TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI:
TAHLISO kama shirikisho lina kanusha taarifa hiyo,na kulaani vikali matumizi mabaya ya kutumia jina la shirikisho kwa manufaa binafsi,aidha anaejiita mwenyekiti wa Tahliso katika taarifa hiyo Musa Mdede si MWENYEKITI HALALI kwa sababu vikao halali vya vya shirikisho vilivyofanyika tarehe 03 hadi 04 /05/2014 katika Chuo cha Kodi vilimwondoa madarakani,na kwa mujibu wa katiba ya shirikisho nafasi yake ilikaimiwa na makamu mwenyekiti wa Tahliso,hivo taarifa aliyoitoa sio sahihi ni ya upotoshaji kwa wanafunzi wa vyuo vikuu Tanzania.
Aidha,uongozi wa Tahliso ulipata taarifa za ucheleweshaji wa malipo ya fedha za mafunzo ya vitendo kwa baadhi ya vyuo na kuweza kulifatilia swala hilo ili kuhakikisha fedha hizo zinapatikana kwa wakati,katika majukumu yake uongozi uliwasiliana na Mkurugenzi wa Bodi ya Mikopo ya wanafunzi wa Elimu ya Juu Tanzania - HESLB ili kupata hatima ya malipo kwa vyuo ambavyo havijapata fedha hizo,hususani Chuo kikuu cha Mtakatifu Augustino (saut) Mwanza na Tabora,Chuo cha usimamizi wa Fedha (IFM), Chuo kikuu cha Teofilo Kisanji-Mbeya,Chuo kikuu cha Tumain Makumira-Iringa, Chuo kikuu Kishiriki cha Kumbukumbu ya Stephano Moshi (SMUCCO) na Chuo Kikuu cha Jordan Morogoro.
Hata hivyo Bodi ya Mikopo imeendelea kuchukua hatua za haraka katika kuhakikisha vyuo husika vinapata fedha hizo haraka iwezekanavyo nakuweza kuzitoa kwa wanafunzi ambao wanaendelea na mafunzo yao ya vitendo katika maeneo mbalimbali,na leo hii Chuo kikuu Kishiriki cha Kumbukumbu ya Stephano Moshi (SMUCCO) na Chuo Kikuu cha Jordan Morogoro vitapatiwa fedha zote zinazohitajika,taratibu za kifedha zinaendelea kufanyika ili vyuo vilivyobakia viweze kupata fedha hizo kwa siku ya kesho.
Uongozi wa Tahliso unawaomba wanafunzi wote wav you vikuu ambao hawajapata fedha hizo kuwa watulivu wakati wakisubili kupata fedha zao,na hatua kadha wa kadha zinaendelea kuchukuliwa katika kuhakikisha wanafunzi wote stahiki wanapatiwa fedha zao kwa wakati.
Imetolewana :
ABDI MAHMOUD ABDI
MAKAMU MWENYEKITI TAHLISO.
14/08/2014