TAHADHARI: Hali ya bahari imechafuka.

TAHADHARI: Hali ya bahari imechafuka.

mbalila

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2013
Posts
824
Reaction score
161
Kwa wale waliopanga kwenda ufukweni leo kama siyo lazima unaweza kuahilisha.

Nimepita barabara ya Obama asubuhi hii maji yanapiga kingo za bahari mpaka yanavuka na kugonga kwenye gari zinazo pita barabarani, Panton kubwa inapata shida kupaki kwa mwimbi ni makubwa sana.

ASANTENI
 
Kwa wale waliopanga kwenda ufukweni leo kama siyo lazima unaweza kuahilisha.

Nimepita barabara ya Obama asubuhi hii maji yanapiga kingo za bahari mpaka yanavuka na kugonga kwenye gari zinazo pita barabarani, Panton kubwa inapata shida kupaki kwa mwimbi ni makubwa sana.

ASANTENI

Ahsante sana. Sijasikia kutoka kwenye mamlaka zetu kusema chochote? Mpaka maafa? Dah
 
Asante kwa habari nzuri na ya kuelimisha jamii.Tuige mfano huu sio kushabikia umbea tu.
 
Asante Mpwa barikiwa sana kama ulikuwa na mpango WA kwenda kugegeda baharini au ufukweni nakusihi usiebde
 
Asante Mpwa barikiwa sana kama ulikuwa na mpango WA kwenda kugegeda baharini au ufukweni nakusihi usiende
 
Nilipita maeneo hayo jana jion,maji yalikuja mengi kutoka baharin yakarukia gari kwa kiasi kikubwa sana...i waz real shocked!!! Cha ajabu watu walikuwa wengi tu maeneo hayo wanakula maisha.Mimi njia ile sijawah pita,jana ndo mara ya kwanza nikadhan ni kawaida.Bado nashangaa wale watu ambao niliwaona,hawaogopi?? Sometimes tunailaumu serikali kwa ujinga wetu,hali kama ile kweli mtu unaendelea kukaa tu hadi uambiwe jaman!!! WaTz tubadilike jaman.
 
Kwa wale waliopanga kwenda ufukweni leo kama siyo lazima unaweza kuahilisha. Nimepita barabara ya Obama asubuhi hii maji yanapiga kingo za bahari mpaka yanavuka na kugonga kwenye gari zinazo pita barabarani, Panton kubwa inapata shida kupaki kwa mwimbi ni makubwa sana. ASANTENI
Asante lakini hilo neno kuahilisha hapo juu nimejaribu kuwauliza zaidi ya watu 10 wakasema hata wao hawajawahi kulisikia. Unaweza kutufafanulia lina maana gani.
 
Nilipita maeneo hayo jana jion,maji yalikuja mengi kutoka baharin yakarukia gari kwa kiasi kikubwa sana...i waz real shocked!!! Cha ajabu watu walikuwa wengi tu maeneo hayo wanakula maisha.Mimi njia ile sijawah pita,jana ndo mara ya kwanza nikadhan ni kawaida.Bado nashangaa wale watu ambao niliwaona,hawaogopi?? Sometimes tunailaumu serikali kwa ujinga wetu,hali kama ile kweli mtu unaendelea kukaa tu hadi uambiwe jaman!!! WaTz tubadilike jaman.

Usiogope sana hiyo ni hali ya kawaida, cha muhimu ni wale wanaofanya kazi ndani ya bahari hasa wavuvi wenye vyombo vidogo kutokwenda bahari sku hiyo, otherwise wapita njia na watu wanaoishi na kufanya biashara ufukweni wangekuwa wanakimbia nyumba zao kila siku!
 
Ahsante sana. Sijasikia kutoka kwenye mamlaka zetu kusema chochote? Mpaka maafa? Dah

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA UCHUKUZI
MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA


Simu: 255 22 2460735/2460706
FAKSI: 255 22 2460735/2460700 S.L.P. 3056
Barua pepe: met@meteo.go.tz DAR ES SALAAM
Tovuti: Tanzania Meteorological Agency - Admin -

Unapojibu tafadhali nakili:
Kumb. Na.: TMA/1622 02 Januari, 2014

Taarifa kwa umma: Upepo mkali pamoja na mawimbi makubwa vinatarajiwa
katika maeneo yote ya ukanda wa pwani.

Taarifa Na. 201401-01
Muda wa Kutolewa
Saa za Afrika Mashariki
Saa 4 Asubuhi
Daraja la Taarifa: Tahadhari
Kuanzia:
Tarehe
03 Januari, 2014
Mpaka:
Tarehe
05 Januari, 2014
Aina ya Tukio Linalotarajiwa
Hali ya Upepo mkali unaozidi kilomita 40 kwa saa pamoja na
mawimbi makubwa zaidi ya mita 2.0 inatarajiwa katika ukanda
wote wa pwani.
Kiwango cha uhakika: Wastani (60%)
Maeneo yatakayoathirika
Pwani ya mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani, Lindi, Mtwara
pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba.
Maelezo:
Hali hii inatokana na kuimarika kwa mfumo wa mgandamizo mdogo
wa hewa katika Bahari ya Hindi, kusini mashariki mwa kisiwa cha
Madagascar. Mfumo huu unatarajiwa kusababisha kuvuma kwa upepo
mkali kutoka pwani ya Somalia kuelekea pwani kusini .
Angalizo:
Wakazi wa maeneo yaliyotajwa (hatarishi) wanashauriwa kuchukua
tahadhari.
Maelezo ya Ziada
Mamlaka ya Hali ya Hewa inaendelea kufuatilia hali hii na itatoa
mrejeo pale itakapobidi.

Imetolewa na
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania.
 
Back
Top Bottom