TANESCO wanaidai Zanzibar bilioni 106

TANESCO wanaidai Zanzibar bilioni 106

Tulimumu

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2013
Posts
14,395
Reaction score
13,266
Kwenye taarifa ya habari ya ITV tarehe 11/03/2016 niliona wakati EWURA wakijadili ombi la TANESCO kutaka kushusha bei ya umeme wakisema wadeni wakubwa wa TANESCO ni pamoja na Zanzibar inayodaiwa zaidi ya Shilingi bilioni 106, serikali (nadhani walimaanisha Tanganyika) wanaidai bilioni 33 na watu binafsi bilioni kadhaa.

Hapo ndipo niliposhangaa kuwa kwa deni lote hilo kwanini TANESCO hawaikatii umeme Zanzibar kama wanavyokata kwa watu binafsi wanaodaiwa sana sana elfu au laki kadhaa.

Vile vile nikashangaa kuwa baada ya kupindua uchaguzi wa wananchi katika uchaguzi wa Decemba mwaka jana wanaitisha uchaguzi mwingine utakogharimu zaidi ya bil 4 wakati tayari wameshasema liwake jua au mvua inyeshe lazima wao watawale kwanini wasingetumia hizo pesa kupunguza deni la TANESCO?
 
Watu hawalipishwi umeme kama mkakati wa kupata kura,matokea Tanganyika tunawalipia kwa ongezeko la tozo
 
Halafu bado wanasema Tanganyika inawanyonya, mimi naona kama Wazanzibar wamevimbiwa dezo dezo. !
 
Dawa yao ni kubadili utaratibu tu,wawe wanalipia kabla ndo wapate huduma halafu walipe kwanza 3/4 ya deni ndo waendelee kupata huduma otherwise wawashe mishumaa.
 
Jamani msije mkatutenga wazenji.. Hatunza vyanzo vya kuzalisha umeme.. Hayo madeni watanganyika watatusaidia kwenye ushuru wao..nasikia tra wanakusanya trillioni siku hizi. mungu awabariki
 
Kwenye taarifa ya habari ya ITV tarehe 11/03/2016 niliona wakati EWURA wakijadili ombi la TANESCO kutaka kushusha bei ya umeme wakisema wadeni wakubwa wa TANESCO ni pamoja na Zanzibar inayodaiwa zaidi ya Shilingi bilioni 106, serikali (Tadhani walimaanisha) Tanganyika wanaidai bilioni 33 na watu binafsi bilioni kadhaa.

Hapo ndipo niliposhanga kuwa kwa deni lote hilo kwanini TANESCO hawaikatii umeme Zanzibar kama wanavyokata kwa watu binafsi wanaodaiwa sana sana elfu au laki kadhaa.

Vile vile nikashangaa kuwa baada ya kupindua uchaguzi wa wananchi katika uchaguzi wa Decemba mwaka jana wanaitisha uchaguzi mwingine utakogharimu zaidi ya bil 4 wakati tayari wameshama liwake jua au mvua inyeshe lazima wao watawale kwani wasingetumia hizo pesa kupunguza deni la TANESCO?
Madeni ya makoloni (colonies) yanastahili kulipwa na mkoloni mwenyewe; (Master)! Serikali ya Tanganyika iyabebe wao ndio wanajua kwa nini bado wanaendeleza na kunufaika na sera za makoloni hadi leo katika karne ya 21!
 
Wawekewe LUKU tu kubwa. Asiyelipa anawaponza na wenzake, matokeo yake watahimizana kila mmoja alipe
 
hii lazima ile kwetu
mfano mke wako akidaiwa na hana uwezo wa kulipa deni inabidi we umlipie tu ndoa yenu ipate kudumu
 
TRA wanakusanya 1.4 trillion kwa mwezi.. Kutoa billion 109 kwenye hyo hela ni sawa na kuchota ndoo ya maji baharini.

Zanzibar na tanganyika wamefunga ndoa.. Mme akizidiwa madeni inabidi mke nae avunje kibubu chake asaidie kulipa
 
Hizo hela mngewaambia tunawadai wakati wa kampaini ingependeza sana
 
Jaman huu muungano sasa tatizo.
Kama haya ni kweli basi hiki kisiwa ni pasua kichwa. Inasemekana the late Mwl Nyerere aliwahi kunukuliwa akisema kama angekuwa na uwezo angekivuta kisiwa mpaka katikati ya bahari ya hindi. Huyu mzee alikuwa anaona mbali sanaa.
 
Kwa hio kuwa na dhamira chafu ya kutaka kukiangamiza hiki kisiwa ndio kuona mbali.Pole bora na wewe uwone karibu
 
Wafungiwe luku moja kama nyumba za uswahilini usipochanga MTU mmoja Zanzibar nzima Giza..
 
Ahh akati bot ilitaka kulipa madai ya bilioni 900 TANZANIA ina hela
 
Nyie nyoko taratibu watanganyika wenzenu wapo huku msituletee balaa
 
Back
Top Bottom