mawazo ya mtu masikini ni tofauti kabisa na ya mtu tajiri!
halafu hao hao wakishapata vipesa vya bagia, huwa wanajisahau kabisa kama walikuwa na malengo hayo!
kuna jamaa yangu mmoja alikuwa na pesa sana miaka ya nyuma wakati anauza dhahabu kule nyamongo!
basi kijana huyu kabla hajazigusa, alikuwa na malengo lukuki ikiwemo kama la mtoa mada. kijana aliishia kutumbua vimilioni
vyake vya dhahabu alivyokuwa akivipata miaka hiyo ya nyuma! alifikia kipindi anakodi gari kutoka nyamongo na kuja kula
starehe villa park mwanza, hapo malengo ya kujenga sijui aliyapeleka wapi!!!
basi bana, mali bila daftari, husepa bila information, kijana baada ya miaka miwili akafulia kabisa kabisa akiwa hajafanya chochote. pamoja na kupata pesa nyingi sana wakati anauza uza madini, hakuweza kujenga hata room moja.
wakati mwingine, kutimizika kwa malengo kunatokana na kichwa mtu kimekaaje na amejipangaje na hata kutoka na kuona wengine wamefanya nini zaidi yako, inasaidia sana kutimiza malengo yako!
lakini endapo utakuwa wewe kila siku uko na watu wale wale wa jana na leo, mtaishia kushauriana mambo yale yale na wengine ndio hao watakaokua wana kuvunja moyo! hutofika popote pale.!