Taifa linahitaji damu changa - Sitta

Taifa linahitaji damu changa - Sitta

ukitaka kuumaliza upinzani kwanza unaanza na kauli kama za akina sitta
 
Hivi Sitta ameshindikana kabisa kabisa kufukuzwa CCM? naona kama lugha yake inatofautiana sana na ya chama chake. Kuna mzee mmoja anaheshimika anasema hivi wewe kijana hujui kuwa sitta ni wa kwetu chadema ila yupo CCM kwa muda tu?
 
sasa naanza kuamini kweli JK sio dikteta? maneno mengine yanachoma moyo lakini kamwacha kila mtu atoe dukuduku lake bwana sitta ni namba moja kamwacha anatema cheche kila kukicha.
 
Familia yake pamoja na familia ya mwanae wametoa jumla ya sh. 2mil. Lema ametoa sh mil 1.

BORA KUTOA SHILLING 2M halali kuliko kutoa 10M hulizopata kwa uharifu(Ufisadi)
 
Hivi Sitta ameshindikana kabisa kabisa kufukuzwa CCM? naona kama lugha yake inatofautiana sana na ya chama chake. Kuna mzee mmoja anaheshimika anasema hivi wewe kijana hujui kuwa sitta ni wa kwetu chadema ila yupo CCM kwa muda tu?

Umetumwa?
 
mzee mwenzangu sitta hama chama kama CCM hapakutoshi? utanung'unika hadi lini?

ni maoni yangu tu mimi mzee busara
 
Mbona siku hizi watu wanakimbialia makanisani kuchangisha michango? Mzee six na Lema? Naanza kuona kama maono nikiwa kwenye lindi la usingizi nahisi kitu au ni maluwe luwe ama ni upofu? Hakuna kitu hapa kweli?

Kunya anye Kuku akinya bata kaharisha, ingekuwa ni EL ungesikia jinsi watu wanavyoachia mashuzi!
 
nasikia sitta ni wa sita kwa ubora Tanzania!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
YESU "NYUMBA YA BABA YANGU MMEIFANYA PANGO LA WALANGUZI"KUMBE HATA WAKATI ULE MAFISADI WALIFANYA HIVYO KANISANI!Yalaaah
 
Hivi Sitta ameshindikana kabisa kabisa kufukuzwa CCM? naona kama lugha yake inatofautiana sana na ya chama chake. Kuna mzee mmoja anaheshimika anasema hivi wewe kijana hujui kuwa sitta ni wa kwetu chadema ila yupo CCM kwa muda tu?

Sitta haamini kabisa katika sera za CDM. Mwaka jana wakati Slaa ananadi sera ya elimu bure hadi A Level, Sitta ndiye alikuwa mpinzani mkubwa wa sera hiyo kuliko hata Kikwete aliyekuwa mgombea urais. Slaa aliwahi pia kuhoji posho wanazolipwa wabunge, Sitta akamuita Slaa majina ya ajabu. Hata alipoona kuna hatari ya kutemwa na CCM aliamua kuanzisha CCJ kwani nanajua CDM hana nafasi. Huyu ni mnafiki aliyekubuhu.
 
Kunya anye Kuku akinya bata kaharisha, ingekuwa ni EL ungesikia jinsi watu wanavyoachia mashuzi!

Hivi lowassa ana mkosi gani mbona alitoa point kama ya sitta ya vijana ni bomu linalosubiri kupasuka lakni JF walimshambulia kama vile hajatoa point. Jf tunaangalia nguvu ya hoja au tunaangalia hoja imetolewa na nani?
 
YESU "NYUMBA YA BABA YANGU MMEIFANYA PANGO LA WALANGUZI"KUMBE HATA WAKATI ULE MAFISADI WALIFANYA HIVYO KANISANI!Yalaaah

hakika umenena nyumba za ibada zimeanza kuwa nyumba za walanguzi.
 
Hayo aliyoyasema Sitta kwa mtazamo wangu ni kauli ambayo inahitaji sapoti kubwa kutoka kwa vijana. Wazee wanatakiwa kupumzika na kuachia damu changa ya vijana ili kushika hatamu za uongozi. Haya mazoea ya wazee kuwa serikalini tena kwenye uongozi wa kisiasa ni kuwanyima vijana fursa na kulirudisha taifa nyuma kwa kuendeleza fikra zilezile , za miaka ileile! Ndio maana nakubaliana na Sitta kwa asilimia zote. Hata kama hamaanishi kutoka moyoni, atleast anatambua hilo na meseji imefika, kazi kwetu vijana!
 
Tofauti kati ya kauli ya Lowassa na ile ya Sitta ni kwamba Lowassa alikuwa anawachochea vijana ili walete machafuko kwa kisingizio cha kukosekana kwa ajira wakati anapaswa kuelewa kwamba suala la ajira, ambalo limechangiwa pakubwa na mdodoro wa kiuchumi linahitaji suluhisho pana zaidi. Lakini pia ameshindwa kueleza kwamba yeye analichangia kutokana na wizi wa rasilimali zetu.

Kwa upande wake Sitta anachosema ni kwamba vijana wa nchi hii wamekomaa vya kutosha kiasi cha kuaminiwa na kupewa dhamana ya uongozi wa nchi. Sasa hapa kuna ugumu gani wa kuelewa kwamba kauli hizi mbili zina-reflect misimamo ya wazungumzaji katika mustakabali wa nchi. Kuna mmoja anayeamini katika nguvu ya vijana kurithishwa uongozi na mwingine anayeamini katika kuwatumia vijana kupanda ngazi za kiutawala bila kujali mustakabali wa nchi au kile kitakachowatokea vijana wanaochochewa kufanya vurugu na uasi. Mfano ulio dhahiri ni ule wa UVCCM waliokusanywa wafanye vurugu na uharibu Dodoma!
 
Jamani jamani viongozi wa makanisa naomba muwe makini na hawa wanasiasa otherwise watatuharibia makanisa yetu kwa kujisafisha kwao kila tukiwaita
 
Kama anaona Taifa linahijati vijana si ajivue gamba apumzike awaachie vijana.

Acha unafki Mzee 6
 
Back
Top Bottom