Tahadhari UKAWA.

Tahadhari UKAWA.

KISHADA

JF-Expert Member
Joined
Oct 18, 2012
Posts
2,226
Reaction score
3,293
Tulio wengi wanaotaka mabadiliko nchini tunafurahishwa na movement zenu na tumepata tumaini jipya kuelekea mabadiliko ya kweli. Lakini tuna kila wasiwasi kutokana na uzowefu wa nchi hii pale inapofika wakati harakati za mabadiliko zinapogusa interest za watawala mara nyingi hutokea yasiyotabiriwa.( Mungu aepushie mbali ). Kwa muktadha huo basi , mimi naomba nitoe tahadhari hizi. 1.Kwanza kipindi hiki mjuwe mmeigusa system ilivyo kuanzia bunge la katiba na bunge la bajeti hasa kuhusu muungano, kwa kuwa huu muungano ndio chaka la watawala kuficha mambo yao basi kutazuka mambo mengi ya hatari ikibidi hata jaribio la kupotezwa watu maisha NAOMBA MUWE MAKINI MARA 100 kuepuka kutoa mianya ya kudhuriwa hasa katika SAFARI ZENU MIKOANI. Tafuteni washauri wenu wa KIUSALAMA ili kuwapa mikakati mizuri zaidi. 2. Kuna kila dalili umoja wenu unawatisha wahafidhina watawala kote Zanzibar na Bara na wako mafichoni kuja na mkakati wa kuvunja umoja wenu immediately, hawatoacha kutumia mianya ya tofauti zenu katika umoja wenu ili kupandikiza mgogoro na hatimae kuvunja nguvu yenu, kamwe msiwe rahisi kwa hilo na mjifunze kwa yaliyopita haiwezekani kuiondowa CCM bila kuwa wamoja, hawa jamaa wameota mizizi katika system kuanzia muhimili wa mahkama, serikali/ utendaji na bunge na hata katika vyama vingi vya upinzani wameweka nyenzo imara. Sahauni tofauti zenu, jengeni umoja imara, aminianeni, tengeneza mkakati wa kitaalamu, shambulieni kwa hoja, muwe wanganganizi wa hoja, toweni data na facts katika hoja, wapotezeni kujuwa mikakati(tunza siri), ongeza intelijensia na kuchimbua katika Banks za mikiakati yao finyu na propaganda, panga safu kali ya mashambulizi, buni njia za kupata bajeti kwa wakati, kuweni waangalifu wa hali kwa jamii na hisia zao halafu muwe tayari- nawaambia jamaa hawawezi kutoka safari hii tafadhali kuweni makini na haya inatosha.
 
umesomeka mkuu
shukurani. Ila naomba MODS waweke para mimi imenishinda na anaejuwa anielekeze maana kila nikitumia hizo ICON zinashindwa kurespond labda sina utaaalamu.tafadhali nifahamisheni.
 
Umenena vema mkuu ,Umoja ni nguvu na ili kuusambaratisha mlima(ccm) lazima kila mwana UKAWA aikane nafsi yake mwenyewe na aje akiwa huru bila kufungamana na msimamo wa chama chake ili aje alete ukombozi katika jamii ya kitanzania inayokerwa na ufisadi,dhuruma na ukandamizwaji wa kifikra.
 
Ushauri mzuri umeutoa mkuu,naamini wahusika wanapita sana humu na hivyo hawatokupuuzia hoja zako hata kidogo japo na wao wanatambua sana haya uliyoyasema. Ukweli unabaki kuwa watanzania wenye nia njema na nchi yao hawakosi neno jema la kushauri lakini wenye hila nao hawakosekani kwa maneno yao ya chuki,visa na matusi.

Ukawa wakijua kuwa ni watanzani wangapi wako nyuma yao,naaminini Si Mbowe,wala Mbatia,wala Prof.Lipumba,wala Lissu,wala Machali,wala KAfulila,wala Mkosamali watakao anzisha zogo la kutengana.Umoja daima mbele!
 
Back
Top Bottom