TANESCO yacharuka! Hamisha hamisha yaanza

TANESCO yacharuka! Hamisha hamisha yaanza

pinpilojr

Member
Joined
Jul 8, 2015
Posts
59
Reaction score
10
Tanesco yacharuka! Hamishahamisha yaanza

Habari za uhakika tulizozipata kutoka kwa mdau wa ndani ya shirika la umeme nchini TANESCO zinasema kwamba pamekuwa na mtikisiko mkubwa wa mameneja na maofisa waandamizwi kuhamishwa vituo, zoezi linalosemekana lina nia ya kuboresha huduma na kuimarisha ufanisi.

Kwa mujibu wa chanzo hicho cha habari miongoni mwa maofisa wanaohamishwa ni pamoja na mameneja wa mikoa ya morogoro na arusha waliokuwa wanalalamikiwa kwa matatizo ya mita katika mikoa hiyo.

Wengine ni mameneja wa mikoa ya Manyara, Lindi, Tabora na Temeke.

Pia inasemekana shirika hilo limeunda tume ya kuchunguza tuhuma za kufunguliwa maji katika bwawa la Mtera. Pia chanzo chetu kinaonyesha kwamba wakuu wote wa vituo vya kuzalisha umeme wamehamishwa vituo.
 
Hii nchi vitu havifanyiki kwa utaratibu bila kutaitiwa
 
Ahamishwe na meneja wa mbeya kwa kuwa ameifanya ofisi yake kama mali yake. Pia na secretary wake aondoke, kwani ndiye anayekataa katakata watu kumwona meneja!:lock1::lock1:
 
yaani badala ya kutimuliwa wanahamishwa...kwa hiyo wanahamisha matatizo toka Morogoro na Arusha kwenda sehemu zingine
 
kibila njoo huku usikie kuhusu meneja wa tanesco Morogoro
 
Last edited by a moderator:
Hiyo ishu ya mabwawa hata Ewura wanahusika. Ngoma ilianzia Symbion ndio waliowashawishi maofisa wa Tanesco na Ewura.. Ili ionekane umeme umepungua jamaa wawashe mitambo ya Gesi waanze kupiga pesa
 
Sio kweli maneja wa Temeke kahamishwa, meneja wa Temeke alifariki hivi karibuni, mmiliki wa bendi ya Fm Academia. Kwa hiyo temeke wameteua meneja mpya sio kuhamisha.
 
Tanesco yacharuka! Hamishahamisha yaanza

Habari za uhakika tulizozipata kutoka kwa mdau wa ndani ya shirika la umeme nchini TANESCO zinasema kwamba pamekuwa na mtikisiko mkubwa wa mameneja na maofisa waandamizwi kuhamishwa vituo, zoezi linalosemekana lina nia ya kuboresha huduma na kuimarisha ufanisi.

Kwa mujibu wa chanzo hicho cha habari miongoni mwa maofisa wanaohamishwa ni pamoja na mameneja wa mikoa ya morogoro na arusha waliokuwa wanalalamikiwa kwa matatizo ya mita katika mikoa hiyo.

Wengine ni mameneja wa mikoa ya Manyara, Lindi, Tabora na Temeke.

Pia inasemekana shirika hilo limeunda tume ya kuchunguza tuhuma za kufunguliwa maji katika bwawa la Mtera. Pia chanzo chetu kinaonyesha kwamba wakuu wote wa vituo vya kuzalisha umeme wamehamishwa vituo.

daah, nikadhani wamecharuka na kuanza kuzalisha umeme kwa ufanisi bila upuuzi wao wa kukata-kata umeme hovyo bila maelezo
 
Hakuna kitu, wanajaribu kuficha ukweli hawa lakini rais anazo zote a-z ...ngoja aje mwenyewe watajuta.
 
Nyoooo.. walikua wapi siku zote...wasubirI MAGUFULI aje awatumbue majipu....hawawez mkwepa..kwanza na hizi mita zao mpya za umeme za luku zichunguzwe nahis ni mrad wa mtu fulani...kwanza vimeo...pili unawekewa tariff za viwandani nyumbani.hela kila siku kununua umeme.kubadilishiwa issue..mpk hongo au ukae miez sita...
 
Tulishasema hakuna mtu kuhamishwa.., ni kusimamishwa kazi ili kupisha uchunguzi
 
mimi siafiki hamisha hamisha.. sababu wanajihami, tochi ya magufuli ikipita ikikuta uozo watasema" tumeshawawajibisha" wakati mtu katoka ofisi moja na anaenda endeleza uozo ofisi nyingine
haya mambo ya kubebana bebana na kuoneana aibu hayatakiwi. kama mtu ni mwizi , mhujumu shirika, mvivu , hafanyi kazi kwa weledi apate adhabu inayostahiki iwe ni kuwekwa kando , uchunguzi ufanyike. kama wa kuonywa au kufukuzwa kazi au kupelekwa lupango na ifanyike hivyo.. kila mtu ahukumiwe anavyostahili kuhukumiwa. sio kuhamishwa kituo..:angry:
 
Back
Top Bottom