TAHLISO ni vibaraka wa CCM-Wasomi

TAHLISO ni vibaraka wa CCM-Wasomi

Molemo

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
14,620
Reaction score
13,361
Wasomi mbalimbali katika vyuo vikuu vya mkoa wa Morogoro wamelaani vikali tamko lililotolewa na Mkiti wa Jumuiya ya vyuo vikuu vya elimu ya juu nchini Amon Chakushemeire kwamba CHADEMA kinachochea migogoro kwenye vyuo vikuu nchini.

Wakizungumza kwa hasira wanafunzi kadhaa na viongozi wa wanafunzi walisema hawakuwahi kushirikishwa katika tamko hilo walilodai ni la kipuuzi kuwahi kutolewa na kiongozi wa TAHLISO.

Tayari tamko hilo la Mkiti wa TAHLISO limewagawa wanafunzi kote chini katika makundi mawili.Lile kundi kubwa la wafuasi wa Chadema na lile dogo la wafuasi wa CCM.Tamko hilo lililotolewa dhahiri lilikuwa likikishambulia Chadema bila kueleza uhalisia wa vurugu katika vyuo vikuu.

Wanafunzi hao wamemtaka Mkiti huyo wa TAHLISO kufuta mara moja tamko lake na kuliomba radhi Taifa kwa kusema uwongo.

Source:Tanzania Daima Jumapili.
 
Tahliso hakuanza leo kuwa kibaraka wa ccm.
Dr godbless unaweza kuelezea zaidi
 
Last edited by a moderator:
Uongo upi?
Kwani si kweli Chadema ndio chanzo cha Migogoro na uchochezi kwenye Vyuo Vikuu??

Me naona Mwenyekiti wa Tahliso yupo sahihi na Tamko lake!
 
hawa vijana wachache wanapewa hela wanaacha uzalendo na wanasahau future na backgroung za zao na za watanzania wengine. wajue usomi ni kuexpress uzalendo na siyo kuwa mfalme kwa wasio na elimu hiyo ni laana.
 
Tamko!! Sorry,wameeleza ki'ushahidi idadi ya vurugu na namna CHADEMA ilivyohusika?? Vipi kuhusu vurugu za wanafunzi wa IFM zilizotokana madai yao kubakwa na kuporwa mwishoe wakaishia kupigwa mabomu na askari (NI CHADEMA)? Vipi kuhusu fujo zilizotaka kujitokeza Mzumbe Mwaka 2009 baada ya wanafunzi kucheleweshewa mikopo (NI CHADEMA)? Vipi kuhusu ile tafrani pale Bodi ya mikopo kiasi cha FFU kusambaratisha watu (NI CHADEMA)? Na tafrani ya kifo cha mwanafunzi chuo cha uhasibu Arusha je,(NI CHADEMA)? Yale maandamano ya wana UDSM kuelekea ofis ya waziri mkuu kupeleka malalamiko ya kiutawala na suala la mikopo je,(NI CHADEMA)? Acheni SIASA katika masuala ya msingi. Chanzo cha vurugu katika vyuo vingi kipo wazi 1. UWEPO WA UTAWALA MBOVU NGAZI YA CHUO KATIKA KUSHUGHULIKIA MATATIZO YA WANAFUNZI KWA WAKATI 2. MFUMO MBOVU WA UPATIKANAJI HAKI YA MKOPO (ucheleweshaji wa mikopo,asilimia isiyoendana na sifa za mhusika etc) 3. UKOSEFU WA USALAMA WA MALI ZA WANAFUNZI NA HATA UHAI WAO (Take a case of SAUT mwanza,wanafunzi wanavamiwa hadi hosteli kuporwa,take a case of IFM,take a case of UDSM haswa pale darajani,take a case arusha juzi hapa). Msipotoshe watu na TAMKO lenu. Mmeshindwa kutekeleza majukumu yenu,mmehamia kwenye siasa za kutumika.
 
Tamko!! Sorry,wameeleza ki'ushahidi idadi ya vurugu na namna CHADEMA ilivyohusika?? Vipi kuhusu vurugu za wanafunzi wa IFM zilizotokana madai yao kubakwa na kuporwa mwishoe wakaishia kupigwa mabomu na askari (NI CHADEMA)? Vipi kuhusu fujo zilizotaka kujitokeza Mzumbe Mwaka 2009 baada ya wanafunzi kucheleweshewa mikopo (NI CHADEMA)? Vipi kuhusu ile tafrani pale Bodi ya mikopo kiasi cha FFU kusambaratisha watu (NI CHADEMA)? Na tafrani ya kifo cha mwanafunzi chuo cha uhasibu Arusha je,(NI CHADEMA)? Yale maandamano ya wana UDSM kuelekea ofis ya waziri mkuu kupeleka malalamiko ya kiutawala na suala la mikopo je,(NI CHADEMA)? Acheni SIASA katika masuala ya msingi. Chanzo cha vurugu katika vyuo vingi kipo wazi 1. UWEPO WA UTAWALA MBOVU NGAZI YA CHUO KATIKA KUSHUGHULIKIA MATATIZO YA WANAFUNZI KWA WAKATI 2. MFUMO MBOVU WA UPATIKANAJI HAKI YA MKOPO (ucheleweshaji wa mikopo,asilimia isiyoendana na sifa za mhusika etc) 3. UKOSEFU WA USALAMA WA MALI ZA WANAFUNZI NA HATA UHAI WAO (Take a case of SAUT mwanza,wanafunzi wanavamiwa hadi hosteli kuporwa,take a case of IFM,take a case of UDSM haswa pale darajani,take a case arusha juzi hapa). Msipotoshe watu na TAMKO lenu. Mmeshindwa kutekeleza majukumu yenu,mmehamia kwenye siasa za kutumika.

Mkuu Chadema wachochezi sana.. Hata mwaka 1994 (nisahihishwe kama nimekosea) walichochea mpaka raisi wa wakati huo Mwinyi akakifunga chuo kikuu cha mlimani.. Yaani wakamchora mpaka ambassador "sidiria"..

Ha ha ha.. Ama kweli ccm wameshikwa kubaya..
 
TAHILISO lmekuwa genge la mafisadi wa ccm,hivyo sisi wanafunzi hatunashida nayo tena tunasubiri 2016 tuwe na tahiliso yenye kutetea maslahi ya wanafunzi CHADEMA ikiingia madarakani.Ukweli ni kwamba hatuitaki ccm tena.
 
Kwani nani asie fahamu kuwa CHADEMA ndio chanzo cha vurugu nchini?

Haya mambo yakutaka kuukataa ukweli utawapa wana-CHADEMA presha ya bure kabisa!

Cha msingi sio kuubishia ukweli, ni nyinyi wenyewe kujifanyia tathmini na kufikia maamuzi ya kubadili mwenendo wenu wa ufanyaji siasa, mbona simple tu.
 
hawa vijana wachache wanapewa hela wanaacha uzalendo na wanasahau future na backgroung za zao na za watanzania wengine. wajue usomi ni kuexpress uzalendo na siyo kuwa mfalme kwa wasio na elimu hiyo ni laana.
ulilo sema ni kweli lakini mwisho haki itasinda. kila mjinga hufa na ujinga wake na kuzikwa na waoga wenzake. kama angekuwa hatumiki angethibitisha hilo kwa kutoa ushahidi wa hilo analo lisema. KIBARAKA MKUBWA HUYO NA ASHINDWE NA KULEGEA KABISA. KILAZA MKUBWA HUYO.
 
tahliso hawakuanza leo wao vibaraka wakubwa sana kwa sisi tujuavyo haitupi shida ni njaa tu hawajui wasemalo.
 
Mkuu Chadema wachochezi sana.. Hata mwaka 1994 (nisahihishwe kama nimekosea) walichochea mpaka raisi wa wakati huo Mwinyi akakifunga chuo kikuu cha mlimani.. Yaani wakamchora mpaka ambassador "sidiria"..

Ha ha ha.. Ama kweli ccm wameshikwa kubaya..

Duh!
Kweli tumetika mbali, yani kumchora kiongozi chuo kizima kinafungwa!
 
tahliso hawakuanza leo wao vibaraka wakubwa sana kwa sisi tujuavyo haitupi shida ni njaa tu hawajui wasemalo.

afadhali umesema mkuu tahliso ni ccm original kumbuka uchaguzi wa 2010 wanafunzi wa walinyinmwa haki ya kupiga kura tahliso ikakaa kimya
 
Kwani nani asie fahamu kuwa CHADEMA ndio chanzo cha vurugu nchini?

Haya mambo yakutaka kuukataa ukweli utawapa wana-CHADEMA presha ya bure kabisa!

Cha msingi sio kuubishia ukweli, ni nyinyi wenyewe kujifanyia tathmini na kufikia maamuzi ya kubadili mwenendo wenu wa ufanyaji siasa, mbona simple tu.
Kweli ccm mmefilisika kimawazo, hivi mgogoro wa LOLIONDO ni CHADEMA?,gesi MTWARA ni CHADEMA? na UVCCM LUMUMBA kutwangana makonde nayo ni CHADEMA?. Shame on you maccm.
 
MLENGWA WA MLIPUKO ALIKUWA BALOZI WA VATICAN?

(Naona mods wana watu wao wenye haki ya kuanzisha threads, sisi wengine haturuhusiwi)

Ndugu WanaJamvi;

Kwa muda sasa kumekuwa na hoja mbali mbali juu ya uhalali wa uwepo wa Ubalozi wa Vatican hapa Tanzania. Katika hili kuna, kuna pande kuu mbili zinazokinzana - wanaopinga na wanaounga mkono kama ifuatavyo:-

(1) Wanaopinga: wanajenga hoja kwamba kwa kuwa Vatican ni nchi ya kidini (Kikatoliki) na kwa kuwa, kwa mujibu wa Katiba, Tanzania haina dini hivyo sio sahihi kwa "nchi" hiyo kuwa na ubalozi wake hapa nchini. Wengine wanaenda mbali zaidi kiasi kwamba hawataki kukubali Vatican ni nchi. Hata hivyo "wanalegeza" masharti kwamba kama Vatican ina ubalozi wake hapa basi ni halali kwa Tanzania kama nchi kuwa mwanachama wa taasisi za kidini kama OIC. La kushangaza hapa ni kwamba kwao uhalali wa Ubalozi wa Vatican utakuwepo endapo Tanzania itakuwa mwanachama wa hizo taasisi za kidini vinginevyo sio halali.

(2) Wanaounga mkono:hawa wanajenga hoja kwamba; kwanza Vatican ni nchi huru, yenye mamlaka kamili, na inayojitegemea kwa mujibu wa tafsiri sahihi ya neno "nchi" lilivyo na linavyotambulika kimataifa. Na wanaenda mbali zaidi kwamba sio tu kwamba Vatican ni nchi bali inatambulika hivyo rasmi na UN. Hivyo, kwa hoja hii, ni sahihi kabisa Vatican na Tanzania kuwa na mabalozi wanowakilisha nchi zao.

MLIPUKO WA LEO:

Kati ya viongozi wakuu wa Kanisa waliokuwepo kwenye shughuli ya leo kule Olasiti, Arusha, ni Balozi wa Vatican nchini Tanzania ambaye pia ana hadhi ya Askofu Mkuu. Hivyo zimeanza kuzagaa habari pengine kutokana na ukinzani wa baadhi ya makundi kutotaka Vatican kuwa na ubalozi wake hapa nchini, kuna uwezekano pia mlengwa mkuu alikuwa Balozi husika. Mimi sijui, ila kama GT tudadavue na hili.

LAWAMA:

Lawama pia zimeanza kuelekezwa kwa serikali kwa kutochukua hatua madhubuti na kwa wakati pindi zinapotokea chochoko kama hizi katika jamii. Kwa mfano, hili la upotoshoji wa uhalali wa Ubalozi wa Vatican hapa nchini propaganda zake zimeenezwa kwa muda mrefu sana kwa njia mbalimbali kama mihadhara, ibada, na hata kwenye media mbalimbali. Badala ya serikali kutolea ufafanuzi wa uhalali wa huo ubalozi, imekuwa kimya bila kujali athari za baadaye za propaganda hizi chafu pengine kwa falsafa ya "ni upepo tu utapita". Je, ni kweli serikali inastahili lawama katika hili?

HITIMISHO:

Je, kama serikali ikitekeleza madai YOTE ya haya makundi, kuna uwezekano wa chokochoko hizi kukoma na hivyo nchi yetu kuwa ya amani na utulivu kama ilivyoachwa na waasisi wetu? Lakini je, walengwa wa haya matukio ni wakatoliki peke yao? Au ni pamoja na makundi mengine? Haya matukio yana uhusiano wowote na siasa za nchi yetu? Mimi sijui, nalileta kwenu wakuu.
 
nilisema mapema, kwamba CHASO Morogoro kwa sasa si ya kubeza, mara tu baada ya huyu anayejiita mwenyekiti wa TAHLISO kuboronga na kuitaja CHADEMA kama waasisi wa vurugu,makamanda wa Chaso mkoa wa Morogoro wakiongozwa na Ebenezer kwayu, walitoa tamko la kukataa taarifa hiyo na kuhoji uhalali wa taaarifa hiyo ikiwa hawakushirikishwa.....
Morogoro pamewaka Moto
 
Duh!
Kweli tumetika mbali, yani kumchora kiongozi chuo kizima kinafungwa!

Ha ha ha KIBANGA Ampiga Mkoloni.. wakati huo punch alikuwa anafanya kazi kisawasawa.. Alichorwa marehemu Diria halafu akavalishwa sidiria.. ilikuwa noma mbona..
 
Last edited by a moderator:
Wasomi mbalimbali katika vyuo vikuu vya mkoa wa Morogoro wamelaani vikali tamko lililotolewa na Mkiti wa Jumuiya ya vyuo vikuu vya elimu ya juu nchini Amon Chakushemeire kwamba CHADEMA kinachochea migogoro kwenye vyuo vikuu nchini.

Wakizungumza kwa hasira wanafunzi kadhaa na viongozi wa wanafunzi walisema hawakuwahi kushirikishwa katika tamko hilo walilodai ni la kipuuzi kuwahi kutolewa na kiongozi wa TAHLISO.

Tayari tamko hilo la Mkiti wa TAHLISO limewagawa wanafunzi kote chini katika makundi mawili.Lile kundi kubwa la wafuasi wa Chadema na lile dogo la wafuasi wa CCM.Tamko hilo lililotolewa dhahiri lilikuwa likikishambulia Chadema bila kueleza uhalisia wa vurugu katika vyuo vikuu.

Wanafunzi hao wamemtaka Mkiti huyo wa TAHLISO kufuta mara moja tamko lake na kuliomba radhi Taifa kwa kusema uwongo.

Source:Tanzania Daima Jumapili.
Ni kweyi kabisa. Viongozi wengi wa TAHLISO ni makada wa Magamba. Na wakitoka hupandikizwa kwenye vyama vingine au kupatiwa nafasi kubwa ndani ya Magamba. TAFAKARI: viongozi walopita wako wapi? Wengine ndani ya CUF, wengine NEC ya MAGAMBA nk.
 
Back
Top Bottom