika kununulia mafuta mazito ya kuendesha mitambo ya kufua umeme, na shilingi bilioni 34 zilitumika kulipa fidia ya ujenzi wa ilani kutoka Somangafungo hadi Kinyerezi.#KwanzaHabari

Reality strikes!

These motherfuckers are coming outta woodworks now!
 
Hawa jamaa si wanauza umeme? Inawezekana TTCL nao wana madeni yao kibao wanawasikilizia TANESCO.

Mtu huna mpinzani ila unashindwa tengeneza fedha. Mpeni mzungu Hilo shirika na mumpe Target. Hao wakugenzi mnaowapa wanatakiwa wawe chini ya mzungu.
Kisa mtu anajua V= IR Mnamkabidhi Tenesko(in Sakaya voice)
Tatizo ni CCM na ufisadi wake na Wala si watendaji wa Tanesco
 
Mkuu huoni wamekukata 5,000 kwenye deni lako la zamani la shilingi 34,697.64 na sasa bado unadaiwa 29,697.64?
Deni limetoka wapi na document zote za kunifungia LUKU na mkataba wao sikuwa na daiwa hata shiling sasa leo ndo nashangaa. Ni sawa sawa na kipindi kile nikiwa tariff 4 na umeme wa 8,000 nilikuwa nautumia kwa mwezi na wiki mbili lakini ghafla bin vuu nilienda nunua umeme nikashangaa nikapewa namba nyingi nyingi nikahamishiwa tariff 1 bila taarifa. Angalia na leo nina deni nimewaambia wanionyeshe nilikuwa nadaiwa lini na wapi wamekosa jibu.

Ndo hivyo subiri dawa nayo inakuja kwenu wacha watukomeshe sisi wa Moshi kesbo ni nyinyi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo ni CCM na ufisadi wake na Wala si watendaji wa Tanesco
Kwahiyo haiwezekani mtendaji wa Tanesco akawa CHADEMA??,, Kiukweli nachukia watu ambao huwa hawatumii akili (LOGIC) kabisa, kwahiyo kama CHADEMA ingekuwa madarakani watumishi ingewatoa mwezini?, matatizo na ufisadi sio swala la vyama, wananchi ni hawa hawa na hulka ni hizi hizi hata kije chama gani mtu mweusi ana asili ya udokozi na ubinafsi(kujilimbikizia Mali),mtu yeyote ambaye huwa anatanguliza mambo ya vyama akidhani kuna chama kina watu ambao ni binadamu tofauti huwa sipepesi macho kumuita MPUMBAVU.
 
Posti 19 kuna jibu lako kule chini

Sent using Jamii Forums mobile app
Nimekuelewa mkuu, maana yake ni kwamba umebambikiwa deni na hujui limetoka wapi, ungekuwa na risiti za manunuzi matatu mfululizo ungeenda nayo wakuonyeshe ni wapi hasa deni limeanza kuhesabiwa na linatoka wapi. TANESCO mje kujibu hizi allegations, mnadhulumu watu haki zao kwa sababu gani...
 
Kwahiyo haiwezekani mtendaji wa Tanesco akawa CHADEMA??,, Kiukweli nachukia watu ambao huwa hawatumii akili (LOGIC) kabisa, kwahiyo kama CHADEMA ingekuwa madarakani watumishi ingewatoa mwezini?, matatizo na ufisadi sio swala la vyama, wananchi ni hawa hawa na hulka ni hizi hizi hata kije chama gani mtu mweusi ana asili ya udokozi na ubinafsi(kujilimbikizia Mali),mtu yeyote ambaye huwa anatanguliza mambo ya vyama akidhani kuna chama kina watu ambao ni binadamu tofauti huwa sipepesi macho kumuita MPUMBAVU.
Dah, kiongozi umeandika vizuri hadi naona like pekee haitoshi. Watu wanadhani hulka za mtu aliyeko CCM leo zipo tofauti na aliyeko CDM. Wasijue kuwa ubinafsi na ulafi imekuwa ndio utamaduni wa mtu mweusi. Watu hatupendi kushirikisha bongo zetu hata kidogo.
 
Hivi hili shirika limewahi kujiendesha kwa faida?

TANESCO
ATCL
TTCL

Haya mashirika yanavyotufanya Watanzania anajua Ngosha mwenyewe.!

Sent using Jamii Forums mobile app
Shida 10% angalia hizo kampuni zinazodai zinaiuzia Tanesco unit zaidi ya 300 alau tanesco wanakuja kuuza 250 wapate wapi faida..! Serikali yeyenyewe ina miaka 2 sasa haijapa Tanesco Ruzuku wameambiwa wagangamae na Sembuse ule mradi wa Rufiji ukiisha sijui kama ao Songas, IPTL kama wataendelea na Tanesco tena
 
Serikali imeombwa kubeba deni la shilingi trilioni 1.39 ambalo Shirika la Umeme nchini(Tanesco), linadaiwa na taasisi mbalimbali ikiwamo watoa huduma wake na mabenki. Katika deni hilo, shilingi bilioni 950, zinadaiwa na watoa huduma ikiwamo kampuni ya IPTL, Songas Pan Africa na TPDC, huku shilingi bilioni 442, zikiwa ni za mkopo wa benki kwa matumizi mbalimbali.

Mkurugenzi wa Tanesco, Dk.Tito Mwinuka, amesema shilingi bilioni 408 zilizokopwa kutoka benki zilitumika kununulia mafuta mazito ya kuendesha mitambo ya kufua umeme, na shilingi bilioni 34 zilitumika kulipa fidia ya ujenzi wa ilani kutoka Somangafungo hadi Kinyerezi.#KwanzaHabari
Haya yote ni kwa sababu weledi na uaminifu TANESCO inaelekea hakuna.Anyway,kabla serikali haijaingilia kati,CAG apewe kazi ya ku-audit TANESCO kwa ujumla wake,ili kujirishisha kwamba hakuna ufujaji na matumizi mabaya ya fedha za shirika.Kama kuna matumizi mabaya ya fedha wahusika wote wachukuliwe hatua stahiki.
 
Back
Top Bottom