Tamko la waislam dhidi ya kauli za maaskofu

Tamko la waislam dhidi ya kauli za maaskofu

Maarifa

JF-Expert Member
Joined
Nov 23, 2006
Posts
4,568
Reaction score
2,925
Jamani mie nimetumiwa e mail tu! just to review whats writtten. Msinihukumu bali nanyi fanyeni review zenu. Angalizo just review as a great thinker na sio mshabiki tu. Hapo tutakuwa sawa. Je wewe unasemaje?

Habari yenyewe hii hapa!!
TAMKO LA WAISLAMU DHIDI YA KAULI ZA MAASKOFU
Utangulizi
Oktoba 31, 2010 Tanzania ilifanya uchaguzi mkuu ambapo wananchi walipata fursa
ya kumchagua Rais, wabunge pamoja na madiwani. Katika uchaguzi huo, Watanzania
kwa ujumla wao walikichagua Chama cha Mapinduzi, CCM, kuongoza tena nchi kwa
kipindi kingine cha miaka mitano.
Hata hivyo, wakati wananchi wakiamini kwamba wanaongozwa na watu waliowapigia
kura, matukio yanayoendelea hivi sasa yanaashiria serikali kutelekeza majukumu
yake na kuwaacha maaskofu wakielekeza nchi wanakotaka.
Itakumbukwa kwamba awali kabla ya uchaguzi mkuu maaskofu walikuwa wametoa Ilani
yao ya uchaguzi bila kueleza kipi chama chao kitakachosimamia na kutekeleza
Ilani hiyo. Baadhi ya viongozi wa serikali na chama tawala, CCM, walishabikia
Ilani hiyo na kuwatetea maaskofu. Kwa hakika taarifa za vyombo vya habari
zilifahamisha kwamba baadhi ya watendaji waandamizi ndani ya serikali
walishiriki katika kuandaa Ilani hiyo.
Ilipofika wakati wa kampeni hadi kuingia siku ya kupiga kura, ilikuwa imedhihiri
kipi kilikuwa chama cha maaskofu ambacho walitarajia kitekeleze Ilani yao.
Haikuwa tena jambo la siri kwani walisimama wazi wazi kuwaelekeza waumini wao
wampigie nani kura. Na katika juhudi zao za kutaka wafuasi wao wawaelewe vizuri,
maaskofu walithubutu hata kuweka kando mafundisho ya Biblia yao juu ya masuala
ya uzinzi wakawahimiza waumini kumpigia kura mtu wanayemtaka bila kujali kwamba
anakabiliwa na kashfa ya kupora mke wa mtu. Waliwaambia wasihangaike na maisha
binafsi ya ndoa ya mgombea.
Hata hivyo, matokeo ya kura yalitoa majibu kwamba Watanzania walikuwa wameikataa
Ilani ya Maaskofu.
Waislamu tumelazimika kukutana na kutoa tamko hili kwa sababu matukio
yanayotokea hivi sasa yanaonesha kuwa wale ambao Watanzania walikataa kuwapa
uongozi na Ilani yao iliyoandaliwa na maaskofu, ndio sasa wanaielekeza nchi pa
kwenda huku viongozi wa CCM na serikali wakijitahidi kadiri ya uwezo wao
kunyenyekea kwa maaskofu hao.
Tumeona na tumemsikia Waziri Mkuu Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda
akihangaika kuwapigia magoti na kuwaomba radhi maaskofu kule Sumbawanga.
Tumesikia jinsi viongozi wanaojaribu kuwaambia maaskofu kwamba kama wanataka
kuingia katika siasa wavue majoho na vyeo vyao vya kikanisa kama Padiri mwenzao
waliyekuwa wakimpigania kuingia Ikulu, wanavyokemewa na kutakiwa wawaombe radhi
maaskofu hao.
Lililo baya zaidi maaskofu walioshindwa kuwashawishi wananchi waipokee na
kukubali Ilani yao, wamekuja na kampeni za kuchochea uasi kwa serikali iliyopo
madarakani. Lakini pamoja na hali hiyo, viongozi wa CCM na serikali wamebaki
wanagwaya. Hakuna aliyeweza kupata ujasiri wa kukemea hali hii. Kinyume chake
Waziri Mkuu na Mzee John Samwel Malecela wanahangaika huku na kule wakiwapigia
magoti maaskofu hao na kuwakemea wanaothubutu kuwakosoa.
Hali kama hii ni hatari kwa usalama na utulivu wa nchi. Ni hali ya kuchochea
udini na kuweka ombwe la uongozi wa kisiasa ambao utazua balaa. Waislamu
hatuwezi kukubali hali hii. Kwa hiyo, ama CCM na serikali vitekeleze wajibu wao
wa kuongoza au kama wanaona hawawezi, basi waseme rasmi ili Maaskofu na wengine
wenye Ilani zao za uchaguzi waingie tena ulingoni kuomba ridhaa ya Watanzania
kuongoza nchi kuliko kuishi katika hiki kiini macho ambapo maaskofu na mawakala
wao ndani ya serikali wameachwa waikokote nchi wanakotaka.
Kiini cha Hali hii ya Kisiasa
Hali hii ya kisiasa tunayoishuhudia leo nchini mwetu ni matunda ya mbegu
liliyopandwa na kupaliliwa kwa zaidi ya miaka 100 iliyopita. Wakoloni walikuwa
na kanuni yao waliyoiita divide et impero yaani wagawe ili uwatawale. Huko
Rwanda wakoloni waliwagawa wananchi kwa misingi ya kikabila. Watusi ambao ni
watawala wapewe elimu ya juu na wanfundishwe kwa Kifaransa, na Wahutu ambao ni
watawaliwa wapewe elimu duni na wafundishwe kwa Kiswahili. Ubaguzi huo wa
kuwagawa raia wa nchi moja ulipandikiza sumu iliyokuja kusababisha Wanyarwanda
kuuana.

Hapa kwetu wakoloni walitugawa kwa misingi ya dini. Kabla ya uhuru wa
Tanganyika, wakoloni kwa kushirikiana na makanisa waliwaona Waislamu kama ni
mahasimu wao kidini na kisiasa. Na kwa sababu hiyo serikali za kikoloni zikaweka
mikakati maalum ya kuwakandamiza Waislamu katika maeneo matatu: kwanza kuwawekea
vikwazo katika kutangaza dini yao ili wasiongezeke; pili kuwabana katika elimu
na ili kuhakikisha kuwa Waislamu wanabanwa jukumu la kuwaelimisha Waafrika
likawekwa mikononi mwa makanisa na kazi ya serikali ni kuzigharimia tu shule
hizo. Lengo likiwa ni kuwabatiza Waislamu wachache watakaoruhusiwa kusoma, na
tatu kuwabana katika ajira serikalini kwa sababu makanisa yote yalisisitiza kuwa
kuwaajiri Waislamu serikalini ni kusaidia kuenea kwa Uislamu..
Kwa kuwa ubaguzi huo haukuwa na kificho chochote, Waislamu wengi walijitokeza
kupambana na ukoloni kwa matarajio kuwa serikali huru itaondosha chuki na uadui
huo dhidi ya Waislamu. Lakini msiba mkuu wa taifa hili ni kwamba kinyume chake,
baada ya uhuru msimamo ukawa ni ule ule wa kuwaona Waislamu kuwa ni maadui wa
kupigwa vita na mikakati ya kuwabana Waislamu katika maeneo yale matatu
ikaimarishwa zaidi wakati wa utawala wa Nyerere. Kuanzia 1957 mkakati uliopangwa
na Kanisa Katoliki ukawa ni kuhakikisha kuwa nafasi zote muhimu za uongozi na
serikali zinashikwa na wao. [Taz. Confidential Diary – Tanganyika, March-April
1957, uk. 3-4 Maryknoll Central Archives, New York ]. Na ni mkakati huu ndio
ambao Mwalimu Nyerere aliokuwa akimuhakikishia Askofu Rweyemamu mwaka 1970 kuwa
anatumia mamlaka yake kama Rais na kama kiongozi wa TANU kuhakikisha kuwa anatoa
upendeleo maalum kwa Wakristo ili wasimamie sera za Chama. Na kwamba amemteua
padiri katika nafasi nyeti ya Chama si kwa sababu anajua siasa bali kwa sababu
ni Mkristo safi. Lakini Nyerere huyo huyo akisimama hadharani alijidai kukemea
udini. Na kwa kazi kubwa aliyoifanya ya kuliimarisha kanisa na kuwadhoofisha
Waislamu, leo Kanisa lake limo katika mchakato wa kumtangaza Nyerere kuwa ni
Mtakatifu!
Sivalon anaarifu katika kitabu chake kuwa mara baada ya uhuru Kanisa katoliki
liliwahamasisha Wakristo wote na hasa watendaji wa serikali juu ya hatari ya
Ukomunisti na Uislamu na walikusanya nguvu zao zote katika kukabiliana na maadui
hao.
Matokeo ya Hujuma Hizo
Matokeo ya hujuma hizo za kichinichini ni kwamba katika sura ya nje na katika
propaganda za kisiasa Tanzania ni nchi moja yenye mshikamano na umoja na kisiwa
cha amani. Lakini uhalisia wa mambo ni kuwa Tanzania ni nchi yenye jamii kubwa
mbili. Jamii ya Wakristo wanaopewa msaada, upendeleo, ulinzi na heshima, na
jamii ya Waislamu ambao wanachukiwa, kudharauliwa na kudhoofishwa na serikali
kabla na baada ya Uhuru. Ifuatayo ni mifano michache tu ya baadhi ya hujuma hizo
baada ya Uhuru.
(1) Mwaka 1963 katika Barua ya Kichungaji, Kanisa Katoliki lilisema Waislamu
walikuwa wanajenga umoja na mshikamano miongoni mwao, jambo ambalo ni “hatari
kubwa kwa hatima ya Wakristo wetu” na Sivalon anabainisha kuwa Wakristo
walimwomba Nyerere awasaidie kuvuruga umoja huo wa Waislamu. Ndio sababu ya
Nyerere kutumia dola kuiparaganya EAMWS. Kwa kuwa Waislamu ni jamii inayotakiwa
kuwa dhalili, hawatakiwi kuwa na umoja. Ndio maana tangu wakati wa Nyerere hadi
leo, uchaguzi wa viongozi wa Waislamu husimamiwa na vyombo vya dola. Nia ikiwa
ni kutokuwapa Waislamu uhuru wa kuwachagua viongozi wao. Katika taifa moja haki
hiyo ni ya Wakristo peke yao. Sote ni mashahidi kuwa mwaka 1994 serikali
ilimwagiza Naibu Waziri Mkuu Mh. Augustino L. Mrema kuhakikisha kuwa Bakwata
inapitisha katiba mpya inayotakiwa na serikali. Na Maaskofu wakachangia gharama.
Waislamu ni maadui kidini na kisiasa, lazima wadhibitiwe.

(2) Mwaka 1992 Serikali ya Tanzania ilitiliana saini Makubaliano ya Itifaki
rasmi na Makanisa ya TEC na CCT. Kwa mujibu wa makubaliano hayo ambayo yalitiwa
saini na Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu, ambaye wakati huo alikuwa
Mh. Edward Lowasa serikali imewajibishwa pamoja na mambo mengine, kutenga nafasi
za masomo kwenye vyuo vyake vya Ualimu mahsusi kwa ajili ya wanafunzi
wanaopangwa kufundisha katika shule za Kanisa; pia kutoa ruzuku ya kuendeshea
taasisi za Makanisa. Kuanzia 1992 hadi leo serikali imetoa mabilioni ya kodi za
wananchi kwa Makanisa. Katika kipindi chote hicho Waislamu wamepinga ubaguzi
huo. Lakini kwa kuwa lengo ni kuwaimarisha Wakristo ambao ni jamii inayotakiwa
kupewa nguvu zaidi dhidi ya jamii ya Waislamu ambao wanatizamwa kama maadui,
serikali imeyapuuza malalamiko ya Waislamu. Lakini propaganda zinaendelea kuwa
Tanzania ni nchi moja yenye mshikamano na umoja na ni kisiwa cha amani.
(3) Waislamu wameiomba serikali kujiunga na OIC kama njia mojawapo
itakayowezesha nchi yetu kupata misaada itakayotumika kuinua hali za Waislamu
ambao wameachwa nyuma sana katika elimu na uchumi. Makanisa yote kwa kauli moja
yamepinga kwa nguvu zao zote pendekezo hilo. Sababu ya kupinga kwao ni kuwa
mkakati uliopo ni kuhakikisha kuwa Waislamu wanadhoofishwa katika kila hali, na
ni makosa makubwa kuwaimarisha kiuchumi au kielimu maadui hao. Serikali
ilipofanya utafiti wake wa kina ikajiridhisha kuwa kujiunga na OIC kuna manufaa
na hakuna madhara yoyote. Na Mh. Bernard Membe alitamka hilo Bungeni. Mara
akaitwa na Askofu Mkuu wa Jimbo la Dar es Salaam, Muadhama Polycarp Cardinali
Pengo na kukumbushwa mkakati wa kuwadhoofisha Waislamu. Msimamo wa serikali
ukabadilika. Lakini propaganda za kuwazuga Waislamu zinasema Watanzania wote ni
kitu kimoja na nchi hii haina ubaguzi!
(4) Kwa kuwa tangu wakati wa ukoloni hadi leo mkakati uliopo ni kuhakikisha kuwa
Waislamu wanaminywa kadiri iwezekanavyo katika nafasi za uongozi na ajira, ndio
maana hadi leo, miaka 50 baada ya Uhuru Waislamu ni wachache sana katika nafasi
zote za uongozi na ajira katika sehemu muhimu serikalini na katika vyombo muhimu
vya maamuzi. Kisingizio kinachotolewa ni kuwa Waislamu hawataki kusoma. Lakini
ukitazama orodha ya Wakuu wa Wilaya wote walioteuliwa na sifa zao, utaona
dhahiri kuwa wapo Waislamu wengi wenye sifa bora zaidi ambao wangestahili kuwa
ma-DC. Waislamu hawateliwi kwa sababu mkakati uliopo ni kuwatenga Waislamu na
ikiwezekana kuwaondosha kabisa katika sehemu muhimu za uongozi, kwa sababu kama
wao hawajui ukweli ni kwamba hawatakiwi kushika nafasi zozote muhimu za uongozi
au ajira. Ndio maana asilimia 75 ya Ma-DC wote ni Wakristo na karibu wasimamizi
wote wa Uchaguzi katika wilaya ni Wakristo. Wabunge asilimia 75 pia ni Wakristo,
na hali ni hiyo hiyo katika Vitengo vya serikali na Mashirika ya uma. Ndio maana
hakuonekani tatizo lolote pale taasisi yote inapokuwa na Wakristo watupu. Na
kelele nyingi maadui wa serikali na Kanisa wanapopewa nafasi hata kama wana
uwezo kiasi gani. Katika sura ya nje Tanzania ni taifa moja, katika uhalisia
wake ni kuna mataifa mawili, moja nyonge na jingine lenye nguvu.
(5) Kwa kuwa Waislamu wanahesabiwa kuwa ni maadui, ule mkakati uliowekwa na
wakoloni wa kuwawekea vikwazo Waislamu katika kutangaza dini yao unaendelea hadi
leo. Ipo mifano mingi sana ya Waislamu kukamatwa, kutiwa ndani na kunyanyaswa na
vyombo vya dola kwa sababu tu ya kulingania hadharani dini yao. Kwa kuwa
Waislamu ni maadui, basi ni muhimu kuhakikisha kuwa hawaongezeki. Wakristo
wanayo haki ya kuitisha mkutano wa hadhara na kutangaza kuwa Yesu ni Mungu. Wao
ni jamii inayostahiki ulinzi wa dola. Lakini pindi Mwislamu atakaposema
hadharani kuwa Mwenyezi Mungu aliyeumba mbingu na ardhi siyo Yesu mwana wa
Mariamu atakuwa amekashifu dini ya dola na atakamatwa na kubughudhiwa. Lakini
kipropaganda, Tanzania ni nchi moja na inafuata katiba moja. Lakini uhalisia ni
tofauti.
(6) Msimamo wa serikali na makanisa kuhusiana na mauaji ya Waislamu katika
msikiti wa Mwembechai ni kielelezo kingine cha ukweli kuwa Tanzania ni
mkusanyiko wa jamii mbili zenye haki na hadhi tofauti katika taifa moja. Kwa
kushinikizwa na Maaskofu serikali iliwauwa Waislamu watatu Mwembechai pasi na
hatia yoyote. Waislamu waliiomba Mahaka, Bunge na hata Rais aunde Tume ya
uchunguzi. Mihimili yote ya dola ilikataa. Kiongozi wa Kanisa Katoliki akenda
mbali zaidi. Akahalalisha mauaji hayo. Kwa sababu waliouliwa ni wale maadui wa
ile jamii nyoge isiyotakiwa kustawi. Lakini alipouliwa mbwa “Imigresheni” mwaka
huo huo wa 1998, Jaji Mkuu wa wakati huo Mh. Francis Nyalali aliamuru uchunguzi
wa kuuliwa mbwa huyo na hakimu akaadhibiwa. Jaji Mkuu alichukua uamuzi huo bila
kuombwa na mtu. Lakini wale waliowauwa Waislamu walipongezwa na kupandishwa
vyeo. Uhasama wa serikali na makanisa dhidi ya jamii ya Waislamu ni wa kiwango
cha kutisha. Msimamo ukawa huo huo walipouliwa Waislamu Unguja na Pemba 2001 kwa
kuandamana kudai Katiba Mpya. Lakini kipropaganda tunaambiwa Watanzania wote
wanahaki sawa.
(7) Rais wa Marekani George W. Bush alipotangaza Vita vya Msalaba dhidi ya
Waislamu mwaka 2001, serikali ya Tanzania ikapata uhalali zaidi wa kuzidi
kuwakandamiza Waislamu. Serikali ikawa radhi kuvunja Katiba ya nchi kwa
kupitisha Sheria ya Kuzuia Ugaidi ya 2002 ili zipatikane fursa zaidi za
kuwanyoongesha Waislamu. Waislamu waliipinga sheria hiyo kwa nguvu zao zote,
lakini kwa kuwa wao ni jamii inayotakiwa kupigwa vita hawakusikilizwa. Bunge
ambalo nalo lina Wakristo wengi likaipitisha haraka sheria hiyo. Naam, tangu
imepitishwa hadi leo, sheria hiyo imetumika kuwadhuru Waislamu wasiokuwa na
hatia yoyote, na kufunga taasisi zilizokuwa zikiwasaidia Waislamu. Misaada ni
haki ya Wakristo, siyo Waislamu. Pamoja na madhila yote hayo Waislamu wanatakiwa
waendelee kuamini kuwa Tanzania ni nchi moja inayojali raia wake wote.
(8) Wakati serikali ikidai kuwa Tanzania ni taifa ambalo raia wote wana haki
sawa, lakini serikali hiyo hiyo kwa makusudi kabisa inafanya jitihada za
waziwazi za kuwahamasisha Wakristo wawaone Watanzania ambao ni Waislamu kuwa ni
maadui zao na maadui wa taifa lao. Januari 2001 Waziri Mkuu Mh. Frederick Sumaye
alisema katika mkutano wake na waandishi wa habari kuwa serikali inazo taarifa
kuwa kundi la magaidi waliopata mafunzo nchi za nje limerejea nchini na magaidi
hao wanapanga kuilipua hospitali ya Muhimbili. Kufuatia kauli hiyo Waislamu
watatu wa Muhimbili ambao ni Waislamu akiwemo Profesa wa Micro-Biology walitiwa
mbaroni. Japo baadaye waliachiwa kwani hawakuwa na hatia yoyote, lengo la
serikali la kupandikiza sumu ya chuki lilikuwa limetimia. Tarehe 24 Agosti 2001
Waislamu walifanya maandamano kupinga kufungwa kwa Dibagula kwa kusema Yesu si
Mungu. Serikali kupitia jeshi la polisi likawatangazia wananchi wote kuwa
Waislamu wamepanga kuyalipua makanisa siku ya Jumapili ya tarehe 2 Septemba
2001. Na serikali ikawahakikishia Wakristo kuwa itaweka maaskari wa kuwalinda na
hiyo shari ya Waislamu. Lengo la uzushi huu ni kuwachochea Wakristo wawachukie
Waislamu na hivyo waunge mkono hatua za serikali za kuwapa kipondo. Hivi sasa
huo umekuwa ni mchezo wa kawaida. Kila baada ya muda Fulani serikali kwa kpitia
jeshi la polisi hutoa taarifa za kuonesha kuwa kuna mpango wa shambulio la
kigaidi. Na watuhumiwa siku zote ni Waislamu. Serikali na makanisa yanawachukia
Waislamu kiasi cha kuwa tayari kushirikiana na wasiokuwa Watanzania katika
kuwahujumu Waislamu. Ni dhahiri kuwa katika mazingira kama haya, Maaskofu
wakipata kisingizio chochote watakuwa tayari kuwauwa Waislamu kama
walivyoshiriki katika mauaji ya kimbari ya Rwanda.
(9) Papa John Paul II alipoitembelea Tanzania mwaka 1990, Kanisa Katoliki
lilimkabidhi Ripoti yenye anwani: Activities of the Church in Tanzania. Katika
ripoti yake hiyo Kanisa Katoliki limetaja kuwapo kwa Tume ya Majeshi ya Kivita
[Commission of Armed Forces] ndani ya Kanisa hilo. Tangu wakati huo hadi leo
Waislamu wameitaka serikali iwaondoshe hofu kwa kuweka wazi kazi za Tume hiyo ya
Majeshi ya Kivita ndani ya Kanisa. Serikali haijajibu na wala haijajishughulisha
na taarifa nzito kama hizo. Hatujui kama Tume hiyo ya Majeshi ya kivita inafanya
kazi ndani ya Jeshi la Wananchi au nje ya jeshi hilo. Lakini kwa muktadha wa
hali ya uhasama wa serikali na hasa wa Maaskofu dhidi ya Waislamu wanaowahesabu
kuwa ni maadui zao, si vigumu kukisia kwa nini Kanisa Katoliki limeunda Tume ya
Majeshi ya Kivita. Lakini serikali ambayo haishughulishwi kabisa na Tume ya
Majeshi ya Kivita ya Wakatoliki imekuwa na tabia ya kuwakamata na kuwatia ndani
Waislamu kwa kesi za kuwabambikia zisizokuwa na kichwa wala miguu. Lakini
propaganda zinasema Tanzania ni nchi moja yenye katiba inayolinda haki za watu
wote. Mwenye mach haambiwi tazama.
Dalili ya Mvua ni Mawingu
Alipokuwa akitoa mada yake juu ya “Mifumo ya Viashiria vya Migogoro” katika
Mkutano wa Kumi na Moja wa Hali ya Siasa Tanzania ulioandaliwa na REDET mwaka
2003, Mh. Bernard L. Membe alisema kwamba migogoro mingi duniani na hasa vita
vya wenyewe kwa wenyewe vina dalili na viashiria vyake. Akasema miongoni mwa
dalili kubwa kuwa nchi karibu itaingia katika machafuko ya vita vya wenyewe kwa
wenyewe ni kutokea kwa mgawanyiko au kutokea kutoelewana kwa viongozi ndani ya
chama au serikali tawala.

Katika siku za hivi karibuni tumeshuhudia viongozi mbalimbali wa serikali
wakiwamo mawaziri wakipingana hadharani juu ya maamuzi waliyoyafanya wenyewe.
Lakini pia katika siku za hivi karibuni tumeshuhudia pia mgongano wa waziwazi
kati ya wabunge wa CCM na Chama chao. Na wote hao hawachoki kujisifu kuwa
wanamuenzi Mwalimu Nyerere. Lakini mwaka 1993, Nyerere katika Kitabu chake
Tanzania! Tanzania! Aliandika na tunanukuu:
Ziko jitihada sasa hivi za kugombanisha Wabunge na chama chao kwa kutumia hoja
ya hadhi ya Bunge. Ni nani huyu anayefanya kazi hii? Ni haki kabisa ya vyama vya
upinzani kujaribu kugombanisha Wabunge wa chama kinachotawala na chama chao.
Lakini viongozi wa chama kinachotawala pamoja na Serikali yenyewe wanapojaribu
kufanya mambo ambayo yatagombanisha Wabunge wa CCM na chama chao, tuna haki ya
kuwauliza viongozi hao wanafanya kazi hii kwa niaba ya nani, na chama chao ni
chama gani? [uk. 41]
Pamoja na kuyajua yote hayo hivi sasa kuna msuguano ulio dhahiri kabisa baina ya
Wabunge wa CCM na Chama chao. Kiashiria kingine alichokitaja Mh. Membe ni kwa
serikali kushindwa kuyashughulikia malalamiko mbalimbali ya wananchi
yanayoelekezwa serikalini.
Maazimio ya Waislamu
Kwa kuzingatia muktadha wa hali ya kisiasa ilipofikia hivi sasa, Waislamu
tumefikia maamuzi yafuatayo:
(1) Maadam Mfumo Kristo umeimarika kiasi cha kuweza kuitisha serikali na
viongozi wake na wakatishika, na maadam Mfumo huo Kristo una nguvu za kuweza
hata kuvitisha na kuvikemea vyombo vya dola na vikasalimu amri, Waislamu tutake
tusitake, kama alivyohadharisha Mh. Membe, ukweli unabaki kuwa hautapita muda
mrefu, dhulma hii ya udini italisambaratisha Taifa letu, kama udini
ulivyoisambaratisha Ivory Coast ambayo katika miaka ya 1960 na 1970 ilikuwa
mfano wa kuigwa.

Hivyo basi wajibu wetu wa mwanzo ni kuufikisha ujumbe huu kwa Waislamu wote
nchini, na kuwataka wazingatie kuwa kwa kuwa wanabaguliwa na kudhalilishwa
katika nchi hii kwa sababu ya Uislamu wao, basi ni wajibu wao na wao kushikamana
kama Waislamu.
(2) Kwa kuwa kila wanchosema Maaskofu ndicho kinachofuatwa na serikali, na kwa
kuwa Maaskofu wamekwishatamka hadharani na kwa sauti kali kuwa katika nchi yetu
hakuna kabisa udini na atakayesema kuna udini basi ni yeye ndiye anayetaka
kuleta udini, na kauli hiyo kudakwa na mawakala wa Maaskofu katika serikali, ni
dhahiri kuwa dhulma za udini zinazoendelea kuwakandamiza Waislamu miaka 50 baada
ya Uhuru hazitaondoshwa na Katiba mpya. Hivyo wajibu wetu mwingine ni kupigania
ukombozi wa Waislamu ili washiriki katika kuandaa katiba mpya wakiwa ni raia
huru na sawa na wenzao. Waislamu popote tulipo tunao wajibu wa kuorodhesha
dhulma zote za udini tunazofanyiwa na kupigania ziondolewe kwanza na kulipwa
fidia.
(3) Kwa kuwa tangu ukoloni hadi leo Waislamu wanahesabiwa na serikali na
Maaskofu kuwa ni maadui wa kupigwa vita na wasiostahiki haki sawa na wengine, na
kwa kuwa Waislamu wameazimia kutokukubali tena kudhulumiwa na kuonewa kwa namna
yoyote ile iwayo, ni wazi kuwa hakuwezi kuwa na katiba itakayoweza kulinda haki
za madhalimu na wadhulumiwa kwa wakati mmoja. Ingawa kwa propaganda za kisiasa
Tanzania ni nchi moja, lakini kiuhalisia ni nchi yenye jamii mbili zenye hadhi
na haki tofauti kabisa. Umefika sasa wakati wa kugawana nchi ili Waislamu
wanaochukiwa na kunyimwa fursa sawa na Wakristo waishi katika maeneo yenye
Waislamu wengi na Wakristo waishi katika maeneo yenye Wakristo wengi. Mwalimu
Nyerere alipigania kwa nguvu zake zote Nigeria igawanywe ili Wakatoliki ambao
walikuwa wanadhulumiwa Nigeria wajitenge na waruhusiwe kuishi katika nchi ya
Biafra. Na katika kijitabu alichokiandika 1966 Nyerere alisema madai ya
kuhifadhi umoja wa kitaifa wa Nigeria hayana maana yoyote pale ambapo baadhi ya
raia wa taifa hilo wanadhulumiwa. Ushahidi wa dhulma za Waislamu upo wazi.
Kugawana nchi kutawawezesha Waislamu kuwa na Mahakama ya Kadhi na kujiunga na
OIC bila ya kuwakera Maaskofu. Ni wajibu wetu kulifikisha hili kwa Waislamu
wenzetu nchi nzima ili lijadiliwe zaidi kabla halijafikishwa rasmi

(4) Kwa kuwa hakuwezi kuwa na amani ya kweli bila ya haki, na kwa kuwa amani ya
Tanzania inashikiliwa na Waislamu walioruhusu dhulma hiyo, Waislamu tunayo dhima
kubwa kwa kustawi kwa Mfumo Kristo ambao sasa hapana shaka yoyote
unalisambaratisha Taifa. Lakini kama alivyosema Nyerere, anayedhulumiwa ni mtu
anayeteseka. Asipopambana na huyo dhalimu, yeye ataendelea kuteseka wakati
dhalimu anastarehe kwa amani. Akiamua kupambana, wote yeye na dhalimu
watateseka. Baada ya miaka 50 ya kuachia kundi moja la jamii likistarehe na hali
Waislamu wanateseka, umefika wakati sasa wa kugawana machungu ya udini
tuliyoyabeba peke yetu kwa miaka hamsini.
 
Tamko limetulia!
Muda utawadia!
Wanafiki Kujutia!
Nchi wataikimbia!
 
Jamani mko wapi mbona hamchangii?? au ni refu mno?? mmezoea heading za line TATU? Mie nimeleat kama lilivyo bila kuchakachua!
 
Jamani mie nimetumiwa e mail tu! just to review whats writtten. Msinihukumu bali nanyi fanyeni review zenu. Angalizo just review as a great thinker na sio mshabiki tu. Hapo tutakuwa sawa. Je wewe unasemaje?

"Haikuwa tena jambo la siri kwani walisimama wazi wazi kuwaelekeza waumini wao wampigie nani kura". Naomba reference ya hii claim.

Waliwaambia wasihangaike na maisha binafsi ya ndoa ya mgombea. Kwani tanzania tuna tabia ya kuangalia tabia za viongozi wetu hasa katika mambo ya familia, mbona skandali zipo nyingi.

"Tumeona na tumemsikia Waziri Mkuu Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda" Mhe Waziri Mkuu anamjua Mungu, anajua yanayowapata viongozi wasiotii unabii, mfano Farao, sauli na wengine wengi.

Ningependa kusisitiza kuwa na nguvu za pomoja kuishauri serikali bila kushambiliana kwa misingi ya kidini. kila dini inawaza sana kuishutumu dini nyingine, lakini kwa manufaa gani. Tuepukane na kuchanganya mambo mengi kwa wakati moja.

Hindu mandal, Aghakan, KCMC, Bugando ni mfano mzuri wa uhusiano kati ya dini na maisha ya kawaida. Dini yenye huduma nyingi kwa jamii ni ya mfano. Tujitahidi kupitia dini zetu kujenga mahospitali, mashule na vyuo ili tuwe mfano kwa matajiri na mafisadi kubadilika. haya sio maswala ya kushambuliana.

Mwalimu alitaifisha shule za kidini, akijitahidi kunyanyua upande uliokuwa chini kielimu bila kujali yeye yuko dhehebu gani. Leo sielewi kwa nini amakuwa adui wa dini fulani. nadhani tunapoteza muelekeo wa utu uzima na tunarudi utotoni, labda ufisadi unaingia kila mahali.

Yapo mengi, lakini tuweke uzalendo mbele, amani, haki, upendo ni muhimu, kumbukeni wengine tumeoleana sasa ndani hapatakalika kama viongozi wa dini mkishikana miereka.

Tushike kazi ya utumishi, utume na unabii, uchungaji, ualimu, kuubiri, uaskofu na usheha usaidie kuonya, kufundisha na kudumisha uongozi uliojaa mapenzi ya Mungu. Tusiwe mbwamwitu tuliovaa ngozi ya kondoo, tukitaka kuwahubiria kondoo.

Kamanda
 
Mbovu sana haina mantiki. Nitatoa adhabu ya kuondoa kopo la kuchambia misikiti yote.
 
Jamani mie nimetumiwa e mail tu! just to review whats writtten. Msinihukumu bali nanyi fanyeni review zenu. Angalizo just review as a great thinker na sio mshabiki tu. Hapo tutakuwa sawa. Je wewe unasemaje?

[COLOR=blue[COLOR=red]]"Haikuwa tena jambo la siri kwani walisimama wazi wazi kuwaelekeza waumini wao[/COLOR] [/COLOR]wampigie nani kura". Naomba reference ya hii claim.[/I]

Waliwaambia wasihangaike na maisha binafsi ya ndoa ya mgombea. Kwani tanzania tuna tabia ya kuangalia tabia za viongozi wetu hasa katika mambo ya familia, mbona skandali zipo nyingi.

"Tumeona na tumemsikia Waziri Mkuu Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda" Mhe Waziri Mkuu anamjua Mungu, anajua yanayowapata viongozi wasiotii unabii, mfano Farao, sauli na wengine wengi.

Ningependa kusisitiza kuwa na nguvu za pomoja kuishauri serikali bila kushambiliana kwa misingi ya kidini. kila dini inawaza sana kuishutumu dini nyingine, lakini kwa manufaa gani. Tuepukane na kuchanganya mambo mengi kwa wakati moja.

Hindu mandal, Aghakan, KCMC, Bugando ni mfano mzuri wa uhusiano kati ya dini na maisha ya kawaida. Dini yenye huduma nyingi kwa jamii ni ya mfano. Tujitahidi kupitia dini zetu kujenga mahospitali, mashule na vyuo ili tuwe mfano kwa matajiri na mafisadi kubadilika. haya sio maswala ya kushambuliana.

Mwalimu alitaifisha shule za kidini, akijitahidi kunyanyua upande uliokuwa chini kielimu bila kujali yeye yuko dhehebu gani. Leo sielewi kwa nini amakuwa adui wa dini fulani. nadhani tunapoteza muelekeo wa utu uzima na tunarudi utotoni, labda ufisadi unaingia kila mahali.

Yapo mengi, lakini tuweke uzalendo mbele, amani, haki, upendo ni muhimu, kumbukeni wengine tumeoleana sasa ndani hapatakalika kama viongozi wa dini mkishikana miereka.

Tushike kazi ya utumishi, utume na unabii, uchungaji, ualimu, kuubiri, uaskofu na usheha usaidie kuonya, kufundisha na kudumisha uongozi uliojaa mapenzi ya Mungu. Tusiwe mbwamwitu tuliovaa ngozi ya kondoo, tukitaka kuwahubiria kondoo.

Kamanda


Hapo kwenye RED.
Rejea waraka wa maaskofu wa PCT. Juu ya kumchagua :Mkristo Mwenzao. Gazeti ninalo na waraka ninao!.
Pia rejea ule wito wa maaskofu kuwa "Msichague chama chagueni mtu". Kauli ambayo mkapa aliwaeleza Maaskofu kuwa ni kauli ya kulaaniwa na hao wanaosema hivyo "WALAANIWE". Ni mashetani!.
SMS nyingi na mikutano ya siri na miito mbalimbali makanisani ni reference nyingine. Kama unataka ushahidi mwingine kamuulize KAKOBE.
 
Hapo kwenye RED.
Rejea waraka wa maaskofu wa PCT. Juu ya kumchagua :Mkristo Mwenzao. Gazeti ninalo na waraka ninao!.
Pia rejea ule wito wa maaskofu kuwa "Msichague chama chagueni mtu". Kauli ambayo mkapa aliwaeleza Maaskofu kuwa ni kauli ya kulaaniwa na hao wanaosema hivyo "WALAANIWE". Ni mashetani!.
SMS nyingi na mikutano ya siri na miito mbalimbali makanisani ni reference nyingine. Kama unataka ushahidi mwingine kamuulize KAKOBE.

utumbo mtupu!!
 
hapo kwenye red.
rejea waraka wa maaskofu wa pct. Juu ya kumchagua :mkristo mwenzao. Gazeti ninalo na waraka ninao!.
pia rejea ule wito wa maaskofu kuwa "msichague chama chagueni mtu". Kauli ambayo mkapa aliwaeleza maaskofu kuwa ni kauli ya kulaaniwa na hao wanaosema hivyo "walaaniwe". Ni mashetani!.
sms nyingi na mikutano ya siri na miito mbalimbali makanisani ni reference nyingine. Kama unataka ushahidi mwingine kamuulize kakobe.
tondo weweee
 
Nilishasema tugawane hii nchi halafu tuwaone watakavyouana hamkusikia!
 
utumbo mtupu!!
Sio suala la utumbo mtupu!![/, ni suala la kutupa qutation, hiyo reference siipati. Sasa kama ni Mchungaji mmoja alisema hivyo, au Baraza fulani lilitoa waraka, hawa wanatakiwa kufutiwa usajili. Sasa hebu tutafute hard evidence, badala ya kusema ni utumbo mtupu. Hii ni hatari kwa taifa letu. singependa sana kutumia magazeti, nimeona mara nyingine wanamisquote

Kamanda
 
Ama kweli debe tupu haliachi kutika. Katika magazeti ya leo yametoa matokeo ya mitihani ya kidato cha nne. Ukiangalia karibu 98% ya shule zilizoongoza ni seminari za kikiristu na 2% ni sekondari za Serikali. Sijaona hata seminari moja ya kiislamu.

Ukiangalia wanafunzi waliofanya vizuri best top ten majina yote ya kikiristu sijaona hata jina moja la kiislamu.

Bado masheikh wanaona wakiristu wanapendelewa shame on their face. Wakiristu wamejenga hospitali Bugando, KCMC etc wao kama masheikh watuonyesha referall hospital yao moja kama sio ukosefu wa akili. Bora hata Agha Khana anawashinda waislamu wanazo Hospitals

Nyerere alitaifisha shule zetu wakiristu ili na nyinyi waislamu muweze kusoma kwa kuondoa kisingizio eti mkienda shule mtabatizwa leo hii mnasema ndiyo adui namba moja wa uislamu Tanzania. Ama kweli shukurani ya punda ni mateke.

Masheikh hao wamekosa hata akili ya mtoto wa chekechea. Kwa taarifa ni kwamba wabunge hawateuliwi na mtu (achilia mbali wale 10 wa Rais). Wabunge wanachaguliwa na wananchi sasa hizo lawama za kuwa wabunge 75% wakiristu zinatoka wapi?

Ukweli ni kwamba waislamu including hao masheikh ni mbumbumbu mzungu wa reli na kwa mantiki hiyo mtabaki kulalamika hadi ahera. Kalaghabaho. Sasa kwa tamko kama hili kweli serikali makini itaweza kuwasikiliza? Hata mnacholalamikia hamafahamu Je mnailamimikia Serikali au Maaskofu au Wakiristu wote au Wakatoriki?!

Kama nyinyi waislamu mnajinadi kwamba nyinyi ndiye mnayemfahamu Mungu wa kweli, Mbona basi huyo Mungu wenu wa kweli hawasaidii kitu chochote na Sisi wakiristu tunao abudu Binadamu Yesu kuwa ni Mungu tuna mafanikio kuliko nyinyi?!

Mimi nafikiri huyo Mungu wenu mnayempigania (Sic) badala ya Mungu kuwapigania nyinyi (Binadamu) because is a creator si Mungu bali Shetani. Mliingizwa mkenge na Muhammed (houseboy wa wa Khadija) Njooni kwa Yesu mpate amani na hayo malalamiko yatakwisha KARIBUNI
 
Jamani mko wapi mbona hamchangii?? au ni refu mno?? mmezoea heading za line TATU? Mie nimeleat kama lilivyo bila kuchakachua!



  • Topical
    • profile.png
      View Profile
    • forum.png
      View Forum Posts
    • message.png
      Private Message
    • article.png
      View Articles
    • add.png
      Add as Contact

    user-online.png

    JF Senior Expert Member
    reputation_pos.png
    reputation_pos.png
    reputation_pos.png
    reputation_pos.png
    reputation_pos.png
    reputation_highpos.png
    reputation_highpos.png
    reputation_highpos.png
    Join DateFri Dec 2010Posts673Thanks39Thanked 110 Times in 53 Posts Rep Power21


    Did you find this post helpful? |
    icon1.png
    Tamko la waislamu (FULL TEXT)


    TAMKO LA WAISLAMU DHIDI YA KAULI ZA MAASKOFU

    Utangulizi
    Oktoba 31, 2010 Tanzania ilifanya uchaguzi mkuu ambapo wananchi walipata fursa ya kumchagua Rais, wabunge pamoja na madiwani. Katika uchaguzi huo, Watanzania kwa ujumla wao walikichagua Chama cha Mapinduzi, CCM, kuongoza tena nchi kwa kipindi kingine cha miaka mitano.

    Hata hivyo, wakati wananchi wakiamini kwamba wanaongozwa na watu waliowapigia kura, matukio yanayoendelea hivi sasa yanaashiria serikali kutelekeza majukumu yake na kuwaacha maaskofu wakielekeza nchi wanakotaka.

    Itakumbukwa kwamba awali kabla ya uchaguzi mkuu maaskofu walikuwa wametoa Ilani yao ya uchaguzi bila kueleza kipi chama chao kitakachosimamia na kutekeleza Ilani hiyo. Baadhi ya viongozi wa serikali na chama tawala, CCM, walishabikia Ilani hiyo na kuwatetea maaskofu. Kwa hakika taarifa za vyombo vya habari zilifahamisha kwamba baadhi ya watendaji waandamizi ndani ya serikali walishiriki katika kuandaa Ilani hiyo.

    Ilipofika wakati wa kampeni hadi kuingia siku ya kupiga kura, ilikuwa imedhihiri kipi kilikuwa chama cha maaskofu ambacho walitarajia kitekeleze Ilani yao. Haikuwa tena jambo la siri kwani walisimama wazi wazi kuwaelekeza waumini wao wampigie nani kura. Na katika juhudi zao za kutaka wafuasi wao wawaelewe vizuri, maaskofu walithubutu hata kuweka kando mafundisho ya Biblia yao juu ya masuala ya uzinzi wakawahimiza waumini kumpigia kura mtu wanayemtaka bila kujali kwamba anakabiliwa na kashfa ya kupora mke wa mtu. Waliwaambia wasihangaike na maisha binafsi ya ndoa ya mgombea.

    Hata hivyo, matokeo ya kura yalitoa majibu kwamba Watanzania walikuwa wameikataa Ilani ya Maaskofu.

    Waislamu tumelazimika kukutana na kutoa tamko hili kwa sababu matukio yanayotokea hivi sasa yanaonesha kuwa wale ambao Watanzania walikataa kuwapa uongozi na Ilani yao iliyoandaliwa na maaskofu, ndio sasa wanaielekeza nchi pa kwenda huku viongozi wa CCM na serikali wakijitahidi kadiri ya uwezo wao kunyenyekea kwa maaskofu hao.

    Tumeona na tumemsikia Waziri Mkuu Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda akihangaika kuwapigia magoti na kuwaomba radhi maaskofu kule Sumbawanga. Tumesikia jinsi viongozi wanaojaribu kuwaambia maaskofu kwamba kama wanataka kuingia katika siasa wavue majoho na vyeo vyao vya kikanisa kama Padiri mwenzao waliyekuwa wakimpigania kuingia Ikulu, wanavyokemewa na kutakiwa wawaombe radhi maaskofu hao.

    Lililo baya zaidi maaskofu walioshindwa kuwashawishi wananchi waipokee na kukubali Ilani yao, wamekuja na kampeni za kuchochea uasi kwa serikali iliyopo madarakani. Lakini pamoja na hali hiyo, viongozi wa CCM na serikali wamebaki wanagwaya. Hakuna aliyeweza kupata ujasiri wa kukemea hali hii. Kinyume chake Waziri Mkuu na Mzee John Samwel Malecela wanahangaika huku na kule wakiwapigia magoti maaskofu hao na kuwakemea wanaothubutu kuwakosoa.

    Hali kama hii ni hatari kwa usalama na utulivu wa nchi. Ni hali ya kuchochea udini na kuweka ombwe la uongozi wa kisiasa ambao utazua balaa. Waislamu hatuwezi kukubali hali hii. Kwa hiyo, ama CCM na serikali vitekeleze wajibu wao wa kuongoza au kama wanaona hawawezi, basi waseme rasmi ili Maaskofu na wengine wenye Ilani zao za uchaguzi waingie tena ulingoni kuomba ridhaa ya Watanzania kuongoza nchi kuliko kuishi katika hiki kiini macho ambapo maaskofu na mawakala wao ndani ya serikali wameachwa waikokote nchi wanakotaka.

    Kiini cha Hali hii ya Kisiasa
    Hali hii ya kisiasa tunayoishuhudia leo nchini mwetu ni matunda ya mbegu liliyopandwa na kupaliliwa kwa zaidi ya miaka 100 iliyopita. Wakoloni walikuwa na kanuni yao waliyoiita divide et impero yaani wagawe ili uwatawale. Huko Rwanda wakoloni waliwagawa wananchi kwa misingi ya kikabila. Watusi ambao ni watawala wapewe elimu ya juu na wanfundishwe kwa Kifaransa, na Wahutu ambao ni watawaliwa wapewe elimu duni na wafundishwe kwa Kiswahili. Ubaguzi huo wa kuwagawa raia wa nchi moja ulipandikiza sumu iliyokuja kusababisha Wanyarwanda kuuana.

    Hapa kwetu wakoloni walitugawa kwa misingi ya dini. Kabla ya uhuru wa Tanganyika, wakoloni kwa kushirikiana na makanisa waliwaona Waislamu kama ni mahasimu wao kidini na kisiasa. Na kwa sababu hiyo serikali za kikoloni zikaweka mikakati maalum ya kuwakandamiza Waislamu katika maeneo matatu: kwanza kuwawekea vikwazo katika kutangaza dini yao ili wasiongezeke; pili kuwabana katika elimu na ili kuhakikisha kuwa Waislamu wanabanwa jukumu la kuwaelimisha Waafrika likawekwa mikononi mwa makanisa na kazi ya serikali ni kuzigharimia tu shule hizo. Lengo likiwa ni kuwabatiza Waislamu wachache watakaoruhusiwa kusoma, na tatu kuwabana katika ajira serikalini kwa sababu makanisa yote yalisisitiza kuwa kuwaajiri Waislamu serikalini ni kusaidia kuenea kwa Uislamu..

    Kwa kuwa ubaguzi huo haukuwa na kificho chochote, Waislamu wengi walijitokeza kupambana na ukoloni kwa matarajio kuwa serikali huru itaondosha chuki na uadui huo dhidi ya Waislamu. Lakini msiba mkuu wa taifa hili ni kwamba kinyume chake, baada ya uhuru msimamo ukawa ni ule ule wa kuwaona Waislamu kuwa ni maadui wa kupigwa vita na mikakati ya kuwabana Waislamu katika maeneo yale matatu ikaimarishwa zaidi wakati wa utawala wa Nyerere. Kuanzia 1957 mkakati uliopangwa na Kanisa Katoliki ukawa ni kuhakikisha kuwa nafasi zote muhimu za uongozi na serikali zinashikwa na wao. [Taz. Confidential Diary – Tanganyika, March-April 1957, uk. 3-4 Maryknoll Central Archives, New York ]. Na ni mkakati huu ndio ambao Mwalimu Nyerere aliokuwa akimuhakikishia Askofu Rweyemamu mwaka 1970 kuwa anatumia mamlaka yake kama Rais na kama kiongozi wa TANU kuhakikisha kuwa anatoa upendeleo maalum kwa Wakristo ili wasimamie sera za Chama. Na kwamba amemteua padiri katika nafasi nyeti ya Chama si kwa sababu anajua siasa bali kwa sababu ni Mkristo safi. Lakini Nyerere huyo huyo akisimama hadharani alijidai kukemea udini. Na kwa kazi kubwa aliyoifanya ya kuliimarisha kanisa na kuwadhoofisha Waislamu, leo Kanisa lake limo katika mchakato wa kumtangaza Nyerere kuwa ni Mtakatifu!

    Sivalon anaarifu katika kitabu chake kuwa mara baada ya uhuru Kanisa katoliki liliwahamasisha Wakristo wote na hasa watendaji wa serikali juu ya hatari ya Ukomunisti na Uislamu na walikusanya nguvu zao zote katika kukabiliana na maadui hao.

    Matokeo ya Hujuma Hizo
    Matokeo ya hujuma hizo za kichinichini ni kwamba katika sura ya nje na katika propaganda za kisiasa Tanzania ni nchi moja yenye mshikamano na umoja na kisiwa cha amani. Lakini uhalisia wa mambo ni kuwa Tanzania ni nchi yenye jamii kubwa mbili. Jamii ya Wakristo wanaopewa msaada, upendeleo, ulinzi na heshima, na jamii ya Waislamu ambao wanachukiwa, kudharauliwa na kudhoofishwa na serikali kabla na baada ya Uhuru. Ifuatayo ni mifano michache tu ya baadhi ya hujuma hizo baada ya Uhuru.

    (1) Mwaka 1963 katika Barua ya Kichungaji, Kanisa Katoliki lilisema Waislamu walikuwa wanajenga umoja na mshikamano miongoni mwao, jambo ambalo ni "hatari kubwa kwa hatima ya Wakristo wetu" na Sivalon anabainisha kuwa Wakristo walimwomba Nyerere awasaidie kuvuruga umoja huo wa Waislamu. Ndio sababu ya Nyerere kutumia dola kuiparaganya EAMWS. Kwa kuwa Waislamu ni jamii inayotakiwa kuwa dhalili, hawatakiwi kuwa na umoja. Ndio maana tangu wakati wa Nyerere hadi leo, uchaguzi wa viongozi wa Waislamu husimamiwa na vyombo vya dola. Nia ikiwa ni kutokuwapa Waislamu uhuru wa kuwachagua viongozi wao. Katika taifa moja haki hiyo ni ya Wakristo peke yao. Sote ni mashahidi kuwa mwaka 1994 serikali ilimwagiza Naibu Waziri Mkuu Mh. Augustino L. Mrema kuhakikisha kuwa Bakwata inapitisha katiba mpya inayotakiwa na serikali. Na Maaskofu wakachangia gharama. Waislamu ni maadui kidini na kisiasa, lazima wadhibitiwe.

    (2) Mwaka 1992 Serikali ya Tanzania ilitiliana saini Makubaliano ya Itifaki rasmi na Makanisa ya TEC na CCT. Kwa mujibu wa makubaliano hayo ambayo yalitiwa saini na Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu, ambaye wakati huo alikuwa Mh. Edward Lowasa serikali imewajibishwa pamoja na mambo mengine, kutenga nafasi za masomo kwenye vyuo vyake vya Ualimu mahsusi kwa ajili ya wanafunzi wanaopangwa kufundisha katika shule za Kanisa; pia kutoa ruzuku ya kuendeshea taasisi za Makanisa. Kuanzia 1992 hadi leo serikali imetoa mabilioni ya kodi za wananchi kwa Makanisa. Katika kipindi chote hicho Waislamu wamepinga ubaguzi huo. Lakini kwa kuwa lengo ni kuwaimarisha Wakristo ambao ni jamii inayotakiwa kupewa nguvu zaidi dhidi ya jamii ya Waislamu ambao wanatizamwa kama maadui, serikali imeyapuuza malalamiko ya Waislamu. Lakini propaganda zinaendelea kuwa Tanzania ni nchi moja yenye mshikamano na umoja na ni kisiwa cha amani.

    (3) Waislamu wameiomba serikali kujiunga na OIC kama njia mojawapo itakayowezesha nchi yetu kupata misaada itakayotumika kuinua hali za Waislamu ambao wameachwa nyuma sana katika elimu na uchumi. Makanisa yote kwa kauli moja yamepinga kwa nguvu zao zote pendekezo hilo. Sababu ya kupinga kwao ni kuwa mkakati uliopo ni kuhakikisha kuwa Waislamu wanadhoofishwa katika kila hali, na ni makosa makubwa kuwaimarisha kiuchumi au kielimu maadui hao. Serikali ilipofanya utafiti wake wa kina ikajiridhisha kuwa kujiunga na OIC kuna manufaa na hakuna madhara yoyote. Na Mh. Bernard Membe alitamka hilo Bungeni. Mara akaitwa na Askofu Mkuu wa Jimbo la Dar es Salaam, Muadhama Polycarp Cardinali Pengo na kukumbushwa mkakati wa kuwadhoofisha Waislamu. Msimamo wa serikali ukabadilika. Lakini propaganda za kuwazuga Waislamu zinasema Watanzania wote ni kitu kimoja na nchi hii haina ubaguzi!

    (4) Kwa kuwa tangu wakati wa ukoloni hadi leo mkakati uliopo ni kuhakikisha kuwa Waislamu wanaminywa kadiri iwezekanavyo katika nafasi za uongozi na ajira, ndio maana hadi leo, miaka 50 baada ya Uhuru Waislamu ni wachache sana katika nafasi zote za uongozi na ajira katika sehemu muhimu serikalini na katika vyombo muhimu vya maamuzi. Kisingizio kinachotolewa ni kuwa Waislamu hawataki kusoma. Lakini ukitazama orodha ya Wakuu wa Wilaya wote walioteuliwa na sifa zao, utaona dhahiri kuwa wapo Waislamu wengi wenye sifa bora zaidi ambao wangestahili kuwa ma-DC. Waislamu hawateliwi kwa sababu mkakati uliopo ni kuwatenga Waislamu na ikiwezekana kuwaondosha kabisa katika sehemu muhimu za uongozi, kwa sababu kama wao hawajui ukweli ni kwamba hawatakiwi kushika nafasi zozote muhimu za uongozi au ajira. Ndio maana asilimia 75 ya Ma-DC wote ni Wakristo na karibu wasimamizi wote wa Uchaguzi katika wilaya ni Wakristo. Wabunge asilimia 75 pia ni Wakristo, na hali ni hiyo hiyo katika Vitengo vya serikali na Mashirika ya uma. Ndio maana hakuonekani tatizo lolote pale taasisi yote inapokuwa na Wakristo watupu. Na kelele nyingi maadui wa serikali na Kanisa wanapopewa nafasi hata kama wana uwezo kiasi gani. Katika sura ya nje Tanzania ni taifa moja, katika uhalisia wake ni kuna mataifa mawili, moja nyonge na jingine lenye nguvu.

    (5) Kwa kuwa Waislamu wanahesabiwa kuwa ni maadui, ule mkakati uliowekwa na wakoloni wa kuwawekea vikwazo Waislamu katika kutangaza dini yao unaendelea hadi leo. Ipo mifano mingi sana ya Waislamu kukamatwa, kutiwa ndani na kunyanyaswa na vyombo vya dola kwa sababu tu ya kulingania hadharani dini yao. Kwa kuwa Waislamu ni maadui, basi ni muhimu kuhakikisha kuwa hawaongezeki. Wakristo wanayo haki ya kuitisha mkutano wa hadhara na kutangaza kuwa Yesu ni Mungu. Wao ni jamii inayostahiki ulinzi wa dola. Lakini pindi Mwislamu atakaposema hadharani kuwa Mwenyezi Mungu aliyeumba mbingu na ardhi siyo Yesu mwana wa Mariamu atakuwa amekashifu dini ya dola na atakamatwa na kubughudhiwa. Lakini kipropaganda, Tanzania ni nchi moja na inafuata katiba moja. Lakini uhalisia ni tofauti.

    (6) Msimamo wa serikali na makanisa kuhusiana na mauaji ya Waislamu katika msikiti wa Mwembechai ni kielelezo kingine cha ukweli kuwa Tanzania ni mkusanyiko wa jamii mbili zenye haki na hadhi tofauti katika taifa moja. Kwa kushinikizwa na Maaskofu serikali iliwauwa Waislamu watatu Mwembechai pasi na hatia yoyote. Waislamu waliiomba Mahaka, Bunge na hata Rais aunde Tume ya uchunguzi. Mihimili yote ya dola ilikataa. Kiongozi wa Kanisa Katoliki akenda mbali zaidi. Akahalalisha mauaji hayo. Kwa sababu waliouliwa ni wale maadui wa ile jamii nyoge isiyotakiwa kustawi. Lakini alipouliwa mbwa "Imigresheni" mwaka huo huo wa 1998, Jaji Mkuu wa wakati huo Mh. Francis Nyalali aliamuru uchunguzi wa kuuliwa mbwa huyo na hakimu akaadhibiwa. Jaji Mkuu alichukua uamuzi huo bila kuombwa na mtu. Lakini wale waliowauwa Waislamu walipongezwa na kupandishwa vyeo. Uhasama wa serikali na makanisa dhidi ya jamii ya Waislamu ni wa kiwango cha kutisha. Msimamo ukawa huo huo walipouliwa Waislamu Unguja na Pemba 2001 kwa kuandamana kudai Katiba Mpya. Lakini kipropaganda tunaambiwa Watanzania wote wanahaki sawa.

    (7) Rais wa Marekani George W. Bush alipotangaza Vita vya Msalaba dhidi ya Waislamu mwaka 2001, serikali ya Tanzania ikapata uhalali zaidi wa kuzidi kuwakandamiza Waislamu. Serikali ikawa radhi kuvunja Katiba ya nchi kwa kupitisha Sheria ya Kuzuia Ugaidi ya 2002 ili zipatikane fursa zaidi za kuwanyoongesha Waislamu. Waislamu waliipinga sheria hiyo kwa nguvu zao zote, lakini kwa kuwa wao ni jamii inayotakiwa kupigwa vita hawakusikilizwa. Bunge ambalo nalo lina Wakristo wengi likaipitisha haraka sheria hiyo. Naam, tangu imepitishwa hadi leo, sheria hiyo imetumika kuwadhuru Waislamu wasiokuwa na hatia yoyote, na kufunga taasisi zilizokuwa zikiwasaidia Waislamu. Misaada ni haki ya Wakristo, siyo Waislamu. Pamoja na madhila yote hayo Waislamu wanatakiwa waendelee kuamini kuwa Tanzania ni nchi moja inayojali raia wake wote.

    (8) Wakati serikali ikidai kuwa Tanzania ni taifa ambalo raia wote wana haki sawa, lakini serikali hiyo hiyo kwa makusudi kabisa inafanya jitihada za waziwazi za kuwahamasisha Wakristo wawaone Watanzania ambao ni Waislamu kuwa ni maadui zao na maadui wa taifa lao. Januari 2001 Waziri Mkuu Mh. Frederick Sumaye alisema katika mkutano wake na waandishi wa habari kuwa serikali inazo taarifa kuwa kundi la magaidi waliopata mafunzo nchi za nje limerejea nchini na magaidi hao wanapanga kuilipua hospitali ya Muhimbili. Kufuatia kauli hiyo Waislamu watatu wa Muhimbili ambao ni Waislamu akiwemo Profesa wa Micro-Biology walitiwa mbaroni. Japo baadaye waliachiwa kwani hawakuwa na hatia yoyote, lengo la serikali la kupandikiza sumu ya chuki lilikuwa limetimia. Tarehe 24 Agosti 2001 Waislamu walifanya maandamano kupinga kufungwa kwa Dibagula kwa kusema Yesu si Mungu. Serikali kupitia jeshi la polisi likawatangazia wananchi wote kuwa Waislamu wamepanga kuyalipua makanisa siku ya Jumapili ya tarehe 2 Septemba 2001. Na serikali ikawahakikishia Wakristo kuwa itaweka maaskari wa kuwalinda na hiyo shari ya Waislamu. Lengo la uzushi huu ni kuwachochea Wakristo wawachukie Waislamu na hivyo waunge mkono hatua za serikali za kuwapa kipondo. Hivi sasa huo umekuwa ni mchezo wa kawaida. Kila baada ya muda Fulani serikali kwa kpitia jeshi la polisi hutoa taarifa za kuonesha kuwa kuna mpango wa shambulio la kigaidi. Na watuhumiwa siku zote ni Waislamu. Serikali na makanisa yanawachukia Waislamu kiasi cha kuwa tayari kushirikiana na wasiokuwa Watanzania katika kuwahujumu Waislamu. Ni dhahiri kuwa katika mazingira kama haya, Maaskofu wakipata kisingizio chochote watakuwa tayari kuwauwa Waislamu kama walivyoshiriki katika mauaji ya kimbari ya Rwanda.

    (9) Papa John Paul II alipoitembelea Tanzania mwaka 1990, Kanisa Katoliki lilimkabidhi Ripoti yenye anwani: Activities of the Church in Tanzania. Katika ripoti yake hiyo Kanisa Katoliki limetaja kuwapo kwa Tume ya Majeshi ya Kivita [Commission of Armed Forces] ndani ya Kanisa hilo. Tangu wakati huo hadi leo Waislamu wameitaka serikali iwaondoshe hofu kwa kuweka wazi kazi za Tume hiyo ya Majeshi ya Kivita ndani ya Kanisa. Serikali haijajibu na wala haijajishughulisha na taarifa nzito kama hizo. Hatujui kama Tume hiyo ya Majeshi ya kivita inafanya kazi ndani ya Jeshi la Wananchi au nje ya jeshi hilo. Lakini kwa muktadha wa hali ya uhasama wa serikali na hasa wa Maaskofu dhidi ya Waislamu wanaowahesabu kuwa ni maadui zao, si vigumu kukisia kwa nini Kanisa Katoliki limeunda Tume ya Majeshi ya Kivita. Lakini serikali ambayo haishughulishwi kabisa na Tume ya Majeshi ya Kivita ya Wakatoliki imekuwa na tabia ya kuwakamata na kuwatia ndani Waislamu kwa kesi za kuwabambikia zisizokuwa na kichwa wala miguu. Lakini propaganda zinasema Tanzania ni nchi moja yenye katiba inayolinda haki za watu wote. Mwenye mach haambiwi tazama.

    Dalili ya Mvua ni Mawingu
    Alipokuwa akitoa mada yake juu ya "Mifumo ya Viashiria vya Migogoro" katika Mkutano wa Kumi na Moja wa Hali ya Siasa Tanzania ulioandaliwa na REDET mwaka 2003, Mh. Bernard L. Membe alisema kwamba migogoro mingi duniani na hasa vita vya wenyewe kwa wenyewe vina dalili na viashiria vyake. Akasema miongoni mwa dalili kubwa kuwa nchi karibu itaingia katika machafuko ya vita vya wenyewe kwa wenyewe ni kutokea kwa mgawanyiko au kutokea kutoelewana kwa viongozi ndani ya chama au serikali tawala.

    Katika siku za hivi karibuni tumeshuhudia viongozi mbalimbali wa serikali wakiwamo mawaziri wakipingana hadharani juu ya maamuzi waliyoyafanya wenyewe. Lakini pia katika siku za hivi karibuni tumeshuhudia pia mgongano wa waziwazi kati ya wabunge wa CCM na Chama chao. Na wote hao hawachoki kujisifu kuwa wanamuenzi Mwalimu Nyerere. Lakini mwaka 1993, Nyerere katika Kitabu chake Tanzania! Tanzania! Aliandika na tunanukuu:

    Ziko jitihada sasa hivi za kugombanisha Wabunge na chama chao kwa kutumia hoja ya hadhi ya Bunge. Ni nani huyu anayefanya kazi hii? Ni haki kabisa ya vyama vya upinzani kujaribu kugombanisha Wabunge wa chama kinachotawala na chama chao. Lakini viongozi wa chama kinachotawala pamoja na Serikali yenyewe wanapojaribu kufanya mambo ambayo yatagombanisha Wabunge wa CCM na chama chao, tuna haki ya kuwauliza viongozi hao wanafanya kazi hii kwa niaba ya nani, na chama chao ni chama gani? [uk. 41]
    Pamoja na kuyajua yote hayo hivi sasa kuna msuguano ulio dhahiri kabisa baina ya Wabunge wa CCM na Chama chao. Kiashiria kingine alichokitaja Mh. Membe ni kwa serikali kushindwa kuyashughulikia malalamiko mbalimbali ya wananchi yanayoelekezwa serikalini.

    Maazimio ya Waislamu
    Kwa kuzingatia muktadha wa hali ya kisiasa ilipofikia hivi sasa, Waislamu tumefikia maamuzi yafuatayo:

    (1) Maadam Mfumo Kristo umeimarika kiasi cha kuweza kuitisha serikali na viongozi wake na wakatishika, na maadam Mfumo huo Kristo una nguvu za kuweza hata kuvitisha na kuvikemea vyombo vya dola na vikasalimu amri, Waislamu tutake tusitake, kama alivyohadharisha Mh. Membe, ukweli unabaki kuwa hautapita muda mrefu, dhulma hii ya udini italisambaratisha Taifa letu, kama udini ulivyoisambaratisha Ivory Coast ambayo katika miaka ya 1960 na 1970 ilikuwa mfano wa kuigwa.

    Hivyo basi wajibu wetu wa mwanzo ni kuufikisha ujumbe huu kwa Waislamu wote nchini, na kuwataka wazingatie kuwa kwa kuwa wanabaguliwa na kudhalilishwa katika nchi hii kwa sababu ya Uislamu wao, basi ni wajibu wao na wao kushikamana kama Waislamu.

    (2) Kwa kuwa kila wanchosema Maaskofu ndicho kinachofuatwa na serikali, na kwa kuwa Maaskofu wamekwishatamka hadharani na kwa sauti kali kuwa katika nchi yetu hakuna kabisa udini na atakayesema kuna udini basi ni yeye ndiye anayetaka kuleta udini, na kauli hiyo kudakwa na mawakala wa Maaskofu katika serikali, ni dhahiri kuwa dhulma za udini zinazoendelea kuwakandamiza Waislamu miaka 50 baada ya Uhuru hazitaondoshwa na Katiba mpya. Hivyo wajibu wetu mwingine ni kupigania ukombozi wa Waislamu ili washiriki katika kuandaa katiba mpya wakiwa ni raia huru na sawa na wenzao. Waislamu popote tulipo tunao wajibu wa kuorodhesha dhulma zote za udini tunazofanyiwa na kupigania ziondolewe kwanza na kulipwa fidia.

    (3) Kwa kuwa tangu ukoloni hadi leo Waislamu wanahesabiwa na serikali na Maaskofu kuwa ni maadui wa kupigwa vita na wasiostahiki haki sawa na wengine, na kwa kuwa Waislamu wameazimia kutokukubali tena kudhulumiwa na kuonewa kwa namna yoyote ile iwayo, ni wazi kuwa hakuwezi kuwa na katiba itakayoweza kulinda haki za madhalimu na wadhulumiwa kwa wakati mmoja. Ingawa kwa propaganda za kisiasa Tanzania ni nchi moja, lakini kiuhalisia ni nchi yenye jamii mbili zenye hadhi na haki tofauti kabisa. Umefika sasa wakati wa kugawana nchi ili Waislamu wanaochukiwa na kunyimwa fursa sawa na Wakristo waishi katika maeneo yenye Waislamu wengi na Wakristo waishi katika maeneo yenye Wakristo wengi. Mwalimu Nyerere alipigania kwa nguvu zake zote Nigeria igawanywe ili Wakatoliki ambao walikuwa wanadhulumiwa Nigeria wajitenge na waruhusiwe kuishi katika nchi ya Biafra. Na katika kijitabu alichokiandika 1966 Nyerere alisema madai ya kuhifadhi umoja wa kitaifa wa Nigeria hayana maana yoyote pale ambapo baadhi ya raia wa taifa hilo wanadhulumiwa. Ushahidi wa dhulma za Waislamu upo wazi. Kugawana nchi kutawawezesha Waislamu kuwa na Mahakama ya Kadhi na kujiunga na OIC bila ya kuwakera Maaskofu. Ni wajibu wetu kulifikisha hili kwa Waislamu wenzetu nchi nzima ili lijadiliwe zaidi kabla halijafikishwa rasmi

    (4) Kwa kuwa hakuwezi kuwa na amani ya kweli bila ya haki, na kwa kuwa amani ya Tanzania inashikiliwa na Waislamu walioruhusu dhulma hiyo, Waislamu tunayo dhima kubwa kwa kustawi kwa Mfumo Kristo ambao sasa hapana shaka yoyote unalisambaratisha Taifa. Lakini kama alivyosema Nyerere, anayedhulumiwa ni mtu anayeteseka. Asipopambana na huyo dhalimu, yeye ataendelea kuteseka wakati dhalimu anastarehe kwa amani. Akiamua kupambana, wote yeye na dhalimu watateseka. Baada ya miaka 50 ya kuachia kundi moja la jamii likistarehe na hali Waislamu wanateseka, umefika wakati sasa wa kugawana machungu ya udini tuliyoyabeba peke yetu kwa miaka hamsini.


    WABILLAHI TAWFIQ




    progress.gif
    Reply Reply With Quote Thanks
  • Remove Your Thanks
    The Following 39 Users Say Thank You to Topical For This Useful Post:

    Adili (20th January 2011), Aikaotana (19th January 2011), Anold (21st January 2011), Baba Mtu (19th January 2011), babayah67 (19th January 2011), ByaseL (20th January 2011), Fernandes Rodri (19th January 2011), Ibrah (20th January 2011), Invisible (19th January 2011), Junius (21st January 2011), KALAMAZOO (20th January 2011), kalamuzuvendi (19th January 2011), KAUMZA (20th January 2011), kayumba (21st January 2011), kishalu (21st January 2011), Lekanjobe Kubinika (20th January 2011), limited (19th January 2011), M TZ 1 (19th January 2011), mapambano (20th January 2011), matungusha (22nd January 2011), MFUKUNYUKU (21st January 2011), Mohammed Shossi (19th January 2011), mpevu (19th January 2011), Mtumishi (19th January 2011), muhogomchungu (19th January 2011), Mzee Mwanakijiji (19th January 2011), Nyumbu- (21st January 2011), Nyunyu (19th January 2011), oba (20th January 2011), Questt (20th January 2011), Recta (20th January 2011), rreporter2010 (20th January 2011), Safari_ni_Safari (20th January 2011), Shkh Yahya (21st January 2011), Sn2139 (20th January 2011), STEIN (20th January 2011), Steve Dii (19th January 2011), Wun (24th January 2011), Xuma (21st January 2011)​


 
Back
Top Bottom