Tambua kama unadukuliwa WhatsApp yako

SangaweJr

JF-Expert Member
Oct 28, 2012
2,972
2,633
Zifuatazo ni hatua jinsi ya kuhakiki kama kuna mtu ana dukua mawasiliano yako ya WhatsApp kupitia kipengele cha Whatsapp web kwa wenye simu yako.
Kwakuwa kipengele hicho kiliwekwa kwaajili ya mtumiaji wa whatsapp aunganishe whatsapp account yake na pc, ili anapokuwa mbali na simu au pc aendelee kuwa connected.

Hatua ya 1.
Fungua whatsapp yako kisha upande wa juu kulia utaona vidoti vitatu (angalia mshale) gusa hapo itakuja menu.
52fc24f62d713b46299b039c0755b7c0.jpg


Hatua ya 2
Katika menu itakayotokea hapo angalia neno whatsapp web kisha gusa hapo.
8ee2ef6f2a9f66747612e441f271012e.jpg


Hatua ya 3.
Angalia kama utapata majibu yafuatayo.

Jibu A
Kama whatsapp yako ikija hivi
932bd7453800144874f3f575301b2309.jpg

Tambua upo safe hakuna mtu anadukua mawasiliano yako kwa njia hiyo ya whatsapp web kuputia App zilizo playstore.

Jibu B
Ukigusa lile neno whatsapp web ikafunguka hivi
6693875404337a2d71b34fcaa0077e93.jpg

Tambua kuna unauwezekano mtu anadukua mawaailiano yako ya whatsapp.
Kwa njia ya computer/laptop au kwa njia ya App ambazo zipo nyingi mno playstore.
Kama ni wewe mwenyewe uli unganisha kwa pc au hizo App hakuna shida.

Ila kama sio wewe
Ili kujiondoa gusa hayo maneno ya blue hapo chini yanayo sema log out from all computers


UPDATE
JINSI YA KUDUKUAA


MAUTUNDU: Namna ya kusoma chat za mwenzako za WhatsApp bila yeye kujua

NB: NIKOSA KISHERIA KUFUATILIA MAWASILIANO YA MTU BILA RIDHAA YAKE.

Nawasilisha.
 
Back
Top Bottom