Tahadhari Kwa Wezi Wa Simu Mtaani!!!

Tahadhari Kwa Wezi Wa Simu Mtaani!!!

chakii

JF-Expert Member
Joined
Sep 15, 2013
Posts
21,359
Reaction score
27,739
Simu ya mkononi iliyokuwa imeibwa ilituma ujumbe mfupi na picha ya mwizi wa simu hiyo kuonyesha ndiye mmiliki wake.

Polisi katika eneo la Essex nchini Uingereza wanamtafuta mwizi wa simu hiyo aina ya HTC iliyoibiwa kutoka kwa koti la mwanafunzi mmoja alipokuwa safarini kuelekea nyumbani.

Mwenye simu alikuwa ameweka kifaa cha usalama kwenye simu hiyo ambacho kinaifanya simu kumpiga picha mtu anapojaribu kuingiza nambari ya siri au PIN mara tatu bila kufanikiwa.

Msemaji wa Polisi alisema simu hiyo ilimpiga picha mwanaume huyo alipojaribu kuingiza nambari hiyo bila kufanikiwa.

Barua Pepe ya mwanafunzi huyo ilituma ujumbe kwa polisi kuwaarifu kuhusu wizi huo.


Mshirikishe na mwenzio habari hii.

Source; BBC Swahili.
 
Mkuu nilifikiri wezi hawa ni wa kariakoo kumbe ni majuu na hao huwa hatuwawezi wako mbali sana na sisi ndio kwanza uko na mchakato wa vipengere vya kumdidimiza mlala hoi na tukimaliza hapo ndio tutakuwa na mashindano ya vazi la tangayika
 
Mkuu nilifikiri wezi hawa ni wa kariakoo kumbe ni majuu na hao huwa hatuwawezi wako mbali sana na sisi ndio kwanza uko na mchakato wa vipengere vya kumdidimiza mlala hoi na tukimaliza hapo ndio tutakuwa na mashindano ya vazi la tangayika

teknolojia inakuwa kwa kasi sana mkuu,. Hata kwetu hizi HTC mbona tunazo? It's just the matter of transforming technology,.
 
Mbona icho kitu cha kawaida sana hata note 3,s4,s5 na android nyngne nying znauwezo huo ni swala la setting wengi hawajui jinsi ya kuset
 
Nimeipenda hiyo app.
Ila kibongo bongo mwizi atakana tu
hata kama picha yake imetumwa kwenye email.
 
Mkuu nilifikiri wezi hawa ni wa kariakoo kumbe ni majuu na hao huwa hatuwawezi wako mbali sana na sisi ndio kwanza uko na mchakato wa vipengere vya kumdidimiza mlala hoi na tukimaliza hapo ndio tutakuwa na mashindano ya vazi la tangayika

Km una i phone ni simple downloads icaughtU probayo yote yapo me cku iz ata nikitoka bafun mipicha kibao ya dem wangu kwenye e-mail kumbe anaangaika kufungua pasword ni nouma kaka!
 
polisi wenyewe wa kwetu wako bize, itakuwa kazi kufatilia matukio ya simu
 
Siemens c25 is beat photo ? not beat. It not steal modern phone with android OS .Customer thiefman of Kinondoni manyanya will steal phone without OS only. so how you can catch thiefman ?
 
Sasa hukuu hata ukiiweka hiyo system polis wetu vilazaaa mpaka uwahongeeee tenaaa lol
 
Mwenyewe yangu nimidownloadia hiyo app. Ila most of time nakuta picha ya my wife!!* hehehehe huwa nacheka sana
 
Km una i phone ni simple downloads icaughtU probayo yote yapo me cku iz ata nikitoka bafun mipicha kibao ya dem wangu kwenye e-mail kumbe anaangaika kufungua pasword ni nouma kaka!

Ngoja na mm nijaribu hii


Sent from my iPhone using JamiiForums mobile...
 
Download AVG antivirus kwenye simu ya adroid utapata hiyo huduma.
 
Siemens c25 is beat photo ? not beat. It not steal modern phone with android OS .Customer thiefman of Kinondoni manyanya will steal phone without OS only. so how you can catch thiefman ?
Hiki nini umeandika jamaa'ngu...
 
Siemens c25 is beat photo ? not beat. It not steal modern phone with android OS .Customer thiefman of Kinondoni manyanya will steal phone without OS only. so how you can catch thiefman ?

R.I.P English!
 
Simu ya mkononi iliyokuwa imeibwa ilituma ujumbe mfupi na picha ya mwizi wa simu hiyo kuonyesha ndiye mmiliki wake.

Polisi katika eneo la Essex nchini Uingereza wanamtafuta mwizi wa simu hiyo aina ya HTC iliyoibiwa kutoka kwa koti la mwanafunzi mmoja alipokuwa safarini kuelekea nyumbani.

Mwenye simu alikuwa ameweka kifaa cha usalama kwenye simu hiyo ambacho kinaifanya simu kumpiga picha mtu anapojaribu kuingiza nambari ya siri au PIN mara tatu bila kufanikiwa.

Msemaji wa Polisi alisema simu hiyo ilimpiga picha mwanaume huyo alipojaribu kuingiza nambari hiyo bila kufanikiwa.

Barua Pepe ya mwanafunzi huyo ilituma ujumbe kwa polisi kuwaarifu kuhusu wizi huo.


Mshirikishe na mwenzio habari hii.

Source; BBC Swahili.

hicho kifaa kinapatikana na huku kwetu pia? Nakihitaj, kama kinapatikana nijulishe
 
Back
Top Bottom