nakumbuka kauli ya Mh. mbowe alimwambia waziri mkuu bado sijaridhika nahuo mpango wadharura kwasababu kila mara mnasema ivo ivo, pinda akamwambia siusubiri tushidwe ndoutuulize.
sasa swali linakuja wame shidwa tayari namgao ndohuo unaanza soon, PINDA UTAMWAMBIA NINI MBOWE?
Walikuwa wanatania mkuuInawezekana hii ni mbinu ya MAGAMBA ili wananchi wasipate fursa ya kufuatilia yale yanayojiri huko Arumeru. Iweje sasa wanadai Aggreko wamezima mitambo ilhal Mkurugenzi wa TANESCO alisema awali (sio zaidi ya wiki moja imepita) kuwa kinachotokea sasa ni matokeo ya mkataba ulioingiwa na NET GROUP pamoja na uchakavu wa mitambo na sio mgawo kama watu wanavyohisi.
Hizi kauli tata zinazotolewa na viongozi wetu zinaashiria nini kwa mustakabali wa taifa letu?
Hata tukibadilisha uongozi wote pale bado hali itakuwa hivi hivi kama tusipobadilisha mbinu za kibiashara za shirika hili na kuondoa siasa kwenye utendaji wake.
Kwa hali ilivyo pale Tanesco, siasa ni nyingi kuliko... Labda tutafute majibu ya maswali haya machache ili tujue hali halisi ilivyo. Hv ilikuwa ni viable kupeleka umeme mabwepande kwenye mahema? Kama jibu ni hapana ile distribution line imegharamiwa na nani au gharama zake zitarudi vp na kwa kipindi gani? The same apply kwa kawawa, kule madale enzi hizo.
Mbona Tanesco wanalazimishwa kujenga hizo line lakin serikali haiwalipi? Mbona taasisi za serikali na wizara zake hazilipi bili zao wakati budget ya matumizi hayo wanatengewa?
Wanatudanganya kwa ruzuku wanazolipatia shirika hili kumbe hata haifiki robo ya madeni yao.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), William Mhando,
Midraji Ibrahim
MKURUGENZI Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), William Mhando, amesema ingawa suala la kupatiwa umeme lipo kwenye stahili za mkataba wake, hawezi kubishana na uamuzi wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) wa kuondoa jenereta nyumbani kwake.
Akizungumza kufuatia agizo la POAC kuondoa jenereta hiyo nyumbani kwake jana, ili aonje uchungu wa kukatika kwa umeme, Mhando alisema alishtushwa na hatua hiyo kwa sababu ni suala la mkataba, lakini hawezi kubishana na kamati.
Mkataba ninao jana (juzi) nilishtuka kuhusu agizo hilo kwa sababu niliajiriwa na bodi na mwenyekiti wangu alikuwapo tutakaa tuangalie, lakini siwezi kupingana na maagizo ya kamati, alisema Mhando.
Hata hivyo, Mwenyekiti wa wa Bodi ya Tanesco, Jenerali mstaafu Robert Mboma, alisema watatii agizo la POAC la kuondoa jenereta la dharura lililopo nyumbani kwa mkurugenzi huyo.
Tumeagizwa na kamati tutaangalia jinsi ya kulitekeleza agizo hilo la kuondoa jenereta, tupeni siku tatu au nne hivi mtaona, alisema Jenerali Mboma.
Alipoulizwa kama kuondoa jenereta hiyo haitakuwa kinyume na mkataba wa ajira unaoonyesha stahili za mkurugenzi huyo, Mboma alisema: Unadhani tutafanya nini kama tumeagizwa tuiondoe, hatuna jinsi hata kama kuna mkataba sisi tutatekeleza tuliyoagizwa.
Mhando alisema suala la kukatika kwa umeme unaondelea hivi sasa, halisababishwi na menejimenti bali inatokana na kutokuwapo kwa uwekezaji muda mrefu kwenye shirika hilo, baada ya kuwekwa chini ya Shirika la Kubinafsisha na Kuuza Mashirika ya Umma (PSRC).
Tangu mwaka 1999 hadi 2007 hakuna uwekezaji uliofanywa kwa Tanesco baada ya shirika kuwekwa chini ya PSRC, kwa hiyo kukatika kwa umeme kunaokoonekana hivi sasa ni matokeo ya ubinafsishaji uliolengwa, alisema.
Mkurugenzi huyo alisema kukatika kwa umeme kunatokana na uchakavu wa miundombinu, lakini siyo kuzidiwa na kwenye uzalishaji kwa sababu hivi sasa wanazalisha Megawati 782.51 ilhali mahitaji ni Megawati 772.15.
Mfano pale City Center (katikati ya jiji), tulikuwa na transfoma mbili zote zimetumika zaidi ya miaka 30, Februari mwaka huu zimeharibika, tumeagiza kutoka Uturuki na sasa zimefika Dubai, tatizo ni miundombinu imechakaa, alisema.
Kuhusu Aggreko na Symbion Dodoma kuzima mitambo yao, Mhando alikiri kuwa hatua hiyo inatokana na deni ambalo linafikia Sh62 bilioni na kwamba, IPTL imepunguza uzalishaji kutoka Megawati 100 hadi 50. Aggreko inadai Sh58 bilioni na Symbion Dodoma Sh4 bilioni.
Mgawo kwa maana ya uwezo wa kuzalisha hatuna, ila hii kukatikakatika kwa sababu ya transfoma hiyo ipo. Tupo kwenye hatua mbalimbali za kukarabati miundombinu hiyo na baada ya kipindi tatizo hilo litatoweka, alisema.
Mhando alisema hivi sasa wamepata dola 85 milioni za Marekani kwa ajili ya Dar es Salaam, Euro 25 milioni kutoka Finland na Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) imetoa dola 40 milioni za Marekani.
Juzi, Mwenyekiti wa POAC, Zitto Kabwe, alisema lazima jenereta lililoweka nyumbani kwa mkurugenzi huyo liondolewe kwa sababu linatumia mafuta ya Serikali.
CHANZO: Mkurugenzi Tanesco asikitishwa uamuzi wa POAC
Mkuki kwa Nguruwe kwa Binadamu ni mchungu. Mkuu itabidi na wewe uonje Machungu ya Umeme wa Mgao.
Pia mimi nashauri haya:
1. Waziri wa elimu naye aondolewe kwenye pay roll kama miezi miwili hivi ili ajue adha ya walimu wanaoondolewa kwenye pay roll kiuzembe halafu wanapata usumbufu mkubwa kurudishwa
Source Majira
Kumbe tunaendelea kuganganywa kuwa mitambo ni michakavu ndo maana kuta kukatika katika kwa umeme kumbe ni madeni yanayowafanya washindwe kuzalisha umeme hasa unaozalishwa na kampuni ya Aggreco (samahani kama nitakuwa nimekosea kuiandika) kuidai tanesco zaidi ya billion 300/=
hiyo imebainishwa na mwenyekiti wa kamati ya nishati na madini mh January Makamba hapo Jana
Watanzania tunaisaidiaje tanesco kuibanafsisha tena au kuongezewa tena bei mpya
nakumbuka kauli ya Mh. mbowe alimwambia waziri mkuu bado sijaridhika nahuo mpango wadharura kwasababu kila mara mnasema ivo ivo, pinda akamwambia siusubiri tushidwe ndoutuulize.
sasa swali linakuja wame shidwa tayari namgao ndohuo unaanza soon, PINDA UTAMWAMBIA NINI MBOWE?
Ningekuwa mimi mdo rais natimua viongozi wote wa tanesco na kuweka uongozi mpya.haiwezekani shirika ambalo halina mpinzani na linalotoa huduma inayotakiwa kila mahali lijiendeshe kihasa.tanesco wakikusanya tu madeni wanayodai matatizo yameisha Its a shame
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), William Mhando,
Midraji Ibrahim
MKURUGENZI Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), William Mhando, amesema ingawa suala la kupatiwa umeme lipo kwenye stahili za mkataba wake, hawezi kubishana na uamuzi wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) wa kuondoa jenereta nyumbani kwake.
Akizungumza kufuatia agizo la POAC kuondoa jenereta hiyo nyumbani kwake jana, ili aonje uchungu wa kukatika kwa umeme, Mhando alisema alishtushwa na hatua hiyo kwa sababu ni suala la mkataba, lakini hawezi kubishana na kamati.
Mkataba ninao jana (juzi) nilishtuka kuhusu agizo hilo kwa sababu niliajiriwa na bodi na mwenyekiti wangu alikuwapo tutakaa tuangalie, lakini siwezi kupingana na maagizo ya kamati, alisema Mhando.
Hata hivyo, Mwenyekiti wa wa Bodi ya Tanesco, Jenerali mstaafu Robert Mboma, alisema watatii agizo la POAC la kuondoa jenereta la dharura lililopo nyumbani kwa mkurugenzi huyo.
Tumeagizwa na kamati tutaangalia jinsi ya kulitekeleza agizo hilo la kuondoa jenereta, tupeni siku tatu au nne hivi mtaona, alisema Jenerali Mboma.
Alipoulizwa kama kuondoa jenereta hiyo haitakuwa kinyume na mkataba wa ajira unaoonyesha stahili za mkurugenzi huyo, Mboma alisema: Unadhani tutafanya nini kama tumeagizwa tuiondoe, hatuna jinsi hata kama kuna mkataba sisi tutatekeleza tuliyoagizwa.
Mhando alisema suala la kukatika kwa umeme unaondelea hivi sasa, halisababishwi na menejimenti bali inatokana na kutokuwapo kwa uwekezaji muda mrefu kwenye shirika hilo, baada ya kuwekwa chini ya Shirika la Kubinafsisha na Kuuza Mashirika ya Umma (PSRC).
Tangu mwaka 1999 hadi 2007 hakuna uwekezaji uliofanywa kwa Tanesco baada ya shirika kuwekwa chini ya PSRC, kwa hiyo kukatika kwa umeme kunaokoonekana hivi sasa ni matokeo ya ubinafsishaji uliolengwa, alisema.
Mkurugenzi huyo alisema kukatika kwa umeme kunatokana na uchakavu wa miundombinu, lakini siyo kuzidiwa na kwenye uzalishaji kwa sababu hivi sasa wanazalisha Megawati 782.51 ilhali mahitaji ni Megawati 772.15.
Mfano pale City Center (katikati ya jiji), tulikuwa na transfoma mbili zote zimetumika zaidi ya miaka 30, Februari mwaka huu zimeharibika, tumeagiza kutoka Uturuki na sasa zimefika Dubai, tatizo ni miundombinu imechakaa, alisema.
Kuhusu Aggreko na Symbion Dodoma kuzima mitambo yao, Mhando alikiri kuwa hatua hiyo inatokana na deni ambalo linafikia Sh62 bilioni na kwamba, IPTL imepunguza uzalishaji kutoka Megawati 100 hadi 50. Aggreko inadai Sh58 bilioni na Symbion Dodoma Sh4 bilioni.
Mgawo kwa maana ya uwezo wa kuzalisha hatuna, ila hii kukatikakatika kwa sababu ya transfoma hiyo ipo. Tupo kwenye hatua mbalimbali za kukarabati miundombinu hiyo na baada ya kipindi tatizo hilo litatoweka, alisema.
Mhando alisema hivi sasa wamepata dola 85 milioni za Marekani kwa ajili ya Dar es Salaam, Euro 25 milioni kutoka Finland na Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) imetoa dola 40 milioni za Marekani.
Juzi, Mwenyekiti wa POAC, Zitto Kabwe, alisema lazima jenereta lililoweka nyumbani kwa mkurugenzi huyo liondolewe kwa sababu linatumia mafuta ya Serikali.
CHANZO: Mkurugenzi Tanesco asikitishwa uamuzi wa POAC
Mkuki kwa Nguruwe kwa Binadamu ni mchungu. Mkuu itabidi na wewe uonje Machungu ya Umeme wa Mgao.
Inawezekana hii ni mbinu ya MAGAMBA ili wananchi wasipate fursa ya kufuatilia yale yanayojiri huko Arumeru. Iweje sasa wanadai Aggreko wamezima mitambo ilhal Mkurugenzi wa TANESCO alisema awali (sio zaidi ya wiki moja imepita) kuwa kinachotokea sasa ni matokeo ya mkataba ulioingiwa na NET GROUP pamoja na uchakavu wa mitambo na sio mgawo kama watu wanavyohisi.
Hizi kauli tata zinazotolewa na viongozi wetu zinaashiria nini kwa mustakabali wa taifa letu?
Hata tukibadilisha uongozi wote pale bado hali itakuwa hivi hivi kama tusipobadilisha mbinu za kibiashara za shirika hili na kuondoa siasa kwenye utendaji wake.
Kwa hali ilivyo pale Tanesco, siasa ni nyingi kuliko... Labda tutafute majibu ya maswali haya machache ili tujue hali halisi ilivyo. Hv ilikuwa ni viable kupeleka umeme mabwepande kwenye mahema? Kama jibu ni hapana ile distribution line imegharamiwa na nani au gharama zake zitarudi vp na kwa kipindi gani? The same apply kwa kawawa, kule madale enzi hizo.
Mbona Tanesco wanalazimishwa kujenga hizo line lakin serikali haiwalipi? Mbona taasisi za serikali na wizara zake hazilipi bili zao wakati budget ya matumizi hayo wanatengewa?
Wanatudanganya kwa ruzuku wanazolipatia shirika hili kumbe hata haifiki robo ya madeni yao.
Kila siku TANESCO inadaiwa, pamoja na kupandisha bei ya umeme bado inadaiwa. Kama wameshaonesha kushindwa ni kwa nini tusitumie njia mbadala? Say, yaruhusiwe makampuni binafsi kuuza umeme kwa watumiaji!