TANESCO: Taarifa ya Katizo la Umeme kwa baadhi ya Mikoa

viatu virefu

Senior Member
May 25, 2015
165
20
TAARIFA YA KUKOSEKANA KWA UMEME KWA BAADHI YA MIKOA ILIYOUNGWA KWENYE GRIDI YA TAIFA FEBRUARI 27 NA 28, 2016


Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawatangazia wateja wake wa mikoa ya Singida, Shinyanga, Tabora, Mwanza, Musoma, Mara, Manyara, Simiyu na baadhi ya maeneo ya mikoa ya Arusha, Kilimanjaro na Tanga kuwa yatakosa umeme siku ya Jumamosi na Jumapili Februari 27 na 28, 2016 kuanzia saa 2.00asubuhi hadi saa 11.00jioni.

SABABU: Kumruhusu Mkandarasi anayejenga Njia Kuu ya Kusafirisha Umeme ya Msongo Mkubwa ya Kilovolti 400 maarufu kama Backbone kutoka Iringa kwenda Shinyanga, kuendelea na kazi ya kuunga njia hiyo eneo la Mtera na kwenye vituo vya Kupooza na Kusambaza Umeme vya Iringa, Dodoma, Singida na Shinyanga.

Mradi wa huo wa Backbone unalenga kuimarisha hali ya upatikanaji wa umeme wa uhakika nchini na utekelezaji wake upo katika hatua za mwisho.

Uongozi unaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.

Imetolewa na Ofisi ya Uhusiano
TANESCO Makao Makuu.
 
TAARIFA YA KUKOSEKANA KWA UMEME KWA BAADHI YA MIKOA ILIYOUNGWA KWENYE GRIDI YA TAIFA FEBRUARI 27 NA 28, 2016


Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawatangazia wateja wake wa mikoa ya Singida, Shinyanga, Tabora, Mwanza, Musoma, Mara, Manyara, Simiyu na baadhi ya maeneo ya mikoa ya Arusha, Kilimanjaro na Tanga kuwa yatakosa umeme siku ya Jumamosi na Jumapili Februari 27 na 28, 2016 kuanzia saa 2.00asubuhi hadi saa 11.00jioni.

SABABU: Kumruhusu Mkandarasi anayejenga Njia Kuu ya Kusafirisha Umeme ya Msongo Mkubwa ya Kilovolti 400 maarufu kama Backbone kutoka Iringa kwenda Shinyanga, kuendelea na kazi ya kuunga njia hiyo eneo la Mtera na kwenye vituo vya Kupooza na Kusambaza Umeme vya Iringa, Dodoma, Singida na Shinyanga.

Mradi wa huo wa Backbone unalenga kuimarisha hali ya upatikanaji wa umeme wa uhakika nchini na utekelezaji wake upo katika hatua za mwisho.

Uongozi unaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.

Imetolewa na Ofisi ya Uhusiano
TANESCO Makao Makuu.
 
Tunashukuru kwamba angalao siku hizi mnatoa Taarifa, haya tunawatakia kazi njema
 
TAARIFA YA KUKOSEKANA KWA UMEME KWA BAADHI YA MIKOA ILIYOUNGWA KWENYE GRIDI YA TAIFA FEBRUARI 27 NA 28, 2016


Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawatangazia wateja wake wa mikoa ya Singida, Shinyanga, Tabora, Mwanza, Musoma, Mara, Manyara, Simiyu na baadhi ya maeneo ya mikoa ya Arusha, Kilimanjaro na Tanga kuwa yatakosa umeme siku ya Jumamosi na Jumapili Februari 27 na 28, 2016 kuanzia saa 2.00asubuhi hadi saa 11.00jioni.

SABABU: Kumruhusu Mkandarasi anayejenga Njia Kuu ya Kusafirisha Umeme ya Msongo Mkubwa ya Kilovolti 400 maarufu kama Backbone kutoka Iringa kwenda Shinyanga, kuendelea na kazi ya kuunga njia hiyo eneo la Mtera na kwenye vituo vya Kupooza na Kusambaza Umeme vya Iringa, Dodoma, Singida na Shinyanga.

Mradi wa huo wa Backbone unalenga kuimarisha hali ya upatikanaji wa umeme wa uhakika nchini na utekelezaji wake upo katika hatua za mwisho.

Uongozi unaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.

Imetolewa na Ofisi ya Uhusiano
TANESCO Makao Makuu.


Naomba kulalamika hapa kabla Tanesco hamjaondoka
  1. Mtaani kwetu yapata mwaka sasa kila siku jioni umeme unakatwa wakati ng'ambo ya pili umeme unawaka continuously,
  2. Kuna waya za umeme zimelalia miti hai kwa muda mrefu, tukiwapigia Tanesco ofisi za Mkoa hawafiki kufanyia kazi tatizo hilo, tunaomba kama kweli mnakerwa na hali hiyo wekeni namba za simu za Boss wenu openly ili naye tumpime kama anatosha
 
Naomba kulalamika hapa kabla Tanesco hamjaondoka
  1. Mtaani kwetu yapata mwaka sasa kila siku jioni umeme unakatwa wakati ng'ambo ya pili umeme unawaka continuously,
  2. Kuna waya za umeme zimelalia miti hai kwa muda mrefu, tukiwapigia Tanesco ofisi za Mkoa hawafiki kufanyia kazi tatizo hilo, tunaomba kama kweli mnakerwa na hali hiyo wekeni namba za simu za Boss wenu openly ili naye tumpime kama anatosha
samahani kwanza pole kwa usumbufu mnao upata na pia naomba kufahamu uko mkoa gani na ningeomba namba yako ya simu ili nipate kwa ufafanuzi
 
Nimesoma tangazo lenu Tanesco la katizo la umeme kuanzia saa 2.00 asubuhi mpaka saa 11.00 jioni Jumamosi na Jumapili, ajabu ni kwamba mpaka ninapoandika hapa saa 12.37 umeme haujarudi, na hiyo ndio imekuwa kasumba yenu. Siku nyingine mnaukata saa 12.00 alfajiri mpaka saa 1 jioni. Halafu semeni ukweli maanake mlianza Jumapili naona sasa mmeongeza na J'mosi, itakuwa na Ijumaa nk. Mnaudhi...
 
Maeneo husika jiandaeni taarifa mmeshapewa.

Kama una mwenzio yuko maeneo hayo tajwa, jaribu kumjulisha kwa njia ya simu.

Kuna wengine wapo ambao hawatopata taarifa, wasaidieni kwa taarifa
 
Back
Top Bottom