Shibuda yupo Makini na ana maanisha anachokiongea ni kwa vile watu wengi hawamuelewi hisia zake ila ni mpambanaji hasiyemuogopa mtu na pia anayeongea ukweli bila kuulemba, hili swala la Posho filosofia ya Shibuda haieleweki kwa sababu wengi wetu tunapenda wana siasa waongo na wanatuhadaa ndio maana tuna sema fulani yupo zaidi ya kuliko fulani, Shibuda anaweza kuwa anapinga Posho kwa dhati kuliko hao wanaongea kuonyesha kwao wao ndio wapingaji namba moja huku wanaichukua na wamekuwa wanaichukuwa miaka yote maana hata hao wanahadaa sasa hivi wamekuwepo Bungeni miaka kadhaa na wamekuwa wakipokea hizi posho mbona hawakuwai kusema hawazitaki? Hapa mjinga na anayeumia ni sisi ambao tunajiliwaza na kuishi kwa imani juu ya maneno ya wanasiasa.