Tanesco kilimanjaro wauwaji?

jambotemuv

JF-Expert Member
Feb 7, 2008
224
62
Matukio ya raia kufa kwa ajali za umeme wilayani Moshi kufuatia hitilafu za wazi katika miundombinu ambazo TANESCO walitaarifiwa mapema na zikapuuziwa sasa yamezidi. Hivi majuzi kafa baba mmoja huko Marangu Moshi (Goodhope Mshanga) alipojikwaa shambani mwake na kuangukia waya ushikiliao nguzo ardhini (stay wire) na kumbe ulishagusana na nyaya za moto juu baada ya tawi kubwa la mti kuziangukia nyaya. TANESCO Himo walitaarifiwa mara kadhaa lakini hawakufanya lolote. Marehemu Mshanga amekuwa mtu wa pili kufa kwa umeme kijijini Sembeti baada ya mtoto wa bwana Manyanga, na vifo vyote vikihusisha 'stay wire'.
Aidha zipo nguzo nyingi za zilizoliwa mchwa na kuangukia miti mashambani humu na taarifa zimetolewa lakini TANESCO hawajali. Waungwana tumlilie nani kwa hili???? TANESCO Moshi mwataka wafe wangapi ndo mjali???
 
Labda muachane na hao wa Himo, ripoti/malalamiko yapelekwe moja kwa moja kwa Meneja wa Mkoa.

Halafu kama uko karibu na familia ya marehemu, waelekeze wafungue kesi ya madai dhidi ya TANESCO. Hata kama wana kipato cha chini kuna mawakili pale Moshi huwa wanachukua kesi chache bila malipo yaani "pro bono" kwa mfano Bi Elizabeth Minde au Bw Juma Mawalla.
 
Good call Injinia. Tabu inakuja kwenye taratibu za kisheria. Wataanza kudai ushahidi wa taarifa za maandishi, uthibitisho wa daktari nk nk. Worse ni ufanisi wa mahakama zetu. Kuishtaki serikali utajichokea tu ila yafaa kujaribu.
 
Good call Injinia. Tabu inakuja kwenye taratibu za kisheria. Wataanza kudai ushahidi wa taarifa za maandishi, uthibitisho wa daktari nk nk. Worse ni ufanisi wa mahakama zetu. Kuishtaki serikali utajichokea tu ila yafaa kujaribu.

Hapana.... wasikate tamaa... tafadhali sana wahimize waonane na wanasheria haraka sana....
 
Back
Top Bottom