Tamko la Chama Cha Walimu(CWT)


Pole sana na Hongera Mukoba kwa uamuzi mwafaka.

Rais Kiwete ni kama mwendawazimu kwa hiyo kushindana naye na wewe unaweza kuonekana kama mwendawazimu. Wazungu wanasema, "Never argue with a fool,people may not notice the difference" .


Watanzania tumeshajua kwamba Serikali ya CCM inayoongozwa na Rais Kiwete HAITAWAHI KUSIKILIZA MADAI YA WAFANYAKAZI WA IDARA YOYOTE HAPA TANZANIA. Tumeona hivyo kwa Madaktari na sasa kwa Waalimu! Kila siku wimbo ni uleule wa serikali haina pesa na madai ya wafanyakazi hayatekelezeki! Lakini Pesa ya KULIPA WABUNGE POSHO ZAO NA MISHAHARA MINONO IPO!PESA YA KULIPA MAFISADI IPO! PESA YA KUNULILIA MASHINGINGI IPO,PESA YA KULIPA WAFANYAKAZI HEWA IPO!!!

MIMI NIWAOMBE WAALIMU WOTE KWA UMOJA WAO,KWAMBA MWAKA 2015 HAUKO MBALI SANA. KAZI ILIYOBAKI NI KUIADHIBU SERIKALI YA CCM KWENYE SANDUKU LA KURA,FULL STOP! NAJUA WAALIMU MUNA USHAWISHI MKUBWA NA MNAWEZA KUHAMASISHA WAPIGA KURA KUKIKATAA CCM KWENYE SANDUKU LA KURA!

Wasalaam.
 
Huhitaji kuwa Sheikh Yahaya kulitambua tamko litakalotolewa. Waalimu wataagizwa warudi kazini wakati chama kinaendelea na taratibu za rufaa!
Hiyo ndo serikali yetu ya TZ. Kila mgomo wanakimbilia mahakamani badala ya kuleta suluhu. Okay, baada ya mgomo wa madaktari na walimu sasa mgomo unaofuata ni wa mahakimu na majaji, tuone serikali itakimbilia wapi kukata rufaa.
 

Mujwahuzia nimeipenda sana hii. Ni falsafa nzuri. wajikite kufundisha vizuri kwa bidii. Kila mwalimu akiingia atumie dak 5 au 10 za mwanzo kufundisha umuhimu wa mabadiliko kwenye nchi hii baadaye ndo afundishe somo. Watoto wanajua mazingira wanayosomea kwamba ni magumu. Muwaambie hali halisi. Mkifanya hivi 2015 nchi itashuhudia mabadiliko makubwa. Ukisoma kile kitabu cha THE ONE BILLION DOLLAR QUESTION: How Can Tanzania Stop Losing So Much Tax Revenue? http://www.policyforum-tz.org/files/ONEBILLIONDOLLARQUESTION.pdf utapata jibu pesa zitapatikana wapi za kuwalipa walimu na madaktari wetu. Hizi tasnia kwa zingetakiwa kulipwa vizuri hadi watu watamani kuwa waalimu. Inatia aibu ukimuuliza mtoto anayefanya vizuri darasani kama atapenda kuwa mwalimu, atakuambia hapana. maana hata watoto wanaiona hiyo kazi ni dhalili. Yoyote atayeingia madarakani 2015 itabidi aheshimu walimu na kujali maslahi yao. Mimi nafurahi hii ni hatua muhimu sana ya kuiangusha CCM. Wananchi wote tuhamasike kupiga kura kwa nguvu tupigie watu wowote wengine isipokuwa hiki chama kinachoangamiza nchi yetu. haya ni mateso ya muda tu walimu wetu vumilieni lakini msambaze elimu ya uraia kila sehemu mnayoishi. Tunawategemea nyinyi ndo viongozi wetu ndo mmetufikisha hapa tulipo.
 

we we we! walimu wanavyoipenda ccm! hahaha leo ndio waiache mwe!
 
...uliositishwa ni mgomo wa kwenda kazini(shuleni),je ule mgomo wa kufundisha kwa moyo wa dhati utasitishwa line?...
 
Asante Mkoba kwa kumaintain deginity ya walimu machoni pa umma.. Huu mgomo umesitishwa kwenye vyombo vya habari lakini MASHULENI MGOMO UKO PALEPALE

MAJIBU KWA WAKOSOAJI WETU MTAYAPATA KWA WATOTO WENU

Tumekupata mwalimu.
Wale wenzio wanaofundisha sayansi waambie kwenye maabara waongeze curriculum ya practical za maabara ya kutengeneza mabumo ya petroli na TNT.
Kuna haja ya vichwa flani vya nazi kupasuliwa upesi!
 
Kweli Tanzania ni kichwa cha mwenda wazimu.
Hivi kuna mgomo mbaya kama mgomo baridi walimu waliouanza miaka kama 7 iliopita?
Jiulize kama walimu hawakuwepo kwenye mgomo kwa miaka mingi,
-IWEJE MTOTO AFAULU STD 7 KUJIUNGA FORM 1 HUKU HAJUI HATA KUSOMA SEMBUSE YA KUANDIKA?
Na hakuna anayehoji nini kinachoendelea chini ya kapeti.
Huwezi shindana na mtu mzima mwenye akili timamu.PERIOD.
 
Kusalimu amri pia ni jibu Watanzania sisi ni waajabu sana hata watu toka nchi zingine wanatushangaa sana.
Hasa wakitembelea migodi yetu na kuona wananchi wa eneo hilo walivyo hohehahe wanatushangaa sana,wakitembelea Mbuga zetu za wanyama wakiwaona wananchi wetu na wanapoona hali za Wa-Tanzania na wanapomuona Mr.Dhaifu wakiongozana na Mzee wa Liwalo na Liwe wakitembeza Bakuli nje ya nchi wanatushangaa sana,wakiwaona walimu wetu walivyo wanazidi kutushangaa kweli hii ni aibu kwetu na serikali yetu tutaendelea kuwa omba-omba na kubadilisha sheria ya Mafao ya wafanyakazi wetu ili tu Mradi wakubwa wetu wapate sehemu ya kwenda kukopa hizo pesa wakati wafanyakazi wetu wakiwa hoi bin taabani
 

endelea kujifariji mkuu
 

Nimeipenda sana hii ingawa wengi sana hawatakuelewa. Umetumia falsafa ya juu sana kuinanga serikali. Big Up!
 
Ama kweli ccm ni janga!


Ila hakika mwisho wao waja!
 
serikali yapaswa kuwa makini katika kumaliza na kuangalia suluhisho la kudumu ili icjitokeze tena
 
Tufanye kazi kwa bidii ili tuijenge tanzania yetu,.mungu ibariki tanzania,mungu wabariki watanzania
 
Kama mapambano huwezi hakuna haja ya kuanzisha! kulikuwa hakuna haja ya kurudi nyuma
 
Kwanini hapa tanzania kumeanza kujengeka na kuzoeleka haka katabia cha mambo kutokwenda hadi migomo?
 
wewe ndio mnafiki mkubwa kwa kujitahidi kupandikiza chuki kwa wananchi.CWT inakula pesa za walim kwa kuwakata mishahara yao kila mwezi tena wengine bila ridhaa yao.huo nao ni ufisadi mkubwa.

Ukweli.....unauma...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…