TAMISEMI toeni tamko, ni watumishi wa aina gani wanastahili kupanda madaraja?

Trust None

JF-Expert Member
Feb 12, 2018
1,260
4,415
Kuna waraka ulitolewa mwezi april kuhusu aina ya watumishi wanaostahili kupanda madaraja ya utumishi, lakini naona kila wilaya ikipandisha kivyake bila kujali kigezo kikubwa cha kutumikia daraja kwa miaka minne na utendaji bora wa kazi.

Kwa mfano, kuna ajira mpya za 2012 na 2013 wameenda masomoni mwishoni mwa 2017 na 2018 lakini walikuwa wamekaa vituoni kwa zaidi ya miaka 4 ila unaambiwa hawastahili kupanda. Kwanini?

Kuna wengine walipanda 2013 na wakaenda masomoni mwishoni mwa 2017 na 2018, eti nao hawapandi! Kwanini?

Kuna baadhi ya halmashauri zimepandisha 2012 tu, wengine 2013, wengine 2014, huku wengine wakipandisha wote (2012, 2013 na 2014) ila cha ajabu ni kwamba mshahara haujabadilika! Je, nani alaumiwe? Serikali au Wakurugenzi?

TAMISEMI majibu yenu yanasubiriwa, kwa maana watumishi wakienda kuulizia wilayani wanaambiwa wawaulize TAMISEMI.
 
Wanaopanda madaraja ni wale tu wa vyombo vya ulinzi wa CCM, wengine kapandeni Mfugale Flyover
 
Kuna jamaa wa 2012 kakosa. nafasi zote ni za Walimu. Kada nyingine unakuta nafasi moja wkt wao wapo 5. Hatari sana. Inasikitisha kimsingi
 
Kuna jamaa wa 2012 kakosa. nafasi zote ni za Walimu. Kada nyingine unakuta nafasi moja wkt wao wapo 5. Hatari sana. Inasikitisha kimsingi

Hata hao walimu wa 2012 unaowasema, sehemu nyingi bado hawajapandishwa.
 
Kuna waraka ulitolewa mwezi april kuhusu aina ya watumishi wanaostahili kupanda madaraja ya utumishi, lakini naona kila wilaya ikipandisha kivyake bila kujali kigezo kikubwa cha kutumikia daraja kwa miaka minne na utendaji bora wa kazi.

Kwa mfano, kuna ajira mpya za 2012 na 2013 wameenda masomoni mwishoni mwa 2017 na 2018 lakini walikuwa wamekaa vituoni kwa zaidi ya miaka 4 ila unaambiwa hawastahili kupanda? Kwanini?

Kuna wengine walipanda 2013 na wakaenda masomoni mwishoni mwa 2017 na 2018, eti nao hawapandi! Kwanini?

Kuna baadhi ya halmashauri zimepandisha 2012 tu, wengine 2013, wengine 2014, huku wengine wakipandisha wote ila cha ajabu ni kwamba Malipo hayajabadilika!

Je, nani alaumiwe? Serikali au Wakurugenzi?

TAMISEMI majibu yenu yanasubiriwa, kwa maana watumishi wakienda kuulizia wilayani wanaambiwa wawaulize TAMISEMI.
Huu mkanganyiko ndiyo serikali inautaka ili uhakiki uanze
 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Vijana na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama ameipongeza Bodi ya wadhamini na menejimenti ya Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jami (NSSF) huku akiitaka kuongeza nguvu katika kuandikisha wanachama kwa sababu sekta binafsi ina wanachama wengi wanaotakiwa wajiunge katika shirika hilo.

Source: https://www.mwananchi.co.tz/habari/...u-kuongeza-/1597296-5142318-303rpi/index.html


Wananchama wa Sekta binafsi - Hawana FAO LA KUJITOA

Hilo Fao la Kukosa Ajira ni Sheria za kikoloni - ukiresign au ukiacha kazi mwenyewe hupati haki

Nani asiejua manyanyaso ya Sekta binafsi? Viwanda vya Wahindi na makapuni yao?

Nani asiyejua magonjwa kutokana na machemically

Je - Lile TAMKO la Raisi kufuta Sheria mpya za mafao mpaka 2023? linahusu?

NSSF wamezidi kushikilia Hakuna Malipo ya mkupuo
 
Back
Top Bottom