Tamko la serikali kuhusu mauaji Tarime?

Tamko la serikali kuhusu mauaji Tarime?




Katika hali ya kutafuta suluhu kati ya wananchi, mgodi na polisi, kesho Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu), Steven Wassira amepanga kukutana na viongozi wa vijiji vya Kewanja, Nyangoto, Matongo, Genkuru, Nyamwaga, Nyakunguru na Kerende.

Baadhi ya viongozi wa vijiji hivyo walilithibitishia gazeti hili lakini wakasisistiza haki za wananchi lazima zipatikane.

Chanzo: Mwananchi

Huyu waziri anatakiwa kwenda nyamongo akawaeleze wananchi hatua zilizochukuliwa na serikali juu ya askari waliouwa wananchi wasio na hatia.

Vile vile anatakiwa kuwaeleza wananchi ni hatua gani zinachukuliwa kulipa fidia wananchi wa nayamongo na maeneo jirani ambao wamekuwa wakiathiriwa na shughuli za mgodi wa north mara kuanzia kutiririsha maji yeneye kemikali hadi mauaji ya kirejareja yanayofanywa na jeshi la pois dhidi ya raia wema.

Kama hatokuwa na majibu ya kueleweka, atastahili kupopoewa mawe kama nyangwini ili wakajipange upya!!
 
Hii ndio dhana ya polisi jamii wanayofundishwa na afande MWEMA.
 
Hayo ndiyo ya afande mwema na Polisi jamii/ulinzi shirikishi.
 
Nimejaribu kusikiliza kwa makini sana kama nitasikia tamko lolote kutoka serikalini kuhusu mauaji ya wananchi huko Tarime yaliyofanywa na polisi. Sijasikia kiongozi yeyote katika ngazi za juu akitoa rambi rambi kwa wafiwa, kuomba radhi na kuelezea ni nini kitakachofanyika baada ya kubainika kuwa marehemu hawakuwa majambazi, bali waliuawa na polisi bila marehemu kuwa na makosa. Kitu ambacho nimekuwa nikikisikia kutoka vyombo mbalimbali vya serikali, mojawapo vikiwa ni polisi, ni kukisakama chama cha CHADEMA kwa kuwa karibu na wafiwa na wahanga wote kwa ujumla, na kusema kuwa chama hicho ndicho chanzo cha vurugu zilizotokea.

Ni dhahiri kwamba wananchi watajuwa wanaunga mkono wote ambao wapko karibu nao na wanaolinda maslahi yao. Upendo kutoka kwa wananchi haulazimishwi, bali unapatikana kwa kuwapa na kuwaonyesha upendo vilevile. Viongozi tuchukue tahadhari hiyo.
 
Chadema inakua karibu baada ya kuona watu wamekufa ndio timu yote ikahamia Tarime safari hii hadi Babu yenu Bepari Edwin Mtei alienda Tarime kuandaa maandamano! Mmezimwa vizuri sana Kimyaaa hakuna maandamno kama mlivyo taka! Chama kinaenda kwa matukio! CDM Hopeless kabisa!
 
! Chama kinaenda kwa matukio! CDM Hopeless kabisa!

Kwa hiyo wewe watu kupoteza maisha sio tukio? Hivi unajua maana ya hope wewe? Hope is the belief in a positive outcome related to events and circumstances in one's life...its the hope that CHADEMA has for TANZANIANS
 
Hivi CDM suala la Meya Arusha limewashinda kabisa? Pamoja na watu wa tatu kufariki naona na madiwani wenu kususa naona mmeshindwa na kukubali yaishe! Eti maandamano ya mikoa ya kusini unaleta swaga ya kuwambia tunataka uchaguzi wa meya arusha urudiwe,watu wa mbeya,ruvuma na umeya Arusha hakuna uhusiano kabisa! Sasa mlitaka mlete ujinga wenu tarime!? Serikali itoe tamko la nini sasa? Kuhusu hao wavamizi wa mgodi? Chadema maiti za watu sio dili ya kupata umaarufu wa kisiasa! Wajinga wakubwa mnafikiri kwa kutumia magoti
 
Kwa hiyo wewe watu kupoteza maisha sio tukio? Hivi unajua maana ya hope wewe? Hope is the belief in a positive outcome related to events and circumstances in one's life...its the hope that CHADEMA has for TANZANIANS

Kaimbe taarabu wewe usitake kujifanya una akiri ya kufundisha watu hapa JF,kawafundishe viongozi wako wa Chadema
 
Chadema inakua karibu baada ya kuona watu wamekufa ndio timu yote ikahamia Tarime safari hii hadi Babu yenu Bepari Edwin Mtei alienda Tarime kuandaa maandamano! Mmezimwa vizuri sana Kimyaaa hakuna maandamno kama mlivyo taka! Chama kinaenda kwa matukio! CDM Hopeless kabisa![/QUOTE]
Ushindwe! Wewe ndiyo hopeless na CCM yako.
Kazi kuhudhuria kwenye misiba ya Mashehe tu.

 
Serikali imekwenda likizo. Wakati watu wanauawa ovyo wako kimya, CDM wamefuatilia hilo wakuu wa serikali ya ccm wanawaita wavunja amani. Walioiba maiti na kuwadhalilisha marehemu na ndugu zao walikuwa polisi. Katika nchi zenye demokrasia ya kweli ilibidi baada ya polisi kukiri kuwa wao ndio walioiba maiti hizo kutoka mortuary na kuzitupa mitaani, wangewajibika kwa kujiuzulu. Hata hao waliowapiga risasi hao marehemu serikali ingepaswa ichukue hatua mara moja dhidi yao kwa kuwafungulia mashitaka, kwa kuwa wanajulikana. Badala ya kufanya hiyvo serikali ya ccm ikawakamata ndugu pamoja na wanasheria wao. Tundu Lissu alikuwa Tarime kama mwanasheria wa familia mojawapo. Sasa wananchi wanaliona hilo, na CDM wanaliona. Iko siku haki yetu itapatikana.

Tumeonewa kiasi cha kutosha, tumenyonywa kiasi cha kutosha, tumepuuzwa kiasi cha kutosha. Sasa tunataka mapinduzi, ili tusionewe tena, tusinyonywe tena na tusipuuzwe tena!

Maneno haya yaliyokuwa kwenye Mwongozo wa TANU wa mwaka 1971, ndiyo kauli mbiu yetu itakayotutoa kwenye mikono ya mafisadi na kuturudisha hadhi mamilioni ya watanzania wanyonge. Sio siri, tumechoka!!!
 
Chadema inakua karibu baada ya kuona watu wamekufa ndio timu yote ikahamia Tarime safari hii hadi Babu yenu Bepari Edwin Mtei alienda Tarime kuandaa maandamano! Mmezimwa vizuri sana Kimyaaa hakuna maandamno kama mlivyo taka! Chama kinaenda kwa matukio! CDM Hopeless kabisa!
Edwin Mtei anahusika vipi na taarifa rasmi ya serikali kuhusu mauaji hayo? Kipi kilitokea kwanza, mauaji au kuzimwa kabisa? Naona bado unashikilia swala la Chadema badala ya mauaji ya wananchi. Mbona una jazba namna hiyo, au huna jibu kuhusu swali langu? Naona umefanya hili jambo la kibinafsi. Kwa taarifa yangu mimi sio Chadema wala si mwanachama wa chama chochote, nimeuliza hapa kama Mtanzania yoyote ambaye ana uhuru wa kujiunga na chama chochote. Lakini kama nilikuwa na nia ya kujiunga na ccm tena (nilikuwa mwanachama hai wa ccm tangu 1977), sina hamu ya kujiunga nacho sasa kama washabiki wake wana mawazo kama yako!
 
hivi cdm suala la meya arusha limewashinda kabisa? Pamoja na watu wa tatu kufariki naona na madiwani wenu kususa naona mmeshindwa na kukubali yaishe! Eti maandamano ya mikoa ya kusini unaleta swaga ya kuwambia tunataka uchaguzi wa meya arusha urudiwe,watu wa mbeya,ruvuma na umeya arusha hakuna uhusiano kabisa! Sasa mlitaka mlete ujinga wenu tarime!? Serikali itoe tamko la nini sasa? Kuhusu hao wavamizi wa mgodi? Chadema maiti za watu sio dili ya kupata umaarufu wa kisiasa! Wajinga wakubwa mnafikiri kwa kutumia magoti

busara hainununliwi, karibu kibaraka wa magamba!
 
Chadema inakua karibu baada ya kuona watu wamekufa ndio timu yote ikahamia Tarime safari hii hadi Babu yenu Bepari Edwin Mtei alienda Tarime kuandaa maandamano! Mmezimwa vizuri sana Kimyaaa hakuna maandamno kama mlivyo taka! Chama kinaenda kwa matukio! CDM Hopeless kabisa!

Wee ndie hopeless kila mahali
 
Hivi CDM suala la Meya Arusha limewashinda kabisa? Pamoja na watu wa tatu kufariki naona na madiwani wenu kususa naona mmeshindwa na kukubali yaishe! Eti maandamano ya mikoa ya kusini unaleta swaga ya kuwambia tunataka uchaguzi wa meya arusha urudiwe,watu wa mbeya,ruvuma na umeya Arusha hakuna uhusiano kabisa! Sasa mlitaka mlete ujinga wenu tarime!? Serikali itoe tamko la nini sasa? Kuhusu hao wavamizi wa mgodi? Chadema maiti za watu sio dili ya kupata umaarufu wa kisiasa! Wajinga wakubwa mnafikiri kwa kutumia magoti
Tumefahamishwa na vyombo vya habari kuwa hawakuwa wavamizi wa mgodi na serikali (polisi) ikatoa coffins na pesa za mazishi kwa wafiwa. (Leo nimesoma mahali kuwa polisi walilazimisha wazikwe kwa kutumia coffins hizo za polisi). Itakuwaje unabadili hapa na kutufanya kuwa walikuwa ni wavamizi wa mgodi? Hata hivyo, serikali haioni kwamba kuna haja ya kutoa tamko hapa, maana jambo hili limeongelewa sana hata kuvuka mipaka ya nchi na kuwa ni polisi walifanya mauaji hayo kwa wananchi? Kuna leo na kesho, angalia jana Mladic kakamatwa na si punde atafikishwa the Hague. Viongozi hawaoni hatari hiyo? Mwisho, mimi sio mwanachama wa Chadema, ni Mtanzania wa kawaida ambaye amestushwa na vitendo vinavyotokea. Nahisi sio mimi peke yangu.
 
Hivi CDM suala la Meya Arusha limewashinda kabisa? Pamoja na watu wa tatu kufariki naona na madiwani wenu kususa naona mmeshindwa na kukubali yaishe! Eti maandamano ya mikoa ya kusini unaleta swaga ya kuwambia tunataka uchaguzi wa meya arusha urudiwe,watu wa mbeya,ruvuma na umeya Arusha hakuna uhusiano kabisa! Sasa mlitaka mlete ujinga wenu tarime!? Serikali itoe tamko la nini sasa? Kuhusu hao wavamizi wa mgodi? Chadema maiti za watu sio dili ya kupata umaarufu wa kisiasa! Wajinga wakubwa mnafikiri kwa kutumia magoti

Jina la Baba yako halifanani na ulichokiandika. Au hilo jina umelitumia tu, hufahamu maana yake? Badilisha hilo jina halikufai. Hayo sio maneno yanayopaswa kutamkwa na Mzee Marwa.
 
Back
Top Bottom