Tafadhali Rais Magufuli Kabla Hujateua Waziri Mwingine wa Madini na Nishati

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,768
41,010
Naomba nitoe pendekezo moja kwa Rais Magufuli kabla hajamfikiria au hata kumteua mtu mwingine kushika nafasi ya Waziri Muhongo aliyefukuzwa kazi kufuatia kashfa ya makontena ya michanga yenye madini.

Pendekezo hili si geni kwani nililitoa pia mara baada ya uchaguzi na kabla hajaunda Baraza la Mawaziri. Msingi wa pendekezo hili ni ukweli kuwa Wizara ya Nishati na Madini imekuwa ni sehemu ambayo ni ngumu watu kukaa lakini pia inagusa sana maisha na uchumi wa nchi kiasi kwamba kila inapotikisika au kunapotokea matatizo basi kuna mengine mengi yanaenda nayo. Kufanikiwa kwa nchi yoyote kunategemea sana kati ya mengi ni hili la madini na nishati.

Pendekezo langu ni kuwa ni wakati muafaka kutenganisha Wizara hii katika sehemu zake za kimantiki badala ilivyo sasa ambapo inaonekana wizara mbili zimelazimishwa kukaa pamoja chini ya mtu mmoja. Kila tatizo linapotokea upande mmoja basi upande mwingine nao unaathirika. Kwa mfano, sasa hivi kumetokea matatizo kwenye upande wa Madini na kusababisha Waziri kujiuzulu lakini upande wa Nishati nao unaenda kupoteza Waziri wake. Na hili linakuwa kweli ikiwa kinyume na hata kwa viongozi wengine wa kuu wa Wizara.

Pendekezo langu - na inawezekana wengine pia wamewahi kulitoa - ni kuwa ipo haja ya kuwa na wizara mbili ambazo zitaweza kusimamia vizuri sekta hizi mbili, chini ya Mawaziri wawili tofauti.

Kuwe na WIZARA YA MADINI, GESI NA UTAFUTAJI WA MAFUTA (Ministry of Mining, Gas and Oil Exploration); pale mafuta yatakapothibitika kupatikana na kuweza kuingizwa katika biashara basi wizara itakuwa ni ya Madini, Gesi na Mafuta. Na hii itahusiana na kazi zote za extraction ya madini, gesi na mafuta.

Hii ndio itakuwa ni wizara itakayohusika na masuala yote ya madini, gesi na mambo mafuta kabla raslimali hizo hazijaingizwa katika mifumo au mabadiliko yoyote ambayo yanaweza kusababisha yahame kwenda majukumu ya wizara nyingine.

Wizara ya pili ibakiwa kuwa ni WIZARA YA NISHATI (Ministry of Energy) ambayo kazi yake kubwa ni kusimamia sekta nzima inayohusiana na uzalishaji, usimamizi, usambazaji na matumizi ya nishati.

Lakini pendekezo langu linaenda mbali zaidi ya kutenganisha tu wizara hizi. Kwa wakati huu na kutokana na uzoefu wetu wa muda mrefu kuhusiana na sekta hizi mbili (Nishati na Madini) naamini si hekima, si vizuri, na si sawa kumteua mtu mwingine kusimamia Sekta ya Madini kwa wakati huu hadi pale mambo yatakapowekwa sawa vya kutosha kuweza kuaminiwa mtu mwingine. Tayari wizara hii imehangaika na watu wengi sana huko nyuma na kuendelea kumpa mtu mwingine basi itakuwa ni kuanza kutengeneza bangusilo mwingine huko mbeleni.

Ni kwa sababu hiyo naamini Wizara ya Madini ibakie kama majukumu ya Rais mwenyewe; yaani Magufuli mwenyewe achukue dhamana ya Sekta ya Madini hadi atakapojiridhisha kuwa mifumo, na misingi mizuri ya kusimamia sekta hii imewekwa. Hivyo, napendekeza amteue Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Madini) ambaye ndiye atakuwa msaidizi wake mkubwa wa kusimamia Wizara ya Madini hadi pale atakapoona ni vyema airudishe nje ya Ikulu.

Uamuzi huu unaweza kufanyika hata kwa mwaka mzima au kwa muda wote uliobakia wa awamu hii ya Magufuli. Uzuri wa kufanya hivi, ni kuwa utaondoa ulazima wa Marais kuwatoa makafara mawaziri lakini pia mawaziri kuona kuwa labda wameonewa. Lakini zaidi pia utampa nafasi Rais mwenyewe kuhusika moja kwa moja na hivyo kuweza kujua kwa ukaribu kinachoendeoea na kuchukua hatua mara moja. Wawezekaji na wafanyabiashara wa sekta hii watakuwa na ujasiri wa pekee wa kwenda kujaribu kutoa kitu kidogo Ikulu ili mambo yao yaende na kwa wale tunaomjua Magufuli kuna watu wanaweza wakageuza toka Ikulu wakiwa na pingu!

Kama Rais mwenyewe alivyosema hili ni jambo zito basi ni vizuri alipe uzito unaostahili. Haifai kabisa kumpa mtu mwingine kwa sasa eneo hili.

Sioni namna nyingine ya kuunda upya eneo hili zaidi ya hii.
 
Kama kutolewa kafara Magufuli mwenyewe si msafi hata chembe na kuna ushahidi wa kutosha tu uliothibitishwa na CAG hata ujenzi kafanya madudu mengi tu. Ingekuwa nchi yetu inafuata utawala wa sheria huyu angeshatumbuliwa siku nyingi tu lakini sera za kulindana ndizo zimetufikisha hapa tulipo.
 
Afumue mikataba ya madini na ijadilowe upya bungeni tena kwa uwazi. Mikataba ndo tatzo kubwa sana. Matatzo mnayatengeneza wenyewe mkitatua kidogo mnaanza kujisifu.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
NA MIMI NAPENDEKEZA WIZARA HII IGAWANYWEEE. MAAANA NI KUBWA NA NI NYETI. NAUNGA MKONO KUIGAWA KAMA IFUATAVYOOO;
1. KUWEPO NA WIZARA YA MADI TU PEEKE YAKE,
2. NA WIZARA YA NISHATI TU PEKEE


SASABABU YANGU NI KUTAKA MAJUKUMU YAWE MEPESI.
MUHONGO KWA MAMBO YA NISHATI AMEFANYA VIZURI XAANAA NA ANASTAHILI PONGEZI KUBWA KWANI UMEME UMEFIKA VIJIJI VINGIII.
 
Sijaona Hoja mzee mwanakijiji, wizara ngapi zimekua na mtambuka, ukienda kilimo ndani yake Kuna maji, mifugo. Ukienda uchukuzi ndani yake Kuna Mawasiliano.ishu watu waache kufanya kazi kwa mazoea
 
too late, waziri mpya Alisha andaliwa hata kabla ya kusomwa ripoti.
 
Naunga mkono hoja....ni sahihi na wakati muafaka kufanya hivyo! Akae nayo hata miaka 3 ajaribu kuweka misingi kusimamia madini haya yatupe pesa za maendeleo kwa kasi ili akimaliza 10yrs yake basi tuwe tumeenda mbele kiasi
 
Kama kutolewa kafara Magufuli mwenyewe si msafi hata chembe na kuna ushahidi wa kutosha tu uliothibitishwa na CAG hata ujenzi kafanya madudu mengi tu. Ingekuwa nchi yetu inafuata utawala wa sheria huyu angeshatumbuliwa siku nyingi tu lakini sera za kulindana ndizo zimetufikisha hapa tulipo.
Yaan umesoma habari yote na kupoteza muda wako bure kabisa.
Nje ya Mada
 
Akili yangu inanigomea kuamini kua matatizo haya yanaletwa na kuunganisha hizi wizara na kua moja.

Kuchagua watu wenye viburi, wanaojiona wao ndiyo wao, wasiosikiliza ushauri na huku wakiwa incompetent ndiyo shida iliyopo hapa.

Naona Tushughulike na mzizi.
 
Akili yangu inanigomea kuamini kua matatizo haya yanaletwa na kuunganisha hizi wizara na kua moja.

Kuchagua watu wenye viburi, wanaojiona wao ndiyo wao, wasiosikiliza ushauri na huku wakiwa incompetent ndiyo shida iliyopo hapa.

Naona Tushughulike na mzizi.

Chukulia kwa mfano hizi Wizara ni makampuni makubwa ya sekta mbili tofauti; unafikiri ni sahihi kuwa na CEO mmoja na akafanya vizuri kwa makampuni yote mawili? Yangekuwa ni makampuni yenye kuhusiana mtu anaweza kuona inawezekana ni makampuni ya kazi mbili tofauti kabisa; moja ya magari nyingine ya kompyuta vipi uwe na CEO mmoja?
 
nchi hii hatujielewi mkuu ushauri wako ni bora kwa mustakabali wa nchi tatizo ni pale raisi atakapoifanya sekta ya madini kuwa chini yake wajinga watamuita dikteta!!
 
Chukulia kwa mfano hizi Wizara ni makampuni makubwa ya sekta mbili tofauti; unafikiri ni sahihi kuwa na CEO mmoja na akafanya vizuri kwa makampuni yote mawili? Yangekuwa ni makampuni yenye kuhusiana mtu anaweza kuona inawezekana ni makampuni ya kazi mbili tofauti kabisa; moja ya magari nyingine ya kompyuta vipi uwe na CEO mmoja?
Kwa ninavyojua, Waziri kazi yake ni kuoversee na kusimamia utekelezaji wa sera za wizara, makatibu ndiyo haswa watendaji kazi wanaotakiwa kuripoti kwake.

Kama mtu anashindwa kusimamia hizo sera na mikakati ila akajikita kwenye mipasho na kumridhisha aliyemteua, tutaangalia mwenzetu alipokosea. Mara zote ni pale kwenye majigambo na kuamini hauna mwisho.

Ushauri huu ukisikilizwa kuna siku tutasema na Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo na yenyewe kufeli kwake ni kwakua imerundikiwa kazi.

Kuna kipindi Manji alikua CEO wa Quality Group na ilishughulika na swala zaidi ya moja.
 
Sikiliza mzee Mwanakijiji angalau wewe umejaribu kuja na solution ya kimfumo, lakini tatizo ni kwamba eventually bado unaamini kuwa kuna mtu somewhere yeye pekee ndo anaweza kuisimamia hiyo wizara ya madini na kwamba Tanzania nzima hayupo mtu mwenye uwezo wa kuifanya vyema zaidi.

Lakini hebu fikiria kwa sasa Mambo mengi na yote nyeti ambayo yako chini ya ofisi ya Raisi.

1) Tamisemi
2) Utumishi
3) Utawala bora ( Maadili ya viongozi etc)
4) Usalama wa Taifa

Hayo ni mambo makubwa sana na mazito, sasa kumrundikia tena Raisi " Uwaziri wa Madini" hii inaweza ikapunguza ufanisi. Ni bora basi ukapendekeza Wizara hii ya Madini iwe chini ya Ofisi ya Makamu wa Raisi, kwa sababu mambo ya utafutaji, na uchimbaji wa madini yanarelate sana na Mazingira kitu ambacho kiko chini ya ofisi ya makamu wa Rais.

Kitu kingine ni kwamba, Hii ni nafasi ya kumaliza au kupunguza kwa kiasi kikubwa sintofahamu katika sekta hii ya madini, Mheshimiwa Rais hana budi sasa kutengeneza MFUMO uliotransparent juu ya kila gramu inayochimbwa nchini, mfumo wa kisheria ikiwemo mikataba yenye manufaa kwa nchi, Kuhakikisha tunarenogotiate Terms za Mikataba ya zamani, na pia kuhakikisha Tunawafikisha wote waliotuingiza kwenye mikataba mibovu mahakamani ili sheria ichukue mkondo wake!. Kama Raisi JK aliwafunga kina Yona na Mramba kwa kuitia nchi hasara kwa nini JPM asiwafungulie mashitaka watu wote waliotufikisha hapa bila kujali walihudumu ktk awamu gani?
 
Mkuu Mwanakijiji kwa matatizo tuliyonayo hata rais mwenyewe akiwa waziri wa wizara husika ataondolewa tu kwa tuhuma tena kubwa..!!

Tatizo ni sisi wenyewe...Viongozi wetu, sera na sheria zetu juu ya utajiri tulionao..!
 
Mikataba mingine ya gesi ilipitishwa bungeni jioni mwishoni karibuni bunge linavunjwa unategemea nini
Baada ya kikao kile cha kimagumasheeeee bunge likavunja.

Tujipe muda itasikia siku mtu anakuja kusema tumepata hasara sana. Siasa ni sayansi ngumu kuliko zote hapa duniani
 
Ubinafsi ndio tatizo ..hata wizara igawanywe vipande vitano ..... ....sijui ubinafsi unaweza ondolewa kivipi!
 
Ameanza kusikiliza ushauri wa mitandaoni? Akiwa yeye ndiye msimamizi wa wizara ataweza Kuwajibika pindi akiboronga? Maana hata yeye Ni binadamu na mikataba hii ilitungwa na akiwa Yuko katoka MFUMO.
 
Sikiliza mzee Mwanakijiji angalau wewe umejaribu kuja na solution ya kimfumo, lakini tatizo ni kwamba eventually bado unaamini kuwa kuna mtu somewhere yeye pekee ndo anaweza kuisimamia hiyo wizara ya madini na kwamba Tanzania nzima hayupo mtu mwenye uwezo wa kuifanya vyema zaidi.

Lakini hebu fikiria kwa sasa Mambo mengi na yote nyeti ambayo yako chini ya ofisi ya Raisi.

1) Tamisemi
2) Utumishi
3) Utawala bora ( Maadili ya viongozi etc)
4) Usalama wa Taifa

Hayo ni mambo makubwa sana na mazito, sasa kumrundikia tena Raisi " Uwaziri wa Madini" hii inaweza ikapunguza ufanisi. Ni bora basi ukapendekeza Wizara hii ya Madini iwe chini ya Ofisi ya Makamu wa Raisi, kwa sababu mambo ya utafutaji, na uchimbaji wa madini yanarelate sana na Mazingira kitu ambacho kiko chini ya ofisi ya makamu wa Rais.

Kitu kingine ni kwamba, Hii ni nafasi ya kumaliza au kupunguza kwa kiasi kikubwa sintofahamu katika sekta hii ya madini, Mheshimiwa Rais hana budi sasa kutengeneza MFUMO uliotransparent juu ya kila gramu inayochimbwa nchini, mfumo wa kisheria ikiwemo mikataba yenye manufaa kwa nchi, Kuhakikisha tunarenogotiate Terms za Mikataba ya zamani, na pia kuhakikisha Tunawafikisha wote waliotuingiza kwenye mikataba mibovu mahakamani ili sheria ichukue mkondo wake!. Kama Raisi JK aliwafunga kina Yona na Mramba kwa kuitia nchi hasara kwa nini JPM asiwafungulie mashitaka watu wote waliotufikisha hapa bila kujali walihudumu ktk awamu gani?
Mkuu Sultan/Mfalme wa Brunei ni kiongozi au mtawala wa nchi lakini pia ni waziri wa wizara kadhaa na zinafanya vizuri sana.
 
Naomba nitoe pendekezo moja kwa Rais Magufuli kabla hajamfikiria au hata kumteua mtu mwingine kushika nafasi ya Waziri Muhongo aliyefukuzwa kazi kufuatia kashfa ya makontena ya michanga yenye madini.

Pendekezo hili si geni kwani nililitoa pia mara baada ya uchaguzi na kabla hajaunda Baraza la Mawaziri. Msingi wa pendekezo hili ni ukweli kuwa Wizara ya Nishati na Madini imekuwa ni sehemu ambayo ni ngumu watu kukaa lakini pia inagusa sana maisha na uchumi wa nchi kiasi kwamba kila inapotikisika au kunapotokea matatizo basi kuna mengine mengi yanaenda nayo. Kufanikiwa kwa nchi yoyote kunategemea sana kati ya mengi ni hili la madini na nishati.

Pendekezo langu ni kuwa ni wakati muafaka kutenganisha Wizara hii katika sehemu zake za kimantiki badala ilivyo sasa ambapo inaonekana wizara mbili zimelazimishwa kukaa pamoja chini ya mtu mmoja. Kila tatizo linapotokea upande mmoja basi upande mwingine nao unaathirika. Kwa mfano, sasa hivi kumetokea matatizo kwenye upande wa Madini na kusababisha Waziri kujiuzulu lakini upande wa Nishati nao unaenda kupoteza Waziri wake. Na hili linakuwa kweli ikiwa kinyume na hata kwa viongozi wengine wa kuu wa Wizara.

Pendekezo langu - na inawezekana wengine pia wamewahi kulitoa - ni kuwa ipo haja ya kuwa na wizara mbili ambazo zitaweza kusimamia vizuri sekta hizi mbili, chini ya Mawaziri wawili tofauti.

Kuwe na WIZARA YA MADINI, GESI NA UTAFUTAJI WA MAFUTA (Ministry of Mining, Gas and Oil Exploration); pale mafuta yatakapothibitika kupatikana na kuweza kuingizwa katika biashara basi wizara itakuwa ni ya Madini, Gesi na Mafuta. Na hii itahusiana na kazi zote za extraction ya madini, gesi na mafuta.

Hii ndio itakuwa ni wizara itakayohusika na masuala yote ya madini, gesi na mambo mafuta kabla raslimali hizo hazijaingizwa katika mifumo au mabadiliko yoyote ambayo yanaweza kusababisha yahame kwenda majukumu ya wizara nyingine.

Wizara ya pili ibakiwa kuwa ni WIZARA YA NISHATI (Ministry of Energy) ambayo kazi yake kubwa ni kusimamia sekta nzima inayohusiana na uzalishaji, usimamizi, usambazaji na matumizi ya nishati.

Lakini pendekezo langu linaenda mbali zaidi ya kutenganisha tu wizara hizi. Kwa wakati huu na kutokana na uzoefu wetu wa muda mrefu kuhusiana na sekta hizi mbili (Nishati na Madini) naamini si hekima, si vizuri, na si sawa kumteua mtu mwingine kusimamia Sekta ya Madini kwa wakati huu hadi pale mambo yatakapowekwa sawa vya kutosha kuweza kuaminiwa mtu mwingine. Tayari wizara hii imehangaika na watu wengi sana huko nyuma na kuendelea kumpa mtu mwingine basi itakuwa ni kuanza kutengeneza bangusilo mwingine huko mbeleni.

Ni kwa sababu hiyo naamini Wizara ya Madini ibakie kama majukumu ya Rais mwenyewe; yaani Magufuli mwenyewe achukue dhamana ya Sekta ya Madini hadi atakapojiridhisha kuwa mifumo, na misingi mizuri ya kusimamia sekta hii imewekwa. Hivyo, napendekeza amteue Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Madini) ambaye ndiye atakuwa msaidizi wake mkubwa wa kusimamia Wizara ya Madini hadi pale atakapoona ni vyema airudishe nje ya Ikulu.

Uamuzi huu unaweza kufanyika hata kwa mwaka mzima au kwa muda wote uliobakia wa awamu hii ya Magufuli. Uzuri wa kufanya hivi, ni kuwa utaondoa ulazima wa Marais kuwatoa makafara mawaziri lakini pia mawaziri kuona kuwa labda wameonewa. Lakini zaidi pia utampa nafasi Rais mwenyewe kuhusika moja kwa moja na hivyo kuweza kujua kwa ukaribu kinachoendeoea na kuchukua hatua mara moja. Wawezekaji na wafanyabiashara wa sekta hii watakuwa na ujasiri wa pekee wa kwenda kujaribu kutoa kitu kidogo Ikulu ili mambo yao yaende na kwa wale tunaomjua Magufuli kuna watu wanaweza wakageuza toka Ikulu wakiwa na pingu!

Kama Rais mwenyewe alivyosema hili ni jambo zito basi ni vizuri alipe uzito unaostahili. Haifai kabisa kumpa mtu mwingine kwa sasa eneo hili.

Sioni namna nyingine ya kuunda upya eneo hili zaidi ya hii.
Mzeee mwanakijiji. Nimekuunga mkono %100. Hayo ndio mawazo ya kujenga na kuisaidia nchi.hongera sn kwana kijiji.
 
Back
Top Bottom