KIBURUDISHO
JF-Expert Member
- Mar 28, 2011
- 1,002
- 274
Hivi Tanesco kwa nini mnafanya vitu ambavyo ukivifikilia kupitia kwenye kichwa chenye akili timamu unatamani ukamate kiboko uanze kuutandika uongozi mzima uliokaa ukasaini mikataba hii.Hivi kwa nini mnakubaliana na hao watu wanaowakodishia mitambo ya kuzalisha umeme kulipwa kwa siku kama ilivyokuwa kwa Richmond.? Kwa nini hawa wazalishaji wa umeme wasiwe wanalipwa kwa MEGAWAT wanazozalisha? Kama mwezi huu ataingiza megawat 100 alipwe hizo megawat 100 kama atazalisha 150 alipwe kwa hizohizo alizozalisha kutokana na utaratibu huu kama ukifuata kutakuwa na ushindani mkubwa kila mmoja atakuwa anajitahidi ili amzidi mwenzake sio huu wa sasa uzalishe usizalishe hesabu yako imeingia Tanesco hebu jaribuni maoni haya ya mlalahoi yatawasaidieni