Tafakuri yakinifu kuhusu wagombea urais

Tafakuri yakinifu kuhusu wagombea urais

budget

Member
Joined
Feb 23, 2015
Posts
42
Reaction score
27
TAFAKURI YAKINIFU KUHUSU WAGOMBEA

*Tuwapime Wagombea Kwa Utashi Wao Kisiasa Katika Mawanda Mapana Ya Kutangaza Kwao Nia, Kuchukua Fomu Na Kutafuta Udhamini


BERNARD KAMILLIUS MEMBE

Membe sio Mwanasiasa mzuri na hana muda mrefu wa utumishi ndani ya Chama Cha Mapinduzi kadi yake Ya kwanza ya CCM ameipata Mwaka 2003 jambo ambalo linampelekea kupoteza sifa ya kuwa Mwenyekiti wa chama kwa kukosa uzoefu ndani ya chama



Kuanzia Mwaka 2003~2012 hakuwahi Kuwa Kiongozi ndani ya Chama kupitia Uchaguzi, hakuwahi kuwa Mwenyekiti,katibu au Mjumbe Wa Nafasi yoyote wa Kugombe na kuchaguliwa ila amekuwa mjumbe wa Kamati ya Siasa baada ya kuchaguliwa kuwa Mbunge hadi 2012,Nec ndio nafasi yake Ya Kwanza ya Kuchaguliwa kama Kiongozi wa Chama hata ivyo aliponea katika nafasi ndogo Kukosa nafasi ya nec na kama si busara na mbeleko za meza basi Ingekuwa historia, ikumbukwe katika uchaguzi huo membe alishindwa mpaka na dr Fenela mkangala,January makamba,mwigulu wasira na wengine hii ilitokana na membe kukosa uzoefu na chaguzi za ccm na kutokukijua chama



Hivyo kwa namna hiyo huwezi kumpa Chama mtu ambaye sio Familia na Chama Cha Mapinduzi na hajui namna Ya kuongoza Chama anahitaji kupata Nafasi zaidi ya kupata Uzoefu ndani ya Chama


HOTUBA YAKE AKITANGAZA NIA

sehemu Kubwa Ya Hotuba Yake Imejikita Kuonyesha Uzoefu wake Katika Kushughulikia Migogoro na Kumaliza Matatizo Yanayozikabili Nchi Jirani,lakini Akasahau Kuwa Amiri Jeshi Mkuu Na Kuiongoza Taasisi Nyeti Kama Ikulu Ni Zaidi Ya Mahusiano Ya Kimataifa, Membe Kama Mtia Nia Hakuonyesha Vipaumbele Vyake Hotuba Yake Ilijaa Mbwebwe Mathalani Kuhitaji Huruma Kupitia Kaburi La Mwalimu Nyerere Ameonyesha Kutokujiamini Katika Mchakato Huu


KUCHUKUA FOMU

Akichukua Fomu Pia Membe Hakuonyesha Kama Mtu Mwenye Dhamira Ya Dhati Na Kweli Katika Mchakato Huu Wa Kugombea Kupitishwa Na Chama, hii Yawezekana ni Kutokana Na Kutokujiamini Kwake Hata Mbinu Zake Za Kuchelewa Kutangaza Nia nia Na Kuchukua Fomu Zinaonyesha Zaidi Jinsi Mabovyo Hakujipanga Na Anatumia Mikakati Ya Kuwatoa Mhanga Wengine Ili Yeye Kufanikiwa


KUTAFUTA WADHAMINI

katika Zoezi Hili Membe Ameonyesha Kupoteza Mwelekeo Katika Mchakato Huu Baada Ya Kuanza Kutafuta Wadhamini Huku Akionyesha anawasiwasi Wa Kutopita Ni Kama Mtu Anayejua Kesho Yake Kusuasua Kwake Na Matamshi Yake Yanadhihirisha Ni Mtu Anayesuburi Miujiza, Akiwa Mkoani Mbeya Alisema Endapo Atakatwa Jina Atamuunga Mkono Mwandosya Hii Inadhihirisha Membe Hana uwakika Katika Mbio Zake.

Huyu Ndie Membe Mgombea anayesaka Nafasi Kupitishwa Kupitia Ccm

Itaendelea Na Wengine.........
Mpiganaji
 
Membe alikuwa akivurunda Nchi za Nje Mahinga a.k.a POSH BoY anamsaidia ....
 
Membe hana sifa ya kuwa mwenyekiti wa CCM na 95% ya wanec na wajumbe wa cc na mkutano mkuu washasema hawapo tayari kuongozwa na mtu asiyekijua Chama vizuri
 
na yule ambaye alishindwa kupanda jukwaani na akashindwa kushika microfon.muda wote anatoa kauli za kumuogopa Mangula kwambaa,kelele zenu zisijekumpa Mangula sababu ya kuniadhibu.Hutu aliyeahid kuongelea Richard Wa monduli na hakutekeleza.
 
Kama utaendelea na uchambuzi unaonesha wewe ni mtu makini ila hoja moja hujaisema
 
Membe ameshasema akishindwa atamuunga mkono Mwandosya?watu 3 wanatakiwa kuondolewa kwenye nafasi za kugombea kupitia ccm.
1-Lowasa
2-Membe
3-Pinda
Hao watu wana makundi makubwa sana ndani ya ccm.
 
na yule ambaye alishindwa kupanda jukwaani na akashindwa kushika microfon.muda wote anatoa kauli za kumuogopa Mangula kwambaa,kelele zenu zisijekumpa Mangula sababu ya kuniadhibu.Hutu aliyeahid kuongelea Richard Wa monduli na hakutekeleza.
Kwa nini anamwogopa Mangula?
 
Membe hana sifa ya kuwa mwenyekiti wa CCM na 95% ya wanec na wajumbe wa cc na mkutano mkuu washasema hawapo tayari kuongozwa na mtu asiyekijua Chama vizuri

Lowasa na Membe wanalingana hafai wote.
 
Hebu tuletee ya mkulima wa kigoma.

Naamini hatuhitaji sabuni kumsafisha
 
Kwa nini anamwogopa Mangula?

hata mimi nilishangaaa sana ,Ina maana chama ni Mangula tu kwa mtazamo wake au labda wengine wote ni wala rushwa na wezi kama yeye hvyo anajua udhaifu wao,Rejea, salaamu toka kuzimu by Ben r mtobwa rip
 
Membe ameshasema akishindwa atamuunga mkono Mwandosya?watu 3 wanatakiwa kuondolewa kwenye nafasi za kugombea kupitia ccm.
1-Lowasa
2-Membe
3-Pinda
Hao watu wana makundi makubwa sana ndani ya ccm.

akili za kuambiwa na pole pole changanya na zako kua kwenye chama tu teyari ni kundi na uchaguzi ni kundi ndio maana wanasema wengi wape hakuna wa kukatwa acha democrasia ifanye kazi
 
Naomba nichangie kidogo kuhusu watia nia wa ccm ambao tayari wamechukua form.Ukiangalia na kuchambua kwa umakini hotuba za watia nia wa ccm,Wengi wao walitoa ahadi tu na kwa kiwango kikubwa hawakuonyesha kwamba wanazitambua matatizo yanayowakabili watanzania.Kwa mfano:Matatizo yanayowakabili watanzania yanaweza kuanishwa kwa kuangalia maeneo kama,Matatizo yanayotokana na sera mbovu,Matatizo yanayotokana na sheria mbovu na matatizo yanayotokana na usimamizi mbovu.Ni watia nia kama wawili hivi ndio kidogo walijaribu kuanisha matatizo hayo,..Lakini kwa kiwango kidogo sana.Mara nyingi walitoka kwenye mstari na kuongelea mpango kazi badala ya uchambuzi yakinifu.Miongoni mwa watia nia hao alikuwa january makamba na mwigulu nchemba,Lakini hata wao walikuwa wanatoka kwenye mstari na kuongelea mpango kazi badala ya uchambuzi yakinifu.Ni vyema watia nia wanapotoa hotuba zao,wajikite katika uchambuzi ili waeleweke.Mathalan;Tatizo la ajira..Je,limesababishwa na nini(sera mbovu za ajira au sheria mbovu za ajira au usimamizi mbovu wa wizara husika?.Baada ya hapo mtia nia aanishe je akichaguliwa atarekebisha sheria hizo,atabadilisha sera ya ajira au atasimamia utekelezaji huo kwa umakini.Baada ya hapo mtia nia ni vyema akatuambia je,Kutokana na hilo, Atazalisha ajira kwa kiasi gani. Kama watia nia watajikita katika maeneo hayo,Itatufanya sisi wananchi tupate nafasi ya kuwachambua na mwisho wa siku tutaanza kuunga hoja za watia nia badala ya sasa ambapo kila mtu anamuunga mkono kwa pesa yake,sura yake,elimu yake,utumishi wake serikalini,udini,ukanda,undugu nk....
 
Back
Top Bottom