1. Subaru forester, 2005
2. Hapa dsm ila pia rough road
3. Mara kwa mara hapa dsm ila inaenda shambani.
4. Ndiyo gari ya mishe mishe pia ndio ya safari ya familia
5. Kiukweli nikiwa na mizigo ili mradi inaingia huwa naitumia hii hii. Na kwa kweli buti yake ni kubwa.
6. Hapana sijawahi kuitumia kuvuta trela
Kuna mdau keshakujibu hapa.
https://www.jamiiforums.com/showthread.php?p=14200139
Kama unataka tairi pana kwa ajili ya show nzuri na stability barabarani recomended size ni 225/60/R16
Au 225/55/R16 ila hii inashusha gari kidogo kama unatumia rough road itakupa shida kidogo.
Pia size 235/50/R17 ni tairi pana kidogo recomended na Subaru wenyewe.
Zingatia ukitumia tairi ya size 225 au 235 lazima rim yako iwe size 7.5J.
Kwa kuwa Forester ni gari yenye nguvu (torque) unatakiwa kununua brand nzuri kwa dealer kama vile Kumho, Good year, Michelin, Pirreli. Etc.
Achana na mchina wa bei nafuu utakula hasara ndani ya miezi 6.