Tambua aina hii ya utapeli

Tambua aina hii ya utapeli

Fasouls

JF-Expert Member
Joined
Jun 24, 2011
Posts
937
Reaction score
321
Utapeli hutokea sana kwa watu wanaoenda kuweka pesa banki
Mara nyingi ikiwa unaenda weka pesa bank huwa kuna vile vikaratasi ambavyo unatakiwa kujaza ndio uweke pesa,kwa wale ambao wanatabia ya kujaza palepale bank, jifunze kuwa na hivi vikaratasi nyumbani kwako ama mahali pako pa biashara ili uweze epuka utapeli huu.

Utapeli wenyewe uko hivi, ukiwa unaendelea kujaza kile kikaratasi unakuja jamaa au mdaa nae hujifanya anajaza kikaratas kama chako,huku bila wewe kugundua anachabo ni kiasi gani cha pesa unataka weka,ikiwa ameridhishwa na kiasi hicho ana mbipu mshirika wake alie nje,aje eneo ulipo wewe ili akufanyie utapeli.

Huyo dada au jamaa akiingia ndani moja kwa moja hadi kwako ataanza kukuambia samahi kaka au dada naomba unisaidie nitawezaje kubadili hizi pesa za kisomali (wakat huo atakuonesha US dolla kama elfu 20 nakuendelea) wakati huo huo yule jamaa aliembipu yupo pembeni nae anasikiliza,nae bila kuulizwa atadakia atakwambia hizo sio pesa za somali ni dolla,atakwambia tumsaidie.

Ila atamwambia yule dada au kaka anaetaka kuchange kwamba atawalipa bei gani,na yule anaetaka kuchange atasema ntawalipa milioni mbili kila mmoja (kwan kwa haraka haraka ukichange dolla elfu 20 ni kama mil 32 za tsh)

Then,atasema mtoke nje huku ukiwa bado hujapeleka hzo pesa zako kwa teller,atakuambia utapeleka ukirudi ngoja tukapate hela ya bure mana jamaa/mdada mwenyewe anaonekana mshamba),kwa akili ya haraka haraka utakubali,mtatoka

Mkifika uko nje yule dada au mkaka (mara nyingi wanatumiwa wadada) atasema naomba msimwambie mtu na mnisaidie pia mana mimi mgeni na maswala ya bank,pia atasema naomba aende mmoja na nibaki na mmoja hapa mana siwezi kaa bank mana hz ela nimeziiba hoteli kwa wasomali wanaweza kuja bank wakanikuta

Then,yule dada atakuteua wewe ndie ukachange,kwahyo atakubidhi zile dolla elfu 20,hapo hapo ataomba ashike pesa zako ulizotaka kuchange kama dhamana, USIKUBALI KWANI HIZO DOLLA NI ZA BANDIA,zaidi wakomalie kuwa wana pesa bandia kwahyo unawahitia polisi.
 
Mmh sasa hapo si nitawaelekeza dirisha la customer care kuhusu foreign currency exchange nishawakwepa
 
Inaendelea.....
kwan ukienda ukirudi hutakuta mtu,
kama umeelewa gonga like..!! by mkubwa Fasouls
 
Last edited by a moderator:
mabwege ndo wataibiwa ukiwa mjanja hawakupati ng'o!
 
Yani mtu aingie mpaka bank halafu asijue kabeba pesa ya nchi gani kweli? kama kusoma hajui je picha?
 
Utapeli auna mjanja ilo linawezekana sana, chamsingi ni kuwa makini la sivyo mtabaki kujuta wakati kinga ni bora kuliko tiba
 
labda kama wana ndumba ila hivihivi bado hawajanipata iasee
 
Ukijifunza kuwa BURE GHARAMA huwezi kutapeliwa.
Ukijifunza kutokuwa na TAMAA huwezi kutapeliwa.
Ukijifunza kuwa na SUBIRA huwezi kutapeliwa.
Ukififunza KUFIKIRI hutotapeliwa kamwe. Hebu fikiria MTU anaingi bank, badala ya lichenji hela dirishani anataka achenji mkononi. Huu ni ujinga wa Kwenye...Yaani huoni kuwa kuna namna.????
 
Inaendelea.....
kwan ukienda ukirudi hutakuta mtu,
kama umeelewa gonga like..!! by mkubwa Fasouls

Wewe siyo Fasouls ila ni Fool! Utapeli wa kitoto hivyo utaukubalije? Huo wanafanyiwa huko huko kijijini kwenu!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom