Taharuki NSSF

Taharuki NSSF

Hata Fao la kujitoa hakuna. Ukienda wanakupa form za fao la kukosa ajira ukiwauliza unaambiwa wewe ni skilled labour Hupewi pesa yako yote . Eti unskilled labour peke yao ndio wanapewa michango yao yote!
 
Hata mimi sijalipwa pensheni yangu toka Serikali Kuu inayotoka LAPF. Tunadai haki zetu na siyo fadhila.
 
Hata kama lugha ina walakini lakini muhimu ni kwamba jambo lenyewe lilikuwepo au halikuwepo.Nimasema hivyo kwa sababu yameshajitokeza mambo mengi nssf ambayo ni usumbufu kwa wazee na wanadhalilika.Mwaka jana palishaandikwa hapa kuwa wazee walicheleweshewa pensheni na wakati wanatafuta majibu mfanyakazi mmoja tunaambiwa akatoa kauli kwa wale wazee kuwa wanasaidiwa tu.Kauli ambayo ni ya ovyo mbaya na chafu kwa watu wazima wale.Usidhani taharuki ni mpaka watu wachapane ngumi na viboko.
Toa tafsiri ya taharuki acha kurukaruka
 
Pensheni shida kwa wastaafu ,bado kidogo tu na mishahara ya watumishi itakuwa kasheshe chini ya uongozi wa mtukufu malaika wa chato Jiwe .We are on the right truck.
 
Bado watu wa Fao la Kujitoa ifanyike kitu kama hii.
 
watulie tu bank clearance huchukua siku 2.5-3 so wawe na subra watapata chao
 
Leo imezuka taharuki NSSF makao makuu pale wazee wastaafu walipokusanyika kudai pension yao ya mwezi January ambapo fedha yao kwa utaratibu mpya zinaenda kwenye benki zao walipofungua akaunti zao.Akaunti zilifunguliwa wakati wa uhakiki hivi karibuni.

Wazee wale kila mmoja alikuwa akiongea lake wengine wakiwa nje ya ofisi ghorofa ya 10 wakitaka waruhusiwe kuingia ndani huku wakiambiwa wasubiri.

Walikuwa pale kuanzia majira ya saa 4 hadi saa saba alipojitokeza mfanyakazi mwananamama akiwaambia wote wakusanyike pamoja ghorofa ya 4 awape maelezo kwa pamoja.

Kule waliambiwa ni taratibu tu za kibenki lakini fedha yao itaenda kwamba wao Nssf walishapeleka NBC na CRDB .Utaratibu wa kuhamishia benki zingine ni wa kibenki.

Sasa kwa hili lina ukakasi kwa sababu Nssf walitakiwa watoe taarifa mapema kwa ujumla kwani vyombo vya habari vipo vingi tu. Sasa wastaafu waliopo mikoani nao waje Dar kupata ufafanuzi ?

Jirekebisheni Nssf.Kwa maneno niliyoyasikua leo kwa wazee wale, hakika mnawajengea chuki na serikali yao bila sababu.
NSSF na mashirika mengine kama PSPF ni wachumia tumbowakubwa. Wao wanaangalia masilahi yao binafsi huku masilahi ya wazee wakiyalalia mlango wazi. Wapuuzi wakubwa!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom