Merry Christmas wana jamvi,
Niende moja kwa moja kwenye mada Tanesco Kibaha ambayo ndo inawakilisha Tenesco mkoa wa pwani, imejaa ubabaishaji na kuendekeza rushwa. Nasema HILI kwa sababu moja.
Mkoa wa Pwani ni mojawapo ya mikoa ambayo inakuwa kwa kasi sana, lakini pia ni mojawapo ya mikoa ambayo imepitiwa na miradi mbalimbali iliyo chini ya shirika la umeme.
Maeneo nilioko mimi ni maeneo yaliyopitiwa na mradi wa nguzo za zege, mradi umekamilika kabisa, shida ni Tanesco kuaunganishia wateja umeme.
Hapa ni rushwa tupu na hii rushwa inaanza unapopeleka mchoro. Ukishafikisha mchoro wako wanaupokea na kukwambia nenda tutakupigia simu kukupangia suryeyor.
Lakini pindi unapotoka tu nje ya ofisi kuna mtu atakufuata na kukuliza bro nyumba yako iko eneo gani?
Kama unataka surveyor wa haraka chukua namba ya simu, ila kama hauna haraka nenda kasubiri, japo naamini utakaa sana.
Kwa udadisi wangu na kutaka kujiridhisha zaidi nikamwambia mhusika sawa nikimuitaji surveyor nje ya ofisi ni shilingi ngapi za kitanzania, bila wasiwasi akanijibu laki moja.
Na je nikishakupatia hilo laki moja ni nini kinafuata? Jibu Surveyor akisha survey utapatiwa control namba ambayo utaenda kulipa malipo halali ya Serikali kiasi cha shilingi laki tatu na ishirini.
Ukishalipia hiyo ya Serikali yule anayekuja kuunganisha umeme naye anatataka laki na nusu.
Na endapo sitokuwa na hiyo hela ina maana sitapata umeme?
Endapo utakuwa kichwa ngumu umeme utausikia na kuuona kwa jirani kwa sababu surveyors tuko wachache na bosi atatupangia kazi kulingana na watu walio mpatia hela, ndio maana na mimi nataka kutumia muda wangu nije nikufanyie survey.
Swali ni je ni mapato kiasi gani ambayo watumishi wa Tanesco Kibaha wanaikosesha Serikali kwa sababu ya kutaka rushwa ya laki moja?
Ukiachana na mimi nyumba kibao ambazo zimepitiwa na huo mradi hazina umeme na umeme upo, binafsi baada ya kukataa kutoa rushwa sijawahi muona surveyor tangu mwezi wa tisa mpaka leo hii.
Majirani zangu walioamua kutoa rushwa tayari wanao umeme. Mimi nimeapa sitotoa rushwa kwa kuwa ninayo solar yangu na pasi yangu ya mkaa ngoja wakae na umeme wao.
Kwa hiki kibarua changu kodi ninayolipa Serikalini ni kubwa mno, lakini pia katika zile billion ngapi kwa mwezi ambazo Serikali inatoa kwa ajili ya elimu bure huko nako mimi nimeipunguzia Serikali mzigo kwa kulipia gharama hizo moja kwa moja.
Tanesco Kibaha badilikeni la sivyo nimejipanga kurudi kivingine hasa wewe jamaa ambaye ndo unawapangia masurveyor kazi pamoja surveyors wako, nitakuja tena najua bado mnaitaji hii laki moja yangu, itaondoka nanyi.
Niende moja kwa moja kwenye mada Tanesco Kibaha ambayo ndo inawakilisha Tenesco mkoa wa pwani, imejaa ubabaishaji na kuendekeza rushwa. Nasema HILI kwa sababu moja.
Mkoa wa Pwani ni mojawapo ya mikoa ambayo inakuwa kwa kasi sana, lakini pia ni mojawapo ya mikoa ambayo imepitiwa na miradi mbalimbali iliyo chini ya shirika la umeme.
Maeneo nilioko mimi ni maeneo yaliyopitiwa na mradi wa nguzo za zege, mradi umekamilika kabisa, shida ni Tanesco kuaunganishia wateja umeme.
Hapa ni rushwa tupu na hii rushwa inaanza unapopeleka mchoro. Ukishafikisha mchoro wako wanaupokea na kukwambia nenda tutakupigia simu kukupangia suryeyor.
Lakini pindi unapotoka tu nje ya ofisi kuna mtu atakufuata na kukuliza bro nyumba yako iko eneo gani?
Kama unataka surveyor wa haraka chukua namba ya simu, ila kama hauna haraka nenda kasubiri, japo naamini utakaa sana.
Kwa udadisi wangu na kutaka kujiridhisha zaidi nikamwambia mhusika sawa nikimuitaji surveyor nje ya ofisi ni shilingi ngapi za kitanzania, bila wasiwasi akanijibu laki moja.
Na je nikishakupatia hilo laki moja ni nini kinafuata? Jibu Surveyor akisha survey utapatiwa control namba ambayo utaenda kulipa malipo halali ya Serikali kiasi cha shilingi laki tatu na ishirini.
Ukishalipia hiyo ya Serikali yule anayekuja kuunganisha umeme naye anatataka laki na nusu.
Na endapo sitokuwa na hiyo hela ina maana sitapata umeme?
Endapo utakuwa kichwa ngumu umeme utausikia na kuuona kwa jirani kwa sababu surveyors tuko wachache na bosi atatupangia kazi kulingana na watu walio mpatia hela, ndio maana na mimi nataka kutumia muda wangu nije nikufanyie survey.
Swali ni je ni mapato kiasi gani ambayo watumishi wa Tanesco Kibaha wanaikosesha Serikali kwa sababu ya kutaka rushwa ya laki moja?
Ukiachana na mimi nyumba kibao ambazo zimepitiwa na huo mradi hazina umeme na umeme upo, binafsi baada ya kukataa kutoa rushwa sijawahi muona surveyor tangu mwezi wa tisa mpaka leo hii.
Majirani zangu walioamua kutoa rushwa tayari wanao umeme. Mimi nimeapa sitotoa rushwa kwa kuwa ninayo solar yangu na pasi yangu ya mkaa ngoja wakae na umeme wao.
Kwa hiki kibarua changu kodi ninayolipa Serikalini ni kubwa mno, lakini pia katika zile billion ngapi kwa mwezi ambazo Serikali inatoa kwa ajili ya elimu bure huko nako mimi nimeipunguzia Serikali mzigo kwa kulipia gharama hizo moja kwa moja.
Tanesco Kibaha badilikeni la sivyo nimejipanga kurudi kivingine hasa wewe jamaa ambaye ndo unawapangia masurveyor kazi pamoja surveyors wako, nitakuja tena najua bado mnaitaji hii laki moja yangu, itaondoka nanyi.