Filipo Lubua
JF-Expert Member
- Nov 18, 2011
- 339
- 578
Baada ya maamuzi yaliyofanywa na Kamati Kuu ya Chadema hapo juzi, tumeuona utetezi walioutoa Zitto Kabwe na Kitila. Kuna mambo kadhaa ambayo nimeyaona yanahitaji kupewa umaanani kwa tahadhari kubwa sana. Kwanza niseme kuwa, kama waraka ulioitwa Waraka wa siri ndio uliotumiwa kumvua Zitto madaraka, basi Zitto hakutendewa haki maana waraka, kama wengi mlivyousoma, haukuonyesha kumshirikisha Zitto, angaau kwa hatua ile. Ila, kama alivyoeleza Zitto, kama amevuliwa madaraka kwa sababu zile alizozitaja, zile za kutoshirikiana na viongozi wnenzake wakuu, basi hukumu hiyo ni ya haki maana Zitto amekuwa akifanya siasa za ubnafsi, za kukijengea chama makundi na kujijenga yeye binafsi. Hizo ni siasa chafu na mtu wa namna hiyo hafai.
Sasa, tahadhari kwa Chadema ni hii: Ni dhahiri kuwa kumwajibisha Zitto Kabwe ulikuwa ni uamuzi mzuri ambao binafsi nilikuwa niiusubiria kwa muda mrefu. Lakini, kama mlivyomsikia Zitto na Mkumbo, wameamua kuitumia nafasi hiyo kwa kuzisaka huruma za wananchi na wapenzi wa Chadema, na wameamua kuitumia nafasi hiyo kujijenga zaidi kisiasa na mwisho kutekeleza tamaa zao. Ndio maana, licha ya Mkumbo kushirikiana na Mwigamba kuandaa waraka huo, waliona hawana haja ya kumshirikisha katika press conference, na waliamua hata kutomzungumzia. Kwa ujumla wamemtupia kapuni na wameamua kujipambanua wao wenyewe kama maswahiba, wanaojijenga kwa pamoja kisiasa.
Ni dhahiri kuwa, hatua hii ya awali ya Kamati Kuu ndiyo ilikuwa hatua muhimu katika kukiokoa Chama na kuyaweka hai matumaini ya Watanzania ya kuing'oa CCM mwaka 2015. Lakini, ni vyema mkaelewa pia, hatua hii muhimu yaweza ikawa ni chanzo ya maporomoko makubwa zaidi kwa Chadema kama haitasaidia kumfungia Zitto Kabwe na Kitila Mkumbo Speed Governor. Hili ni kwa sababu, sasa wamejipambanua kama wapigania haki ndani ya chama (na si wapigania vyeo, kama walivyo) na sasa watakihujumu chama waziwazi katika majukwaa ya chama, kwa hoja ya uhuru wa kidemokrasia. Wanajua kuwa, wameshafanikiwa kuwafanya wananchi wawaone kuwa wanaonewa na uongozi wa Chadema; linalofuata sasa, watafanya hujuma nyingi za wazi dhidi ya uongozi, kwa sababu wanajua watu wameshawachukuliwa kama waonewa kwenye chama.
Ni kweli kuwa, bado chama hakijafikia hitimisho ya swala hili maana kimewapa watu hawa siku 14 wajitetee. Mkumbuke kuwa, wasaliti wana nguvu zaidi wakiwa ndani ya chama kuliko wawapo nje. Kama kweli Zitto amekuwa akitumiwa na CCM, basi kwa hao CCM kutakuwa na ushindi bado, ikiwa Zitto ataendelea kuwa ndani ya Chadema. CCM wanamhitaji Zitto akiwa ndani ya Chadema, maana wanajua hawana uwezo kuivuruga Chadema bila mamluki wao ndani ya Chadema. Ikiwezekana, chama kichukue hatua zaidi mapema ili kuhakikisha tunaondoa unafki huu mapema. Mkichelewa, Zitto na Kitila wataibua matatizo mengine makubwa karibu zaidi na uchaguzi Mkuu wa 2015 na hilo litakuwa na athari kubwa zaidi kwenye chama. Sisi tulio wanachama wa Chadema na waathirika wa siasa za CCM, tutaumia sana pale Zitto atakapotumika kukibomoa chama zaidi, hasa karibu na Uchaguzi Mkuu 2015. Chukueni tahadhari, Zitto asije akafifisha ndoto zetu za kuing'oa CCM.
Na nyinyi viongozi wakuu, onyesheni ukomavu wenu kwa kufanya na kuikuza demokrasia ndani ya Chama. Tunahitaji uhuru wa maoni (sio ule wa siri wa akina Mkumbo) uendelezwe chamani. Watu wawe huru kutoa maoni yao. Narudia, NI VYEMA ZITTO KABWE ACHUKULIWE HATUA ZAIDI, BILA KUJALI KUTAKUWA NA ATHARI GANI KWA SASA. NI VYEMA TUPATE MPASUKO MKUBWA SASA, KULIKO KUSUBIRI MPASUKO AWEZAO KUULETA SIKU CHACHE KABLA YA UCHAGUZI MKUU.
Sasa, tahadhari kwa Chadema ni hii: Ni dhahiri kuwa kumwajibisha Zitto Kabwe ulikuwa ni uamuzi mzuri ambao binafsi nilikuwa niiusubiria kwa muda mrefu. Lakini, kama mlivyomsikia Zitto na Mkumbo, wameamua kuitumia nafasi hiyo kwa kuzisaka huruma za wananchi na wapenzi wa Chadema, na wameamua kuitumia nafasi hiyo kujijenga zaidi kisiasa na mwisho kutekeleza tamaa zao. Ndio maana, licha ya Mkumbo kushirikiana na Mwigamba kuandaa waraka huo, waliona hawana haja ya kumshirikisha katika press conference, na waliamua hata kutomzungumzia. Kwa ujumla wamemtupia kapuni na wameamua kujipambanua wao wenyewe kama maswahiba, wanaojijenga kwa pamoja kisiasa.
Ni dhahiri kuwa, hatua hii ya awali ya Kamati Kuu ndiyo ilikuwa hatua muhimu katika kukiokoa Chama na kuyaweka hai matumaini ya Watanzania ya kuing'oa CCM mwaka 2015. Lakini, ni vyema mkaelewa pia, hatua hii muhimu yaweza ikawa ni chanzo ya maporomoko makubwa zaidi kwa Chadema kama haitasaidia kumfungia Zitto Kabwe na Kitila Mkumbo Speed Governor. Hili ni kwa sababu, sasa wamejipambanua kama wapigania haki ndani ya chama (na si wapigania vyeo, kama walivyo) na sasa watakihujumu chama waziwazi katika majukwaa ya chama, kwa hoja ya uhuru wa kidemokrasia. Wanajua kuwa, wameshafanikiwa kuwafanya wananchi wawaone kuwa wanaonewa na uongozi wa Chadema; linalofuata sasa, watafanya hujuma nyingi za wazi dhidi ya uongozi, kwa sababu wanajua watu wameshawachukuliwa kama waonewa kwenye chama.
Ni kweli kuwa, bado chama hakijafikia hitimisho ya swala hili maana kimewapa watu hawa siku 14 wajitetee. Mkumbuke kuwa, wasaliti wana nguvu zaidi wakiwa ndani ya chama kuliko wawapo nje. Kama kweli Zitto amekuwa akitumiwa na CCM, basi kwa hao CCM kutakuwa na ushindi bado, ikiwa Zitto ataendelea kuwa ndani ya Chadema. CCM wanamhitaji Zitto akiwa ndani ya Chadema, maana wanajua hawana uwezo kuivuruga Chadema bila mamluki wao ndani ya Chadema. Ikiwezekana, chama kichukue hatua zaidi mapema ili kuhakikisha tunaondoa unafki huu mapema. Mkichelewa, Zitto na Kitila wataibua matatizo mengine makubwa karibu zaidi na uchaguzi Mkuu wa 2015 na hilo litakuwa na athari kubwa zaidi kwenye chama. Sisi tulio wanachama wa Chadema na waathirika wa siasa za CCM, tutaumia sana pale Zitto atakapotumika kukibomoa chama zaidi, hasa karibu na Uchaguzi Mkuu 2015. Chukueni tahadhari, Zitto asije akafifisha ndoto zetu za kuing'oa CCM.
Na nyinyi viongozi wakuu, onyesheni ukomavu wenu kwa kufanya na kuikuza demokrasia ndani ya Chama. Tunahitaji uhuru wa maoni (sio ule wa siri wa akina Mkumbo) uendelezwe chamani. Watu wawe huru kutoa maoni yao. Narudia, NI VYEMA ZITTO KABWE ACHUKULIWE HATUA ZAIDI, BILA KUJALI KUTAKUWA NA ATHARI GANI KWA SASA. NI VYEMA TUPATE MPASUKO MKUBWA SASA, KULIKO KUSUBIRI MPASUKO AWEZAO KUULETA SIKU CHACHE KABLA YA UCHAGUZI MKUU.