PreGE2025 Tamasha la kuombea uchaguzi mkuu 2025 laungwa mkono na hotuba ya rais Samia

PreGE2025 Tamasha la kuombea uchaguzi mkuu 2025 laungwa mkono na hotuba ya rais Samia

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Ambakucha

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2019
Posts
403
Reaction score
676
Wakati maandalizi ya Tamasha la Kuombea Uchaguzi Mkuu 2025 yakipamba moto wake, hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan nayo imekazia amani na utulivu kipindi cha uchaguzi.

Akihutubia kwenye Baraza la Eid El Fitr kwenye Ukumbi wa Julius Nyerere jijini Dar, Rais Samia amewataka viongozi wa dini kuomba amani kuelekea Uchaguzi Mkuu na kukemea viongozi wenye matamko yenye kushiria vurugu.

Hotuba ya Rais imekwenda sambamba na wazo la Mkurugenzi wa Msama Promotion, Alex Msama kuandaa tamasha la kuombea Uchaguzi Mkuu mwaka huu.

Kwa mujibu wa Msama, lengo la tamasha hilo litakalofanyika Mei, 2025 ni kumlilia Mungu ili taifa la Tanzania lipite salama kwenye kipindi hiki kuelekea uchaguzi mkuu na siku yenyewe hadi kuapishwa rais ajaye.
Mbali na Rais Samia kusisitiza hayo kwa viongozi wa dini, pia alisema licha ya kuwepo kwa vyombo vya ulinzi kusimamia wajibu wao lakini viongozi wa dini waendelee kuhubiri amani ya nchi.

Aidha, akizungumza katika Baraza hilo, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert John Chalamila naye aliwahakikishia wananchi wa Dar es Salaam na nchi nzima (kwa niaba ya wakuu wa mikoa wenzake) nchi ipo salama, ina amani hivyo, wafanyabiashara wakubwa hawana sababu ya kuondoa pesa zao benki wakiamini kutakuwa na vurugu.
Chalamila alisema katika mkoa wake (Dar) wamejipanga kwa kusimamia amani na utulivu katika kipindi chote cha kuelekea uchaguzi.
 
1743449601548.jpg
 
Wakati maandalizi ya Tamasha la Kuombea Uchaguzi Mkuu 2025 yakipamba moto wake, hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan nayo imekazia amani na utulivu kipindi cha uchaguzi.
Akihutubia kwenye Baraza la Eid El Fitr kwenye Ukumbi wa Julius Nyerere jijini Dar, Rais Samia amewataka viongozi wa dini kuomba amani kuelekea Uchaguzi Mkuu na kukemea viongozi wenye matamko yenye kushiria vurugu.
Hotuba ya Rais imekwenda sambamba na wazo la Mkurugenzi wa Msama Promotion, Alex Msama kuandaa tamasha la kuombea Uchaguzi Mkuu mwaka huu.
Kwa mujibu wa Msama, lengo la tamasha hilo litakalofanyika Mei, 2025 ni kumlilia Mungu ili taifa la Tanzania lipite salama kwenye kipindi hiki kuelekea uchaguzi mkuu na siku yenyewe hadi kuapishwa rais ajaye.
Mbali na Rais Samia kusisitiza hayo kwa viongozi wa dini, pia alisema licha ya kuwepo kwa vyombo vya ulinzi kusimamia wajibu wao lakini viongozi wa dini waendelee kuhubiri amani ya nchi.
Aidha, akizungumza katika Baraza hilo, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert John Chalamila naye aliwahakikishia wananchi wa Dar es Salaam na nchi nzima (kwa niaba ya wakuu wa mikoa wenzake) nchi ipo salama, ina amani hivyo, wafanyabiashara wakubwa hawana sababu ya kuondoa pesa zao benki wakiamini kutakuwa na vurugu.
Chalamila alisema katika mkoa wake (Dar) wamejipanga kwa kusimamia amani na utulivu katika kipindi chote cha kuelekea uchaguzi.

Ndugu zetu mnamuomba Mungu gani ? Maana kwa wengine tunajua huwezi kumuomba Mungu kwenda kuiba au kudanganya. Sasa utaombeaji uchaguzi ambao ni wa kura za Polisi, usalama, fututa wagomeaji. Halafu Mungu akiwachukuwa wanaofanya uamuzi tutawaita Mahayati. Nawapa Tahadhari mkiendelee na Chaguzi za wizi kama 2019, 2020 na 2024 kama wakati wa Magu badi natoa ahadi hapa yaliyo mtokea Magu na wengine wakati ule wa 2020 yatatokea tena. Kama mnawapenda kweli hao viongozi washaurini watende haki. Mungu akiamua kitu msikofuata msilaumu. wekeni huu ujumbe kabisa tutaona kama nipo sawa au la
 
Hakuna haja ya Tamasha la kuombea UCHAFUZI, kinachotakiwa ni Tamasha la kumwambia Samia kuwa enough is enough tunataka Tume HURU ya UCHAGUZI.

Au hata Wananchi waende wamevaa tusheti za NO REFORMS NO ELECTION au LINDA DEMOKRASIA
 
Back
Top Bottom