Tahadhari ya hatari: CCM Imepania Kufanya Kinyume cha Maumbile!

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,494
113,590
...Ya Rasimu ya Katiba ya Muundo wa Serikali Tatu?!.

Wanabodi, naomba nianze na Preamble ya sarufi ya lugha yetu adhimu ya Kiswahili kuhusu semantiki ya neno "kinyume cha maumbile" kwa maana safi iliyomaanishwa ndani ya uzi huu, ili kuepuka matumizi mabaya ya neno hilo yanayohusishwa na mambo mabaya!.

"Umbile" ni linatokana na neno "umbo", yaani muundo halisi wa jinsi kitu fulani kilivyoumbwa!.
"Kinyume cha Maumbile" ni kufanya kitendo tofauti na njia rasmi iliyoainishwa ya jinsi ya kufanya jambo fulani!"

Kwa msingi huo sasa twendeni kwenye mada halisi ya jinsi CCM inavyotaka kutufanya kinyume cha maumbile katika mchakato wa Katiba ndani ya Bunge Maalum la Katiba.

Hivyo tukirejea Umbo la Rasimu ya Katika katika Mfumo wa uundaji wa serikali, rasimu hiyo imeumbwa kwa umbo la mfumo wa serikali tatu. Hivyo maumbile halisi ya rasimu ya katiba ni umbile la serikali tatu!. Ni kufuatia maumbile yake halisia nia ya Bunge la Katiba ni kuijadili rasimu hiyo kwenye umbo lake la asili la jinsi ya kuunda katiba mpya yenye mfumo wa serikali tatu, na rasimu hiyo haikuweka option ya kuibadili maumbile ya rasimu hiyo kutoka maumbile ya serikali tatu, kwenda maumbile ya serikali mbili au maumbile ya serikali moja.

Hivyo kitendo cha CCM kuendelea kushikilia msimamo wa kuibadili rasimu ile kutoka muundo wake halisi wa serikali tatu na kwenda muundo wa serikali mbili, huku ni kwenda kinyume cha maumbile! hivyo inachokifanya CCM ni kutaka kutufanya kinyume cha maumbile!.

Nimefuatilia mjadala katika kipindi cha Tuongee Asubuhi na Star TV kilichokuwa live leo asubuhi, ambapo Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM, ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Mjumbe wa Bunge la Katiba, Alhaj Abdalah Bulembo, amesisitiza msimamo wa CCM itashikilia serikali mbili na utautetea msimamo huo kwa hoja, na kuwataka UKAWA warudi ndani ya Bunge la Katiba, walete mezaji hoja zao za kutetea muundo wa serikali tatu, washindane kwa hoja, hoja itakayoshinda kati ya serikali mbili na serikali tatu, ndipo ipelekwe kwa wananchi wapige kura kuipitisha hiyo katiba au kuikataa!.

Naomba kuuliza, hivi Rasimu ya Katiba iliweka options au za serikali mbili au za serikali tatu?, au CCM inataka kutupeleka kinyume cha maunbile halisi ya Rasimu ya Warioba yenye maoni ya wananchi ambao wengi wametaka serikali tatu?!.

Jee kwenye mchakato wa katiba mpya, jee tuiache CCM ikitupeleka kinyume cha maumbile rasmi ya ile rasimu ya Warioba, au tuungane kuikemea CCM ikubali kurudi kwenye mstari wa kuijadili rasimu ya Warioba katika umbile lake la asili ambalo ndio maoni ya wananchi?!.


NB. Disclaimer: Leo ni Jumapili, ni siku ya ibada kwa baadhi yetu, hivyo naomba michango kuhusu hili la CCM kutaka kuwafanya watanzania kinyume cha maumbile, tulijadili kwa mawazo safi kuhusu matumizi ya neno "kinyume cha maumbile" lijadiliwe maana safi niliyoimaanisha hapa ambayo ni ya umbile la Rasimu ya Katiba na sio kinyume cha maumbile ya tendo jingine lolote nje ya mjadala wa katiba!.

Pasco
 
Mkuu Pasco umeleta hoja ya maana.. hata mimi nimepata kumshangaa bwana Bulembo alichoongea asubuh.
Hakika sifa ya kwanza ya kuwa mwanaCCM ni kujitoa ufahamu.
 
Last edited by a moderator:
...Ya Rasimu ya Katiba ya Muundo wa Serikali Tatu?!.

Wanabodi, naomba nianze na Preamble ya sarufi ya lugha yetu adhimu ya Kiswahili kuhusu semantiki ya neno "kinyume cha maumbile" kwa maana safi iliyomaanishwa ndani ya uzi huu, ili kuepuka matumizi mabaya ya neno hilo yanayohusishwa na mambo mabaya!.

"Umbile" ni linatokana na neno "umbo", yaani muundo halisi wa jinsi kitu fulani kilivyoumbwa!.
"Kinyume cha Maumbile" ni kufanya kitendo tofauti na njia rasmi iliyoainishwa ya jinsi ya kufanya jambo fulani!"

Kwa msingi huo sasa twendeni kwenye mada halisi ya jinsi CCM inavyotaka kutufanya kinyume cha maumbile katika mchakato wa Katiba ndani ya Bunge Maalum la Katiba.

Hivyo tukirejea Umbo la Rasimu ya Katika katika Mfumo wa uundaji wa serikali, rasimu hiyo imeumbwa kwa umbo la mfumo wa serikali tatu. Hivyo maumbile halisi ya rasimu ya katiba ni umbile la serikali tatu!. Ni kufuatia maumbile yake halisia nia ya Bunge la Katiba ni kuijadili rasimu hiyo kwenye umbo lake la asili la jinsi ya kuunda katiba mpya yenye mfumo wa serikali tatu, na rasimu hiyo haikuweka option ya kuibadili maumbile ya rasimu hiyo kutoka maumbile ya serikali tatu, kwenda maumbile ya serikali mbili au maumbile ya serikali moja.

Hivyo kitendo cha CCM kuendelea kushikilia msimamo wa kuibadili rasimu ile kutoka muundo wake halisi wa serikali tatu na kwenda muundo wa serikali mbili, huku ni kwenda kinyume cha maumbile! hivyo inachokifanya CCM ni kutaka kutufanya kinyume cha maumbile!.

Nimefuatilia mjadala katika kipindi cha Tuongee Asubuhi na Star TV kilichokuwa live leo asubuhi, ambapo Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM, ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Mjumbe wa Bunge la Katiba, Alhaj Abdalah Bulembo, amesisitiza msimamo wa CCM itashikilia serikali mbili na utautetea msimamo huo kwa hoja, na kuwataka UKAWA warudi ndani ya Bunge la Katiba, walete mezaji hoja zao za kutetea muundo wa serikali tatu, washindane kwa hoja, hoja itakayoshinda kati ya serikali mbili na serikali tatu, ndipo ipelekwe kwa wananchi wapige kura kuipitisha hiyo katiba au kuikataa!.

Naomba kuuliza, hivi Rasimu ya Katiba iliweka options au za serikali mbili au za serikali tatu?, au CCM inataka kutupeleka kinyume cha maunbile halisi ya Rasimu ya Warioba yenye maoni ya wananchi ambao wengi wametaka serikali tatu?!.

Jee kwenye mchakato wa katiba mpya, jee tuiache CCM ikitupeleka kinyume cha maumbile rasmi ya ile rasimu ya Warioba, au tuungane kuikemea CCM ikubali kurudi kwenye mstari wa kuijadili rasimu ya Warioba katika umbile lake la asili ambalo ndio maoni ya wananchi?!.


NB. Disclaimer: Leo ni Jumapili, ni siku ya ibada kwa baadhi yetu, hivyo naomba michango kuhusu hili la CCM kutaka kuwafanya watanzania kinyume cha maumbile, tulijadili kwa mawazo safi kuhusu matumizi ya neno "kinyume cha maumbile" lijadiliwe maana safi niliyoimaanisha hapa ambayo ni ya umbile la Rasimu ya Katiba na sio kinyume cha maumbile ya tendo jingine lolote nje ya mjadala wa katiba!.

Pasco

Rasimu iliweka option ya serikali moja kwa nini way rioba aamulie waliowengi option ya serikali alilotakiwa ni kuweka option nyingi akielezea uzuri na na ubaya wake na kuachia bunge kufanya maamuzi.
 
Kwa msingi huo sasa twendeni kwenye mada halisi ya jinsi CCM inavyotaka kutufanya kinyume cha maumbile katika mchakato wa Katiba ndani ya Bunge Maalum la Katiba. Pasco
With due respect, pamoja na ufafanuzi wako wa awali, lakini please, badili hiyo sentensi na iwe kama kichwa cha habari kinavyosema kwamba "CCM Kufanya kinyume na....!!" Lakini "kutufanya kinyume..." hapana aisee, ngumu kumeza...
 
Unahitaji uwe mlevi ili uweze kumsikiliza bulembwe!

Kuhusu mada...
Je ndugu Pasco waweza kumjua ni nani hasa ndani ya ccm mwenye nia thabiti ya kuwafanya watanzania kinyume na maumbile?kwangu mimi naamini si wote ingawa hao wenye msimamo wa kupinga tendo la kinyume cha maumbile ni waoga na kwa mbaali ni wanafiki ndio maana tulipoteza majuma kadhaa kujadili aina ya upigaji kura-wazi vs siri.

Ndugu Pasco wataje kwa uchache wao ili watanzania waanze kuwafanya kinyume na maumbile mapeema!

Bado naendelea kukuita wewe Pasco mzee wa vibahasha, sasa leo hii ndio umeshitukia hili??? Au kwa kuwa umenyimwa bahasha???
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Pasco
Si CCM peke yake, hata mimi sizitaki serikali tatu. Sina imani nazo kabisa na usalama wa nchi yetu. Nchi haiendeshwi kwa majaribio. Pamoja na kwamba tume pendwa imependekeza serikali tatu, kwangu naona ni kama nadharia tu ambayo practically haiwezi kutoa majibu kama rasimu yenyewe inavyopendekeza. Kushauri ni jambo moja, na kuutumia huo ushauri katika uendeshaji na kutoa majibu tarajiwa ni jambo jingine. Kwangu mimi, ni mara mia kuwa na serikali moja kuliko kuwa na serikali tatu. Niweke tu wazi, endapo bunge litabariki serikali tatu, mimi na familia yangu tutakuwa wa kwanza kwenye foleni ya upigaji kura ili kupiga kura ya kuikataa rasimu hiyo.
 
Last edited by a moderator:
Rasimu iliweka option ya serikali moja kwa nini way rioba aamulie waliowengi option ya serikali alilotakiwa ni kuweka option nyingi akielezea uzuri na na ubaya wake na kuachia bunge kufanya maamuzi.

Hivi hii ndio ile rasimu mliyoipokea kwa mbwembwe na bashasha au kuna nyingine?
 
Pasco, leo kwa mara ya kwanza hiyo creativity yako imenikera. Maumbile yanatumika kuelezea viumbe hai. Katiba ni muundo au ungeweza hata kusema umbile! Kwenye siasa ubunifu wa hivi haupendezi
 
Last edited by a moderator:
Niseme wazi kwamba suala zima limevurundwa... ni bahati mbaya sana hakuna hapo kabla ambae alifikiria suala la muundo wa serikali ingekuwa ni hoja ngumu kiasi hiki vinginevyo hata sheria za mabadiliko ya katiba zingekaa imara katika hili... matokeo yake, hata sheria yenyewe haiaminiki... ndio maana hata wadau watetezi wa serikali tatu nao wanaogopa hata kwenda mahakamani kuomba ufafanuzi wa ile sheria kama ibara inaweza kubadilishwa au hapana... wana hofu kwamba, wanaweza kwenda mahakamani na bado ikala kwao... hayo ni matokeo ya kutoangalia nini kinaweza kutokea! Sioni sababu kwanini sheria haikua crystal clear kwamba BMK halitakuwa na mamlaka ya kubadili ABC...
 
MKUU PASCO, kwanza nideclare interest kwamba mimi ni kada wa ccm kabla sijaanza kuchangia uzi wako ila nataka kuwa objective kwenye hili,kwanza suala la msingi hapa sio muundo wa muungano,bali ni muungano wa nani na nani,wa nchi ipi na ipi,wananchi wajue kwa sasa TANZANIA imepoteza uhalali wa kuwa nchi tangu siku wanachi wa zanzibar walipoamua kuwa na katiba yao,na nchi yao na taifa lao na dola yao na bendera pia na nembo yao. swali la serikali mbili ni zipi kama sio tanganyika na zanzibar ? tanzania hapa inatoka wapi wakati katiba ya uhalali huo imevurugwa 2010,sote tuwe wakweli mbele za MUNGU,kisha mbele ya katiba ya jamhuri ya muungano ya tanzania iliyovunjwa,kisha mbele ya ukweli na mwisho mbele ya HAKI. tusiruhusu kusema uongo kama bulembo tutageuka jiwe la chumvi kama ilivyokuwa kwa mke wa lutu,na kwanini tuipoteze nchi yetu ya TANGANYIKA kwa hofu za udhanifu tu kama bulembo ? na bado TANZANIA sio jina halali kwa sasa mara baada ya zanzibar kuwa nchi.kwa hiyo ndani ya tanzania sasa kuna nchi moja ya tanganyika na TANZANIA NI KOTI LA MUUNGANO na sio la WATANGANYIKA. WATANGANYIKA wasinyimwe haki yao ya msingi kwa kuvikwa koti lisilo lake.watanganyika wajue ukweli huu
 
Hapo ni kupoteza muda na fedha zangu mvuja jasho. Zaidi ya asilimia 30 ya maisha yangu yanakamuliwa kodi kwa ajili ya kuwalipa wapuuzi hawa eti wanatunga sheria ambazo hawataki kuzifuata wala kuzisimamia. Wao ni mstari wa mbele kutolipa kodi lakini wakati huo huo wanatunga sheria na kutaka serikali ikusanye kodi sana na walipwe zaidi? kwa performance zipi? Wao hawanataki wala kuonyesha nia ya kulipa kodi ILA WALIPWE ZAIDI kwa kazi za kipuuzi zisizo leta tija kwa Taifa??

Kama ni hoja zilishatolewa na hao UKAWA na yeyote mwenye mawazo ya kawaida anaona umuhimu wa rasimu ya pili ya katiba isipokuwa kipofu wa maandiko hayo anayehofia kupata hasara kwa utekelezaji wa andiko lile. Kama vipi kama lengo ni kutaka kudumisha muungano nadhani wahenga wamesema sana kwamba umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu hivyo moja ni bora zaidi kuliko mbili au tatu au nne.!!!!??

Lakini pia kama hawataki kukubaliana na hoja ya serikali tatu je, wanaweza kukubali kubaki na serikali mbili halafu mambo mengine katika rasimu ya pili ya katiba yabaki kama yalivyo?

Kuanzia sasa napendekeza wabunge wote wasiitwe kwa kutanguliza neno Mheshimiwa, wanayo yafanya pale Bungeni hawastahili kuitwa waheshimiwa hata kidogo!

Kama taifa hatutambui umuhimu wa muda katika kazi zetu, sheria waliyotunga wao wenyewe waliandika kuwa vikao vya majadiliano ya Rasimu ndani ya Bunge yatakuwa kwa siku 60-70 na kama ikibidi basi wataongezewa hadi siku 90 kwa maana ya ongezeko la siku 20-30. Siku hizo zikapita na sasa wameongezewa hadi siku 60 kwa mapenzi ya mkuu wao Rahisi. Kama kawaida yao siku hizi zilizoongezwa nazo zitakwisha na hakutakuwa na lolote la maana. Na kipi kipya cha kujadili na kuchukua muda wote huo katika Rasimu ya pili ya katiba mpya?????????

Hapo ni kufanyia kazi matumbo yao tu. Na walipe kodi basi ili wale zaidi?? Hakika hawana maan yoyote na vitendo vyao ni sawa na anaye kamua ndama ili ashibishe ng'ombe wa Maziwa???? Mimi ni ndama wao ni ng'ombe wa maziwa na nyama.

Inafika mahali mtu unajuta kuitwa Mtanzania, kila kitu hovyo! Utadhani hatuna viongozi? Hivi nini maana ya Kiongozi?????????
 
Kwa mtazamo wangu wanaotufanya kinyume cha maumbile ni Jaji Warioba kwa kubadili mfumo wetu uliotuhakikishia amani kwa muda mrefu. Sasa yeye wakafanya jaribio la kutuingilia kinyume cha maumbile bila ya ridhaa yetu. Waliozoea kufanya kinyume cha maumbile (UKAWA) wakanogewa. Sisi ambao hatujazoea kuingilia au kuingiliwa kinyume na maumbile tukakataa na kusimamia msimamo wetu. Kwa vile hawa walionogewa kuingiliwa kunyume cha maumbile ni wachache, wakaamua kutoka nje ya bunge na kuapa kuwa hawatarejea bungeni ikiwa tulio wengi hatutakubali kuingiliwa kimaumbile. Nasema potelea mbali. Tutaendelea na msimamo wetu wa kutoingilia au kuingiliwa kinyume na maumbile. Tuwaachie akina Pasco walionogewa kuingiliwa kinyume cha maumbile
 
MKUU PASCO, kwanza nideclare interest kwamba mimi ni kada wa ccm kabla sijaanza kuchangia uzi wako ila nataka kuwa objective kwenye hili,kwanza suala la msingi hapa sio muundo wa muungano,bali ni muungano wa nani na nani,wa nchi ipi na ipi,wananchi wajue kwa sasa TANZANIA imepoteza uhalali wa kuwa nchi tangu siku wanachi wa zanzibar walipoamua kuwa na katiba yao,na nchi yao na taifa lao na dola yao na bendera pia na nembo yao. swali la serikali mbili ni zipi kama sio tanganyika na zanzibar ? tanzania hapa inatoka wapi wakati katiba ya uhalali huo imevurugwa 2010,sote tuwe wakweli mbele za MUNGU,kisha mbele ya katiba ya jamhuri ya muungano ya tanzania iliyovunjwa,kisha mbele ya ukweli na mwisho mbele ya HAKI. tusiruhusu kusema uongo kama bulembo tutageuka jiwe la chumvi kama ilivyokuwa kwa mke wa lutu,na kwanini tuipoteze nchi yetu ya TANGANYIKA kwa hofu za udhanifu tu kama bulembo ? na bado TANZANIA sio jina halali kwa sasa mara baada ya zanzibar kuwa nchi.kwa hiyo ndani ya tanzania sasa kuna nchi moja ya tanganyika na TANZANIA NI KOTI LA MUUNGANO na sio la WATANGANYIKA. WATANGANYIKA wasinyimwe haki yao ya msingi kwa kuvikwa koti lisilo lake.watanganyika wajue ukweli huu

we jamaa ni gamba lenye damu ya kikamanda!
Ndio maana nikamtaka pasco awe wazi ni magamba wangapi wanataka kutenda upuuzi huo?
 
Asubuhi Bulembo ametapatapa na kutapika mengi sana, lakini anasahau kwamba

1. Dunia inabadilika na watu wanabadilika, hivyo ccm inapaswa kubadilika ilikukabili mabadiliko na kuenda na wakati ili ikubalike katika jamii.


2. Watanzania waleo sio wale wa miaka ya kupigia kura picha na kivuli, watu wanataka ukweli sio ufundi wa propaganda, uraghai, unafiki na janjajanja.

3. Wazanzibar wanataka uhuru wao kamili hivyo muundo pekee watakaoukubali ni waserikali tatu yaani uhuru kamili.



-Wana katikaba yao ya Zanzibar

-Wana bendera yao ya Zanzibar

-Wana amirijeshi wao Zanzibar

-Wana mipaka na

-Bunge lao ambamo watanganyika hawana mwakilishi

kwa mantiki hiyo njia sahihi nikuwapa watanganyika uhuru nao wamiliki maamuzi sahihi badala ya kuificha tanganyika ndani ya blanketi la muungano

Rasim ya Jaji mstaaf Warioba kwa wakati tulionao yupo sahihi kwa 100%-serikali3
 
Back
Top Bottom