MduduWashawasha
JF-Expert Member
- Mar 5, 2008
- 1,653
- 601
Habari wana JF.kuna kitu kimekuwa kikinishangaza wakati nakisikia kwa watu na sasa kinanitokea na mimi.Hawa kampuni ya umeme wako ktk kazi ya kufunga mita mpya kwa wateja.Cha kushangaza unit 50 Wanazojuwekea zikiisha basi tarajia usumbufu mkali sana kwani hiyo meter itagoma kupokea umeme utakaonunua.Utahangaika na fundi aliyefunga, naye atakupa namba ya call center ambako mtasumbuana sana na hao jamaa kwa majibu ya ovyo.Mpaka mambo yarekebishwe amin nakuambia wiki moja au mbili utakaa bila umeme nyumbani kwako.Najiuliza hawa jamaa wana client service charter?na ndivyo inavyosema? kama ni kitu common kwann wasijipange jinsi ya kudeal na hili tatizo?inabore sana nchi hii sioni hata shirika moja la serikali lunalofanya kazi kwa ufanisi