Taifa Stars na Bafana Bafana ya kichina

Mphamvu

JF-Expert Member
Jan 28, 2011
10,702
3,288
Leo timu yetu ya soka imecheza na Afrika Kusini, mechi ambayo imeisha kwa sisi kufungwa goli 1-0. Ingawa sikutazama mechi kuna mambo kadhaa yananikanganya, Bafana Bafana imecheza mechi ya leo bila nyota wake 11, Siphiwe Tshabalala, Reneilwe Letsholonyane, Steven Pienaar, Tsepo Masilela na Bongani Khumalo wakiwemo. Mechi hii haikuwa katika ratiba za FIFA na TFF wanajua fika ugumu wa kuratibu mechi hizi.

Ndiyo, Kaizer Chiefs, Preston North End, Ajax Cape Town, Tottenham Hotspurs, Rubin Kazan na timu nyinginezo zenye wachezaji wa Bafana Bafana zisingeweza kuruhusu wachezaji wao kurudi hasa wakati huu ambapo ligi nyingi duniani zinaelekea ukingoni, tena kuja kucheza mechi ambazo hazitambuliwi na FIFA. Tatizo langu si kutotambuliwa kwa mechi, tatizo ni kucheza na timu moja chini ya mwavuli wa nyingine. Wote tunaijua Bafana iliyoichachafya Mexico pale Soccer City na baadae kuifunga Ufaransa pale Royal Bafokeng, kama vile haitoshi majuzi ikafunga Misri kwenye michuano ya kufuzu AFCON 2012.

Je, timu iliyocheza michezo hii ndiyo tuliocheza nayo leo? Endapo tungeshinda mechi ya leo, mbwembwe za magazeti zingekuwa nyingi hapo kesho, ingawa ukweli ni kuwa hatujacheza na Bafana Bafana halisi. Kwao, mechi hii ina faida kwa kuwa wameitumia kujaribu kikosi chao cha pili, ila sisi tumejidanganya kwa kudhani kuwa tumecheza na Afrika Kusini, kumbe tumecheza na kikosi cha pili. Kama ni kucheza na timu za kiwango cha kati, tungeomba hata Rwanda au Kenya, na kama tunataka timu za kiwango cha juu, basi tucheze na timu halisi.

Naomba kuwasilisha!
 
Jana baada ya mechi niliweka uzi wenye utafiti, ukihoji uhalali wa Taifa Stars kucheza na Afrika Kusini iliyokuwa bila nyota wake 11. Mods wakaiunganisha kwenye updates za matokeo, nikaweka tena uzi kwenye jukwaa la ulalamishi, hiyo ndo ikafutwa kabisaa! Najua mnatingwa, ila ni vema kujua kutofautisha maudhui kati ya uzi na uzi. Naombeni uzi wangu urudi kwa ajili ya mjadala na wadau watoe maoni yao, natumia mobile hivyo siwezi kukopi na kupesti nitengeneze mwingine... Tutendeane haki!
 
Inauma mkuu, uzi haujachangiwa siku ya pili sasa... Kisa wameuchanganya!

Mi naanza kuchangia hivi:

Kwa kiwango gani tulichonacho hadi bafana walete nyota wao 11 kama timu B yao tu inatuchakaza? Unadhani wangekua wanaenda kucheza na black stars ama timu nyingine kali wangeleta yale mafotokopi yao?

Suluhisho: tukuze kiwango chetu, kikipanda tutaombwa friendly matches na timu bora
 
Mi naanza kuchangia hivi:

Kwa kiwango gani tulichonacho hadi bafana walete nyota wao 11 kama timu B yao tu inatuchakaza? Unadhani wangekua wanaenda kucheza na black stars ama timu nyingine kali wangeleta yale mafotokopi yao?

Suluhisho: tukuze kiwango chetu, kikipanda tutaombwa friendly matches na timu bora

Hapana kaka, kosa lilikuwa la kwetu kuomba gemu ambayo FIFA hawaitambui, klabu zikagoma kuruhusu wachezaji wao, matokeo yake tukacheza na Bafana ya maboksi, mbona Brasil walileta kikosi full pamoja na ubovu wetu, Kodivaa pia walicheza wakiwa kamili, pia usisahau mechi yetu na Misri kule Aswan!
 
Mi naanza kuchangia hivi:

Kwa kiwango gani tulichonacho hadi bafana walete nyota wao 11 kama timu B yao tu inatuchakaza? Unadhani wangekua wanaenda kucheza na black stars ama timu nyingine kali wangeleta yale mafotokopi yao?

Suluhisho: tukuze kiwango chetu, kikipanda tutaombwa friendly matches na timu bora

Haikuwa vibaya kuomba mechi ile, ila matatizo yetu ni yalyale miaka nenda rudi, kushindwa kujumuisha wale vijana wa timu za chini hata katika mechi ambazo tunajua kuwa wenzetu watachezesha kikosi cha tatu!.

Nadhani tulitaka kushinda ili tujisifu sana, kuwa tumecheza soka ya hali ya juu, Mrope ni noma, Bafanabafana yapata kiboko yake n.k.

Tuendelee na mwendo huu wa kutaka kutengeneza Headlines, tuone mwisho wake, haikuwa vibaya hata kidogo kama tungechukua wachezaji 6 katika kikosi cha olimpiki kinachosubiri kucheza na Nigeria hata kama wangekuwa chini ya Jan.
 
Nimekuelewa N'gombe, lakini nadhani lengo la kucheza na Bafana ni kujaribu uwezo wetu na timu za kiwango chake. Ili kama tukiwafunga Misri, Kodivaa na Cameroon, kisha tukaenda suluhu na Algeria, Nigeria na Angola, na pengine Morroco wakatufunga kwa taabu, tuseme kuwa kiwango chetu kimepanda. Je, kama timu zote zitaleta kikosi cha tatu kwenye mechi za kirafiki, tukipangwa na timu hizo kwenye mashindano si kimeo?
 
Nimekuelewa N'gombe, lakini nadhani lengo la kucheza na Bafana ni kujaribu uwezo wetu na timu za kiwango chake. Ili kama tukiwafunga Misri, Kodivaa na Cameroon, kisha tukaenda suluhu na Algeria, Nigeria na Angola, na pengine Morroco wakatufunga kwa taabu, tuseme kuwa kiwango chetu kimepanda. Je, kama timu zote zitaleta kikosi cha tatu kwenye mechi za kirafiki, tukipangwa na timu hizo kwenye mashindano si kimeo?
Kucheza na kikosi cha tatu kama ilivyokuwa mechi iliyopita, si vibaya kwa mazoezi, ila kwa maandalizi ya mechi za kimashindano naona haikai sawa kwa vile haituandai kiushindani, na pia unakuta hata wachezaji wetu ambao wengi huwa wanapenda kukamia wachezaji wenye majina makubwa kimtindo wanakuwa kama wameidharau mechi,wakati kiukweli wanapaswa kutambua kuwa hakuna mechi ndogo, so ukiwajumuisha na yoso kidogo na wao(wakongwe) itabidi waendane na spidi ya mchezo.
 
Kucheza na kikosi cha tatu kama ilivyokuwa mechi iliyopita, si vibaya kwa mazoezi, ila kwa maandalizi ya mechi za kimashindano naona haikai sawa kwa vile haituandai kiushindani, na pia unakuta hata wachezaji wetu ambao wengi huwa wanapenda kukamia wachezaji wenye majina makubwa kimtindo wanakuwa kama wameidharau mechi,wakati kiukweli wanapaswa kutambua kuwa hakuna mechi ndogo, so ukiwajumuisha na yoso kidogo na wao(wakongwe) itabidi waendane na spidi ya mchezo.

Naungana na wewe kwa asilimia zote, ile mechi kidhima ina manufaaa kwao kwa vile wanajaribu plan B zao. Kama ni mazoezi ya kawaida, tungeomba na timu kama Kenya, Rwanda, Uganda n.k ambazo ni bora maradufu ya kikosi B cha Afrika Kusini na timu hizo zingetuheshimu kwa kuleta vikosi vya kwanza.
 
Haikuwa vibaya kuomba mechi ile, ila matatizo yetu ni yalyale miaka nenda rudi, kushindwa kujumuisha wale vijana wa timu za chini hata katika mechi ambazo tunajua kuwa wenzetu watachezesha kikosi cha tatu!.

Nadhani tulitaka kushinda ili tujisifu sana, kuwa tumecheza soka ya hali ya juu, Mrope ni noma, Bafanabafana yapata kiboko yake n.k.

Tuendelee na mwendo huu wa kutaka kutengeneza Headlines, tuone mwisho wake, haikuwa vibaya hata kidogo kama tungechukua wachezaji 6 katika kikosi cha olimpiki kinachosubiri kucheza na Nigeria hata kama wangekuwa chini ya Jan.

Nakubaliana nawe mkuu. Tunaomba mechi si kwa lengo la kukuza na kuimarisha kiwango cha timu bali kwa kutafuna upenyo wa kufanyia propaganda (ikiwa tutabahatisha matokeo mazuri katika mechi husika)
 
Hapana kaka, kosa lilikuwa la kwetu kuomba gemu ambayo FIFA hawaitambui, klabu zikagoma kuruhusu wachezaji wao, matokeo yake tukacheza na Bafana ya maboksi, mbona Brasil walileta kikosi full pamoja na ubovu wetu, Kodivaa pia walicheza wakiwa kamili, pia usisahau mechi yetu na Misri kule Aswan!

Duh, kaaaazi kweli kweli! Kumbe haikua katika ratiba! Ni bora basi mechi ile isingekuwapo kabisa. Na Nakuunga mkono hoja yako, Mara mia tungecheza na uganda ama kenya iliyokamilika kuliko kucheza na south africa B. Kwa mtaji ule wao south africa ndio waliofadika zaidi na mchezo ule
 
Nakubaliana nawe mkuu. Tunaomba mechi si kwa lengo la kukuza na kuimarisha kiwango cha timu bali kwa kutafuna upenyo wa kufanyia propaganda (ikiwa tutabahatisha matokeo mazuri katika mechi husika)

Uko sahihi kaka. Siasa za kuchumia tumbo zimekuwa nyingi pale TFF, wanaleta timu kubwa ili wapange viingilio vikubwa, wanajua wakileta Uganda pesa ya mlango haitakuwa kubwa hata kama game ina manufaa kwetu. Hakuna hata siku moja Kaijage alifanya press conference akasema mikakati ya ushindi, always viingilio, viingilio!
 
Duh, kaaaazi kweli kweli! Kumbe haikua katika ratiba! Ni bora basi mechi ile isingekuwapo kabisa. Na Nakuunga mkono hoja yako, Mara mia tungecheza na uganda ama kenya iliyokamilika kuliko kucheza na south africa B. Kwa mtaji ule wao south africa ndio waliofadika zaidi na mchezo ule

Ndio, game haikuwa kwenye ratiba za mechi za kirafiki za kimataifa. Sheria ya FIFA ni kuwa kama gemu wanaitambua, timu ya taifa ina haki ya kumchukua mchezaji wao wakati wowote hata kama wana mechi na Mbinguni FC, kama ni kinyume chake, hawakupi mchezaji, na kashtaki popote!
 
Back
Top Bottom