Mphamvu
JF-Expert Member
- Jan 28, 2011
- 10,702
- 3,288
Leo timu yetu ya soka imecheza na Afrika Kusini, mechi ambayo imeisha kwa sisi kufungwa goli 1-0. Ingawa sikutazama mechi kuna mambo kadhaa yananikanganya, Bafana Bafana imecheza mechi ya leo bila nyota wake 11, Siphiwe Tshabalala, Reneilwe Letsholonyane, Steven Pienaar, Tsepo Masilela na Bongani Khumalo wakiwemo. Mechi hii haikuwa katika ratiba za FIFA na TFF wanajua fika ugumu wa kuratibu mechi hizi.
Ndiyo, Kaizer Chiefs, Preston North End, Ajax Cape Town, Tottenham Hotspurs, Rubin Kazan na timu nyinginezo zenye wachezaji wa Bafana Bafana zisingeweza kuruhusu wachezaji wao kurudi hasa wakati huu ambapo ligi nyingi duniani zinaelekea ukingoni, tena kuja kucheza mechi ambazo hazitambuliwi na FIFA. Tatizo langu si kutotambuliwa kwa mechi, tatizo ni kucheza na timu moja chini ya mwavuli wa nyingine. Wote tunaijua Bafana iliyoichachafya Mexico pale Soccer City na baadae kuifunga Ufaransa pale Royal Bafokeng, kama vile haitoshi majuzi ikafunga Misri kwenye michuano ya kufuzu AFCON 2012.
Je, timu iliyocheza michezo hii ndiyo tuliocheza nayo leo? Endapo tungeshinda mechi ya leo, mbwembwe za magazeti zingekuwa nyingi hapo kesho, ingawa ukweli ni kuwa hatujacheza na Bafana Bafana halisi. Kwao, mechi hii ina faida kwa kuwa wameitumia kujaribu kikosi chao cha pili, ila sisi tumejidanganya kwa kudhani kuwa tumecheza na Afrika Kusini, kumbe tumecheza na kikosi cha pili. Kama ni kucheza na timu za kiwango cha kati, tungeomba hata Rwanda au Kenya, na kama tunataka timu za kiwango cha juu, basi tucheze na timu halisi.
Naomba kuwasilisha!
Ndiyo, Kaizer Chiefs, Preston North End, Ajax Cape Town, Tottenham Hotspurs, Rubin Kazan na timu nyinginezo zenye wachezaji wa Bafana Bafana zisingeweza kuruhusu wachezaji wao kurudi hasa wakati huu ambapo ligi nyingi duniani zinaelekea ukingoni, tena kuja kucheza mechi ambazo hazitambuliwi na FIFA. Tatizo langu si kutotambuliwa kwa mechi, tatizo ni kucheza na timu moja chini ya mwavuli wa nyingine. Wote tunaijua Bafana iliyoichachafya Mexico pale Soccer City na baadae kuifunga Ufaransa pale Royal Bafokeng, kama vile haitoshi majuzi ikafunga Misri kwenye michuano ya kufuzu AFCON 2012.
Je, timu iliyocheza michezo hii ndiyo tuliocheza nayo leo? Endapo tungeshinda mechi ya leo, mbwembwe za magazeti zingekuwa nyingi hapo kesho, ingawa ukweli ni kuwa hatujacheza na Bafana Bafana halisi. Kwao, mechi hii ina faida kwa kuwa wameitumia kujaribu kikosi chao cha pili, ila sisi tumejidanganya kwa kudhani kuwa tumecheza na Afrika Kusini, kumbe tumecheza na kikosi cha pili. Kama ni kucheza na timu za kiwango cha kati, tungeomba hata Rwanda au Kenya, na kama tunataka timu za kiwango cha juu, basi tucheze na timu halisi.
Naomba kuwasilisha!