Tafakuri ya Wasiojulikana

vasilius

Member
Feb 28, 2017
10
17
Hivi mpaka leo kuna mtu anajifanya hawafahamu hao wanaoitwa "WASIOJULIKANA"? Mimi nafikiri ni sifa tu watu wameamua kuwapa. Ukweli ni kwamba wanajulikana kwa sababu ya tabia za kuogopa binadamu wenzetu kuliko aliyetuumba basi tumeamua wawe hawajulikani hata kama wanajulikana.

Katika jambo linaloniumiza kichwa sana ni binadamu kama wewe kucheza na uhai wako kama vile anacheza na mpira wa kitenisi. Yaani mtu unaweza kukatika mguu binadamu akakutengenezea mguu wa bandia. Ikawa huna nywele kichwani ukavaa wigi. Afya ikadorora au ukaumwa ukatumia dawa. Lakini uhai wa binadamu ukiondoka ndio basi hakuna kiumbe yoyote au kiumbe yoyote hapa duniani anaweza kukurudishia uhai wako. Hivi inakuwaje mtu anathubutu kuutishia uhai wenu au kukutoeni uhai, wa kwanza, wa pili, wa tatu, ... bado tupo tupo tu km vile kuku kachinjwa huyu kesho atachinjwa mwingine na bado tupo tupo.

Kwangu mimi watu hawa wakija kuna option 3 tu.
1. Waondoke na mimi nikiwa maiti, hapo waliponikuta hawawezi kuondoka na mimi nikiwa mzima hata siku moja.
2. Wabaki wao wakiwa maiti, au
3. Waondoke wao wakiwa wazima au wamejeruhiwa na kuniacha mimi mzima au nimejeruhiwa.

Nasema hivi kwa sababu sheria za polisi zipo wazi kabisa za ukamataji. Ukamataji usiofata taratibu kwa sasa ni kuendelea kuwalinda hao wanaitwa "WASIOJULIKANA". Hivi inakuwaje jeshi la polisi linashawishi watu kufuata sheria bila shuruti wakati wao ndio wa kwanza kutofuata taratibu zao wenyewe hasa za ukamataji. Hivi kweli unaniambia kuanzia sasa upo chini ya ulinzi nakuuliza kwa kosa gani unanijibu kosa utalijulia kituoni sasa umeja kunikamatia nini? Kama unasema kosa nitalijulia kituoni wewe umekuja kufanya nini si ungenipigia simu au kunipa taarifa nikaja huko kituoni halafu nikajua hilo kosa langu.

Unajua sisi binadamu wakati mwingine ni wajinga sana. Unakuta mtu anafurahia mwenzake kutekwa na kuuwawa au kuteswa kana kwamba yeye hatakufa. Wakati mwingine ni bora huyo anaepata mateso kwa kupigania haki yake kuliko wewe uwe kitandani unateseka kwa UKIMWI tu ambapo ungeweza kuuzuia kwa kutumia kondom ya bure. Pamoja na elimu yote iliyotolewa ya kujikinga na maradhi hayo bado kwa ujinga wa kutojitambua unauvaa lkn haraka kufurahia wenzako kupata mateso na kufa.

Pamoja na wengi kutoa sababu mbalimbali kwa nini watu wanatekwa. Fikra yangu mimi inaona kwamba hawa watu wanataka sisi tuwe hivi:-
1. Tuzoee hii hali ya watu kutekwa tuone ni kitu cha kawaida, wao waamue wakurudishe hai, majeruhi au umekufa. Ndio maana jeshi la polisi kila mara linasisitiza mtu akitekwa tusikimbilie kusema hivyo. Maanake ni kwamba mtu atekwe tukae kimya.
2. Tusijali na kuuthamini uhai wetu kama ambavyo hawauthamini. Yaani wanatuona sisi ni kuku tu wanaweza kutufanya kitoweo muda wowote pale wanapotaka.
3. Wanataka kutupangia nini cha kuongea na nini usiongee, nini cha kufanya na nini usifanye hata kama ni sheria. Yaani kwa kifupi wao ndio iwe sheria wanapanga wao kila kitu. Hivi hawajui zama za utumwa zimeshaisha?
4. Tusiwe na uthubutu na ujasiri wa kudai haki yako yoyote ile.
5. Kutia watu hofu kuelekea kwenye uchaguzi wa 2020 na nyinginezo. Kwa hili uwe mgombea au iwe umejitayarisha kwenda kumchagua mtu ambae wao hawamtaki.

Je wewe una tafakuri gani?
 
Maelezo mengi ila utumbo mtupu ,unakamatwa na polisi wanajitambulisha na wanakuja na gari ya serkali harafu unasema ametekwa ,

Nyambafu


USSR

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maelezo mengi ila utumbo mtupu ,unakamatwa na polisi wanajitambulisha na wanakuja na gari ya serkali harafu unasema ametekwa ,

Nyambafu


USSR

Sent using Jamii Forums mobile app

Haya mambo kwa mtu kama wewe huwezi kudadavua unachoweza ni kutukana tu. Hivi mtu lugha yako ya taifa unashindwa kuandika vizuri, unashindwa kutofautisha kati ya 'r' na 'l' katika maandishi utaweza kupambanua mambo kama haya. Kwanza toka huko katika hoja za matusi halafu ujifunze kuandika vizuri.

Baada ya hapo ujifunze kusoma hoja vizuri uielewe ndio uchangie. Hivi kuna sehemu nimeandika polisi hata wakijitambulisha na kuja na gari la serikali uendelee kugoma au isemwe umetekwa?

Yaani wewe unafikiri mtu kusema tu mimi ni mtu wa usalama basi inatosha hiyo kuwa utambulisho na gari aliyokuja nayo ina private namba?
 
Ile ni kazi kama kazi nyingine ni kama doctor anavyosomea kukupasua tumbo au popote pale katika mwili wako hivyo nao ni kitengo maalum cha kazi hizo tena unafanya kazi kwa furaha kabisa au usipoifanya unajisikia vibaya kabisa
 
Ile ni kazi kama kazi nyingine ni kama doctor anavyosomea kukupasua tumbo au popote pale katika mwili wako hivyo nao ni kitengo maalum cha kazi hizo tena unafanya kazi kwa furaha kabisa au usipoifanya unajisikia vibaya kabisa
Kila kazi ina taratibu zake na sheria zake. Sijajua unamaanisha kazi ipi? Ila kama kazi ya utekaji basi sikubaliani na wewe kama ni kazi kama kazi nyingine. Ila kama unamaanisha jeshi la polisi nakubaliana na wewe ile ni kazi kama kazi nyingine. Ninavyojua bila shaka pamoja na majukumu mingine lakini kazi kuu ya jeshi la polisi ni kulinda raia na mali zao. Kama wao wanahusika kuteka au kuwalinda wanaoteka watu basi hilo silo jukumu lao lililoanishwa katika katiba na PGO. Siamini wala sikubaliani kwamba jeshi la polisi linahusika katika utekaji ila matendo yao ndio yanayotia shaka katika hawa wanaoitwa WASIOJULIKANA.
 
Kila kazi ina taratibu zake na sheria zake. Sijajua unamaanisha kazi ipi? Ila kama kazi ya utekaji basi sikubaliani na wewe kama ni kazi kama kazi nyingine. Ila kama unamaanisha jeshi la polisi nakubaliana na wewe ile ni kazi kama kazi nyingine. Ninavyojua bila shaka pamoja na majukumu mingine lakini kazi kuu ya jeshi la polisi ni kulinda raia na mali zao. Kama wao wanahusika kuteka au kuwalinda wanaoteka watu basi hilo silo jukumu lao lililoanishwa katika katiba na PGO. Siamini wala sikubaliani kwamba jeshi la polisi linahusika katika utekaji ila matendo yao ndio yanayotia shaka katika hawa wanaoitwa WASIOJULIKANA.
Aisee....!! Lakini umemwelewa vizuri wa stendi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi mpaka leo kuna mtu anajifanya hawafahamu hao wanaoitwa "WASIOJULIKANA"?
Je wewe una tafakuri gani?
Sisi wengine tuliisha watafakari kitambo
P
 
Hivi mpaka leo kuna mtu anajifanya hawafahamu hao wanaoitwa "WASIOJULIKANA"? Mimi nafikiri ni sifa tu watu wameamua kuwapa. Ukweli ni kwamba wanajulikana kwa sababu ya tabia za kuogopa binadamu wenzetu kuliko aliyetuumba basi tumeamua wawe hawajulikani hata kama wanajulikana.

Katika jambo linaloniumiza kichwa sana ni binadamu kama wewe kucheza na uhai wako kama vile anacheza na mpira wa kitenisi. Yaani mtu unaweza kukatika mguu binadamu akakutengenezea mguu wa bandia. Ikawa huna nywele kichwani ukavaa wigi. Afya ikadorora au ukaumwa ukatumia dawa. Lakini uhai wa binadamu ukiondoka ndio basi hakuna kiumbe yoyote au kiumbe yoyote hapa duniani anaweza kukurudishia uhai wako. Hivi inakuwaje mtu anathubutu kuutishia uhai wenu au kukutoeni uhai, wa kwanza, wa pili, wa tatu, ... bado tupo tupo tu km vile kuku kachinjwa huyu kesho atachinjwa mwingine na bado tupo tupo.

Kwangu mimi watu hawa wakija kuna option 3 tu.
1. Waondoke na mimi nikiwa maiti, hapo waliponikuta hawawezi kuondoka na mimi nikiwa mzima hata siku moja.
2. Wabaki wao wakiwa maiti, au
3. Waondoke wao wakiwa wazima au wamejeruhiwa na kuniacha mimi mzima au nimejeruhiwa.

Nasema hivi kwa sababu sheria za polisi zipo wazi kabisa za ukamataji. Ukamataji usiofata taratibu kwa sasa ni kuendelea kuwalinda hao wanaitwa "WASIOJULIKANA". Hivi inakuwaje jeshi la polisi linashawishi watu kufuata sheria bila shuruti wakati wao ndio wa kwanza kutofuata taratibu zao wenyewe hasa za ukamataji. Hivi kweli unaniambia kuanzia sasa upo chini ya ulinzi nakuuliza kwa kosa gani unanijibu kosa utalijulia kituoni sasa umeja kunikamatia nini? Kama unasema kosa nitalijulia kituoni wewe umekuja kufanya nini si ungenipigia simu au kunipa taarifa nikaja huko kituoni halafu nikajua hilo kosa langu.

Unajua sisi binadamu wakati mwingine ni wajinga sana. Unakuta mtu anafurahia mwenzake kutekwa na kuuwawa au kuteswa kana kwamba yeye hatakufa. Wakati mwingine ni bora huyo anaepata mateso kwa kupigania haki yake kuliko wewe uwe kitandani unateseka kwa UKIMWI tu ambapo ungeweza kuuzuia kwa kutumia kondom ya bure. Pamoja na elimu yote iliyotolewa ya kujikinga na maradhi hayo bado kwa ujinga wa kutojitambua unauvaa lkn haraka kufurahia wenzako kupata mateso na kufa.

Pamoja na wengi kutoa sababu mbalimbali kwa nini watu wanatekwa. Fikra yangu mimi inaona kwamba hawa watu wanataka sisi tuwe hivi:-
1. Tuzoee hii hali ya watu kutekwa tuone ni kitu cha kawaida, wao waamue wakurudishe hai, majeruhi au umekufa. Ndio maana jeshi la polisi kila mara linasisitiza mtu akitekwa tusikimbilie kusema hivyo. Maanake ni kwamba mtu atekwe tukae kimya.
2. Tusijali na kuuthamini uhai wetu kama ambavyo hawauthamini. Yaani wanatuona sisi ni kuku tu wanaweza kutufanya kitoweo muda wowote pale wanapotaka.
3. Wanataka kutupangia nini cha kuongea na nini usiongee, nini cha kufanya na nini usifanye hata kama ni sheria. Yaani kwa kifupi wao ndio iwe sheria wanapanga wao kila kitu. Hivi hawajui zama za utumwa zimeshaisha?
4. Tusiwe na uthubutu na ujasiri wa kudai haki yako yoyote ile.
5. Kutia watu hofu kuelekea kwenye uchaguzi wa 2020 na nyinginezo. Kwa hili uwe mgombea au iwe umejitayarisha kwenda kumchagua mtu ambae wao hawamtaki.

Je wewe una tafakuri gani?
Umesema ukweli maana wanajulikana ila hawataki wajulikane ili wafanye kazi wanazotumwa na msihoji uwajibikaji wa walinzi wa wananchi na Mali zao.
Hawa wenzetu wanafikiri Watanzania ni wajinga,IPO siku watakunywa Sumu wanayoikoroga na kuipika sasa.Nahofia nyasi ndiyo zitazoumia,nahisi ndiyo maana bado hapajawa na Shari.Lakini haya yakiendelea,hakuna aliyesalama.
 
Ile ni kazi kama kazi nyingine ni kama doctor anavyosomea kukupasua tumbo au popote pale katika mwili wako hivyo nao ni kitengo maalum cha kazi hizo tena unafanya kazi kwa furaha kabisa au usipoifanya unajisikia vibaya kabisa
Ndio maana mpka leo bado upo stand hujatoka
 
Sisi wengine tuliisha watafakari kitambo
P
Nimekupata sana kaka. Andiko lako linafikirisha sana, bahati mbaya sikupata kulisoma hapo kabla. Andiko lako linaleta tafakuri nyingine HIVI VYOMBO VYETU VYA USALAMA VIPO KWA AJILI YA TANZANIA AU WATU (au chama) MAALUM? Kwa nini nauliza hivyo kwa sababu najiuliza hivi mtu wa CHADEMA akishughulikiwa na wenzake wa CHADEMA hivi vyombo vyetu havina wajibu wa kufanya lolote? Wajibu wao ni upi kwa Watanzania?
 
Nimekupata sana kaka. Andiko lako linafikirisha sana, bahati mbaya sikupata kulisoma hapo kabla. Andiko lako linaleta tafakuri nyingine HIVI VYOMBO VYETU VYA USALAMA VIPO KWA AJILI YA TANZANIA AU WATU (au chama) MAALUM? Kwa nini nauliza hivyo kwa sababu najiuliza hivi mtu wa CHADEMA akishughulikiwa na wenzake wa CHADEMA hivi vyombo vyetu havina wajibu wa kufanya lolote? Wajibu wao ni upi kwa Watanzania?
Vyombo vyetu viko vya aina tatu
Ulinzi wa Taifa-JWTZ chini ya CDF hawa wanalinda nchi na mipaka yetu.
Usalama wa Taifa, TISS chini ya DGTISS hawa wanalinda usalama wa taifa, rais na serikali.
Polisi-:Hawa wanalinda raia na mali zao.
P
 
Back
Top Bottom