Tahadhari kwa Zitto Kabwe

Tahadhari kwa Zitto Kabwe


Siasa zetu za kiafrika sio sawa na zile za nchi zilizoendelea, kwamba sera pekee zinaweza kumshawishi mtu akuunge mkono katika chama chako, hapa kwetu unajua vyama vyetu wafuasi wengi wana matarajio ya muda mfupi na wanalenga kupata jambo fulani kipindi fulanI, katika muktadha huu utakuta Migogoro mingi inaibuka kwenye vyama hivi ambavyo havina rasilimali za kutosha mwisho mgogoro ukikomaa utakuta chama kinakufa kifo cha kawaida, na hapa sina maana chama kifutwe kwa msajiri.

= msajili
 
mnashangaza sana nyie mijusi. zitto siameshaondoka chadema? hizi porojo zote zanini tena? fanyeni yenu muacheni na zitto afanye yake.

Naam, Bwana Zitto Sikia haya ninayoenda kuandika hapa. Siasa zetu katika nchi za kiafrika ni zaidi ya Siasa.Ujenzi wa chama si kazi ya lelemama kwanza inahitaji watu makini,pesa,mipango mkakati iliyo madhubuti na uwanja sahihi wa kufanyia siasa zenyewe.

Siasa zetu za kiafrika sio sawa na zile za nchi zilizoendelea, kwamba sera pekee zinaweza kumshawishi mtu akuunge mkono katika chama chako, hapa kwetu unajua vyama vyetu wafuasi wengi wana matarajio ya muda mfupi na wanalenga kupata jambo fulani kipindi fulanI, katika muktadha huu utakuta Migogoro mingi inaibuka kwenye vyama hivi ambavyo havina rasilimali za kutosha mwisho mgogoro ukikomaa utakuta chama kinakufa kifo cha kawaida, na hapa sina maana chama kifutwe kwa msajiri.

Hakika kuna matarajio uliyonayo moyoni mwako lakini hayataweza kutokea katika siasa za ACT maana sasa wale waliokupokea wanahitaji muda ili waanze kupishana na wewe na hapo ndio utajikuta unakuwa Easy target.Chama kikiyumba utakuwa unajiona unalo jukumu la kurekebisha mambo na hapo Zitto utakuwa hauna amani tena moyoni utakuwa unajutia yale yaliyotokea na yanayobeba historia ya maisha yako kisiasa.

Sasa jukumu unalo tena zito,kipindi hiki unapoangalia mbele kwenye uchaguzi mkuu ujao,hakika itakuwa ni kazi ngumu mno wewe kurudi bungeni katika kipindi hicho ijapokuwa unaweza ukadhani ni rahisi lakini nataka nikwambie kwamba si rahisi maana kazi uliyonayo itakuwa kukijenga chama na si kujenga himaya yako ndani ya ACT,Akina Mwigamba naweza kusema hakuna chemistry kati yako na Mwigamba na hilo litakuwa tatizo la msingi.

Mwigamba anaamini katika mawazo yake na wewe pia, kamwe hamtaweza ku compromise pindi mkitofautiana katika harakati zenu mlizo anza.

Safari hii uliyoianza ni tofauti kabisa na ile uliyoianza pale ulipokua na umri wa miaka 16. kipindi hicho ulipata mafanikio mengi ndani ya siasa na nje ya siasa, ulipewa nafasi na chama chako kutenda majukumu makubwa,lkn safari hii ukiwa na umri wa 39 umeanza safari mpya yenye mashaka mengi.

Anaamini atakijenga chama chake kwa hisani ya CCM, hiyo ndo turufu pekee aliyonayo. Lakini akumbuke wakiona jitihada zake zinakwama watamtupa kama kondom iliyotumika!

Zitto atakuja sana kumlaumu Kitila Mkumbo. Mambo yakianza kukwama tu Zitto ataanza kumtafuta mchawi wake. Na hapa ndipo Kitila Mkumbo atakapoanza kutofautiana na Zitto.

zitto anadhani kejenga chama cha siasa ni mchezo haya sasa kazi kwako

Ushauri wako na tahadhari ni muhimu. Zitto ana anadhani atarudi tu bungeni kirahisi. Thubutu anatakiwa atoke jasho!

Nina hakika ZZK hatakuwa mgombea wa urais wa ACT ila mfadhiri wao mkuu ambae pia amekalia kuti kavu CCM. Yeye anadhani asipopitishwa na CCM atakimbilia ACT na kushinda, huoni mashehe tayari wameanza kuwa karibu nae.MARK MY WORD.

Zito atakuwa kama Lamwai au mrema. Anadhani chama kinajengwa kwa cku moja. Kwanza mpaka sasa amesha choka kwani zile transactions kutoka ccm hakuna tena
 
I
Kigoma Kaskazini unaposema ni safe harbour kwa Zitto si sahihi Ukiangalia matokeo yake ya kwanza na ya uchaguzi uliopita. Anakukimbia huko kwa sababu anajua yaweza kuwa ngumu kwake kushinda. Siasa za kigoma tunajua ni za upinzani, lakini huwezi kuwatoa kabisa chama tawala. It is a risk undertaking, ikiwa bahati mbaya akashindwa kupata ubunge na wabunge sijui kama anayo subira ya miaka mitano. Lakini pia yawezekana kwake haikuwa rahisi kwenda ccm kwa sababu maalumu ikiwemo pia uwezekano kwamba huko hasingetimiza matarajio yake?
Kaka Zitto alishinda kata 9 kati ya 11 Kigoma Kaskazini jee kuna ushindi landslide zaidi ya huo? Kusema kwamba Kigoma Kaskazini inaweza kwenda CCM hilo kaka nadhani utakuwa umekosea, UKAWA hawezi kusimamisha mgombea Kigoma Kaskazini sababu hiyo ni wastage ya resources.

Kigoma yoyote Zito akigombea anashinda, sababu that is facts huko kwao yeye ni shujaa wao. Pili, katika majimbo ambayo ama CUF au CDM walikuwa na wagomebea wenye nguvu sawa na UKAWA wakigawa jimbo kwenda kwa moja ama CUF au CDM basi jua mwingine atajiunga ACT. Zitto is not stupid, yeye sherehe yake ni UKAWA kwani anakuja na mbadala au alternative.

Anachotakiwa ni kushinda wabunge 5-10 ili apate pesa ya Ruzuku, baada ya hapo miaka 5 ijayo akafanya national politics. Kitila anajua fika kabisa kwamba wao kushinda national politics ni ndoto za mfalme njozi, lakini wanaweza kushinda Kigoma, Tabora na wakatoa upinzani mkali sana baadhi ya sehemu kama Arusha. Ninavyoona Msando atagombea Arusha, he have money and mvuto maana yake atagawana Kura na Lema, means CCM will win.

Kwa mara ya kwanza tunaweza kuona analytical and calculated political campaign, sababu ya scarcity of resources nadhani ACT watajikita sehemu ambazo wana chance.
 
Naam, Bwana Zitto Sikia haya ninayoenda kuandika hapa. Siasa zetu katika nchi za kiafrika ni zaidi ya Siasa.Ujenzi wa chama si kazi ya lelemama kwanza inahitaji watu makini,pesa,mipango mkakati iliyo madhubuti na uwanja sahihi wa kufanyia siasa zenyewe.

Siasa zetu za kiafrika sio sawa na zile za nchi zilizoendelea, kwamba sera pekee zinaweza kumshawishi mtu akuunge mkono katika chama chako, hapa kwetu unajua vyama vyetu wafuasi wengi wana matarajio ya muda mfupi na wanalenga kupata jambo fulani kipindi fulanI, katika muktadha huu utakuta Migogoro mingi inaibuka kwenye vyama hivi ambavyo havina rasilimali za kutosha mwisho mgogoro ukikomaa utakuta chama kinakufa kifo cha kawaida, na hapa sina maana chama kifutwe kwa msajiri.

Hakika kuna matarajio uliyonayo moyoni mwako lakini hayataweza kutokea katika siasa za ACT maana sasa wale waliokupokea wanahitaji muda ili waanze kupishana na wewe na hapo ndio utajikuta unakuwa Easy target.Chama kikiyumba utakuwa unajiona unalo jukumu la kurekebisha mambo na hapo Zitto utakuwa hauna amani tena moyoni utakuwa unajutia yale yaliyotokea na yanayobeba historia ya maisha yako kisiasa.

Sasa jukumu unalo tena zito,kipindi hiki unapoangalia mbele kwenye uchaguzi mkuu ujao,hakika itakuwa ni kazi ngumu mno wewe kurudi bungeni katika kipindi hicho ijapokuwa unaweza ukadhani ni rahisi lakini nataka nikwambie kwamba si rahisi maana kazi uliyonayo itakuwa kukijenga chama na si kujenga himaya yako ndani ya ACT,Akina Mwigamba naweza kusema hakuna chemistry kati yako na Mwigamba na hilo litakuwa tatizo la msingi.

Mwigamba anaamini katika mawazo yake na wewe pia, kamwe hamtaweza ku compromise pindi mkitofautiana katika harakati zenu mlizo anza.

Safari hii uliyoianza ni tofauti kabisa na ile uliyoianza pale ulipokua na umri wa miaka 16. kipindi hicho ulipata mafanikio mengi ndani ya siasa na nje ya siasa, ulipewa nafasi na chama chako kutenda majukumu makubwa,lkn safari hii ukiwa na umri wa 39 umeanza safari mpya yenye mashaka mengi.

Well said. Take my LIKE!!
 
Changamoto kubwa ipo mbele yake!! kama ataendelea kusikiliza maneno ya wapambe wake na siasa za kuihujumu CDM mwisho wake utakiwa mbaya zaidi.

Hivi Zitto anaujasiri gani kwa sasa wa kuichachafya CCM? wanamfaham A to Z. Mnafikiri wale akina Kibajaji na Ngeleja ni wajinga sana kiasi hicho kwa kuropoka maneno yale? Ni kwa sababu bado mfumo unamuhitaji ndio maana wanapotezea wasimuabishe!!

The moment atakapoonekana the really threat kwa CCM ndiyo wakati muafaka watakapomuacha uchi. Ila kwa sasa kwakua anapambana na adui wao mkuu ni kipenzi kupitiliza!!

Huwezi kuitaja CDM bila kumtaja Zitto. Wao ni watu wa mwanzo kabisa kurecruit vijana. Kama atatumia same strategy na kuweka ego nyuma few years badae tutazungumza hapa kwamba ACT is a powerhouse. Muhimu hapa ni discipline, maana chama kipya lazima awe na discipline ya juu. Well organized and executed strategy maana bila ya hilo hakuna litakalo wezekana.

Chance anayo. How big or slim is yet to be determine. Kwa ambao ni critics jee mlitaka aende wapi baada ya kuondoa jina lake? He have very few options, mwanaume akimbii majukumu bali anayakabili. For this I support his motive am yet to support his movement. Mwaka 2006 nilipoonana na zitto first time nilimuuliza kwamba wewe unakubali vipi kuongozwa na Mboe, alitoa sababu za kizungu mkuti. Miaka 8 badae amefanya jambo ambalo wengine tulidhani angelifanya miaka hiyo.
 
mnashangaza sana nyie mijusi. zitto siameshaondoka chadema? hizi porojo zote zanini tena? fanyeni yenu muacheni na zitto afanye yake.

Tuli dawa ikuingie, kumbe ukweli unauma siyo !!? na bado dose inaendelea.
 
Hata mbuyu ulianza kama mchicha, hiki chama kitakuja kuwa tishio kwa Chadema, wait and see...ZZK ana wafadhili wengi ndani na nje ya nchi...wewe waache tu hawa kina Mtei na Mbowe waendeleze ukabila, udini na ukanda ktk hiyo NGO yao!...

Kwani cdm ndio chama tawala?mbona unaongea kama unachuki binafsi na cdm?kumbuka kuwa cdm ni chama cha upinzani tu kama hiyo act,
 
Nje ya CDM Zito si kitu kabisa.
Pia namusihi awe mwangalifu na katibu wake.Katiba ya ACT inaonyesha inampatia madaraka makubwa zaidi Katibu kuliko mwenyekiti,hususani katika uitishaji vikao vya maamuzi.Ndiyo maana iliwezekana kumuondoa aliyekuwa mwenyekiti Limbu.
 
unaonaje mkuu ukijiunga na familia ya sheikh yahya mkafanya kazi ya utabiri wa nyota maana unafaa sana.

Shekhe yahya alitabiri simba inafungwa ikawa tofauti akaokolewa na ffu
 
kwani act nia yao ni kuwa chama kikuu cha upinzani au kushika dola?
kama dhamira yao nikuwa chama kikuu cha upinzani waendelee kuitishia chadema
ila kama wanalengo la kushika dola itabidi wawe tishio kwa ccm

Mkuu act ni chama cha kuidhoofisha cdm na hawana nia ya kushika dola,wanapigania ccm iendelee kutawala milele huo ndio ukweli.
 
Duh leo bavicha naona hamjakunywa chai wala lunch, zitto kawamaliza kabisa maana mnapokezana tu kufungua uzi wake, mara Facebook mara twitter mara Jf, bundle leo zinalipwa ufipa kwa foleni,

Bavicha hawana mpango na msaliti,wapo busy kuhesabu ni vitongoji vingapi cdm imeshinda ktk uchaguzi wa serikali za mitaa.
 
Kwanza namsihi Zitto asisimamie pesa,asimamie umma wa Tanzania katika kumiliki uchumi wa nchi na haki za raia. Huu ni mtaji tosha kuliko pesa. Kina Nyerere walichangiwa pesa sembuse wewe? Kazana kaka hilo BARAZA LA VICHAA (BAVICHA) lina assigment maalum humu jf. Pengine sasa tutapata chama cha kizalendo cha ukweli

Chama cha kizalendo kwa act?
 
Zitto alijiona yupo juu ya chama aende kujenga chama chao cha wasaliti ACT. Yeye anadhani kujenga chama cha siasa ni kazi rahisi aende kuijenga ACT tuone sasa

Act ni kundi la wasaliti na malipo ya msaliti ni aibu
 
CCJ wamepotelea wapi mbona siwasikii tena walianza kwa mbwembwe kama hizi
 
Naona focus ya upinzani inaanza kupotea. Vyama pinzani vinaanza kuwindana vyenyewe kwa vyenyewe. CCM itazidi kupeta miaka nenda rudi. Sasa naanza kuamini ule usemi wa wazungu kwamba demokrasia ya kweli itachukua muda mrefu sanaaaa kuja kupatikana katika nchi za africa.

Hata mbuyu ulianza kama mchicha, hiki chama kitakuja kuwa tishio kwa Chadema, wait and see...ZZK ana wafadhili wengi ndani na nje ya nchi...wewe waache tu hawa kina Mtei na Mbowe waendeleze ukabila, udini na ukanda ktk hiyo NGO yao!...
 
Back
Top Bottom