Victor Mlaki
JF-Expert Member
- May 1, 2016
- 3,542
- 3,451
Nimekuwa nikijiuliza maswali mengi sana licha ya kuwa sehemu ya waajiriwa ambao tumekuzwa na mfumo wa hatari sana uliotuandaa kujenga imani ya kusoma kwa bidii ili kupata ajira nzuri badala ya kusoma kwa bidii ili kuzalisha ajira nzuri.
Nakiri kwa dhati kabisa kuwa mfumo huu umeua ubunifu kwa kiasi kikubwa na kukuza uvuvu, ulalamishi,upotezaji muda na uwajibikaji duni kwa wengi. Siyo jambo la ajabu mtu kuwa elimu ngazi ya digirii moja au mbili na bado akawa anasubiri ajira.
Mfumo wetu wa elimu umetujenga zaidi kuamini hata kama hatuwajibiki. Haishangazi kusikia mtu akisema soma kwa bidii ili uje uajiriwe sehemu nzuri na upate mshahara mzuri. Thamani ya mshahara leo imepewa ukubwa kuliko thamani ya elimu kwa sababu tunashindwa kutambua kusudi la elimu hasa ni lipi na je tunaandaliwa kuwa watu gani ukiachilia mbali kule kuamini tu kuwa ulisoma kwa bidii na kufauli vizuri utaajiriwa na upata mshahara mzuri.
Ni kawaida kabisa leo kusoma siyo kwa lengo la uelimika ila kwa lengo la kuajiriwa tu. Hali hii ni kiashiria cha hatari kubwa kwa Taifa lolote lile.
Nakiri kwa dhati kabisa kuwa mfumo huu umeua ubunifu kwa kiasi kikubwa na kukuza uvuvu, ulalamishi,upotezaji muda na uwajibikaji duni kwa wengi. Siyo jambo la ajabu mtu kuwa elimu ngazi ya digirii moja au mbili na bado akawa anasubiri ajira.
Mfumo wetu wa elimu umetujenga zaidi kuamini hata kama hatuwajibiki. Haishangazi kusikia mtu akisema soma kwa bidii ili uje uajiriwe sehemu nzuri na upate mshahara mzuri. Thamani ya mshahara leo imepewa ukubwa kuliko thamani ya elimu kwa sababu tunashindwa kutambua kusudi la elimu hasa ni lipi na je tunaandaliwa kuwa watu gani ukiachilia mbali kule kuamini tu kuwa ulisoma kwa bidii na kufauli vizuri utaajiriwa na upata mshahara mzuri.
Ni kawaida kabisa leo kusoma siyo kwa lengo la uelimika ila kwa lengo la kuajiriwa tu. Hali hii ni kiashiria cha hatari kubwa kwa Taifa lolote lile.