TANESCO yacharuka! Hamisha hamisha yaanza

TANESCO yacharuka! Hamisha hamisha yaanza

Aaaa mkuu uwe unaoanisha bana kichwa cha habari na maelezo yako! Yani mimi nilipoona kichwa cha habari tu nikadhani kuna majipu yametumbuliwa lakini wapi, daaaaah nimekwazika sana mkuu!
 
Sio kuhamishwa peke yake, ufanisi nao uongezeke, kuna suala la mita( lowvolteg) ni kero ya kutosha, umeme unawaka kwa jirani mpaka amalize shughuli zake ndio kwako uwake, hapa arusha ni kero sana hii kitu..!!
 
Mkuu, hoja yako ina mashiko ila, Tunahitaji wataalamu wa nje/ independent hydrologist kuchunguza flow mita za kabla maji kuingia Mtera, levels at dam, bypass, flow downstream before Kidatu na correlation ya before Kidatu na downsteam, Hili litaondoa kiwingu na kuipa haki TANESCO. Pia weKeni CCTV cameras kumonitor water gates. Mashamba ya mpunga mengi upstream yamedoda, uzalushaji mdogo na bado umeme tabu.
nafkiri mawazo yako ni ya msingi sana kama serikali wangekuwa wanapita kwenye majukwaa kama haya wangepata pa kuanzia big up!
 
Tanesco yacharuka! Hamishahamisha yaanza

Habari za uhakika tulizozipata kutoka kwa mdau wa ndani ya shirika la umeme nchini TANESCO zinasema kwamba pamekuwa na mtikisiko mkubwa wa mameneja na maofisa waandamizwi kuhamishwa vituo, zoezi linalosemekana lina nia ya kuboresha huduma na kuimarisha ufanisi.

Kwa mujibu wa chanzo hicho cha habari miongoni mwa maofisa wanaohamishwa ni pamoja na mameneja wa mikoa ya morogoro na arusha waliokuwa wanalalamikiwa kwa matatizo ya mita katika mikoa hiyo.

Wengine ni mameneja wa mikoa ya Manyara, Lindi, Tabora na Temeke.

Pia inasemekana shirika hilo limeunda tume ya kuchunguza tuhuma za kufunguliwa maji katika bwawa la Mtera. Pia chanzo chetu kinaonyesha kwamba wakuu wote wa vituo vya kuzalisha umeme wamehamishwa vituo.

Lets be serious, Rais alishasema mtu akivurunda sehemu moja, hakuna kuhamishwa-badala yake ni kufukuzwa tu. Hii hamisha hamisha ni kupuuzwa kwa agizo la Rais.
 
Kwani tatizo kukatika umeme ni la Mameneja?

Nona wanataka tu kumchanganya Magufuli, Uzuri Magufuli anajua kuliko wao!
 
yaani badala ya kutimuliwa wanahamishwa...kwa hiyo wanahamisha matatizo toka Morogoro na Arusha kwenda sehemu zingine
Kwanza huyo meneja Wa ARUSHA mwezi Wa 3 Leo naendaga hapo .naambiwa amesafiri Mara yuko site Mara Yuki dar.yaani kwa ujumla ni ajafika ofisini mwezi Wa 3 Leo.
 
mimi nadhani mtendaji mkuu wa tanesco ameshindwa kusimamia shirika na ndiye anastahili kumulikwa na raisi maana meneja analalamikiwa kwa matatizo badala ya kumshusha cheo au kumuondoa eti unamhamisha sasa maana yake matatizo yake ayapeleke huko ulikompeleka?

utaoreshaje shirika kwa kubadilisha watu waaoshindwa kazi?

aliyeko mfano lindi analalamikiwa kwa matatizo ya mita na aliyeko manayara analalamikiwa kwa matatizo hayohayo sasa unamchukua wa lindi unamuamishia manyara na wa manyara unamuamshia lindi ??????

Tanesco yacharuka! Hamishahamisha yaanza

Habari za uhakika tulizozipata kutoka kwa mdau wa ndani ya shirika la umeme nchini TANESCO zinasema kwamba pamekuwa na mtikisiko mkubwa wa mameneja na maofisa waandamizwi kuhamishwa vituo, zoezi linalosemekana lina nia ya kuboresha huduma na kuimarisha ufanisi.

Kwa mujibu wa chanzo hicho cha habari miongoni mwa maofisa wanaohamishwa ni pamoja na mameneja wa mikoa ya morogoro na arusha waliokuwa wanalalamikiwa kwa matatizo ya mita katika mikoa hiyo.

Wengine ni mameneja wa mikoa ya Manyara, Lindi, Tabora na Temeke.

Pia inasemekana shirika hilo limeunda tume ya kuchunguza tuhuma za kufunguliwa maji katika bwawa la Mtera. Pia chanzo chetu kinaonyesha kwamba wakuu wote wa vituo vya kuzalisha umeme wamehamishwa vituo.
 
Hao peleka HQs, wakae kijiweni kama miaka 5 hivi! No marupurupu no what!
Chukua vijana graduates(UDSM only) watapewa ushirikiano mzuri tu! Kwa sababu watendaji si wao!
 
Back
Top Bottom