Wont be the same
JF-Expert Member
- Aug 15, 2024
- 1,564
- 2,483
Watendaji wa vituo wa Halmashauri ya Manispaa ya Tabora, Mkoani Tabora katika uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura wakitoa tamko la kujitoa uanachama wa chama cha siasa au kutokuwa mwanachama wa chama cha siasa na kiapo cha kutunza siri, mbele ya Afisa Mwandikishaji (hayupo pichani) kabla ya kuanza kwa mafunzo yao ya siku moja leo Aprili 29, 2025. Mafunzo hayo ni sehemu ya maandalizi ya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura awamu ya pili.
Uboreshaji wa Daftari awamu ya pili unafanyika sambamba na uwekaji wazi wa Daftari la Awali la Wapiga Kura kwenye mikoa ya Geita, Mara, Kagera, Shinyanga, Mwanza, Simiyu, Rukwa, Tabora, Katavi, Kigoma, Iringa, Ruvuma, Njombe, Mbeya na Songwe. Mazoezi hayo kwenye mikoa tajwa yatafanyika kwa siku saba kuanzia tarehe 01 Mei, 2025 hadi tarehe 07 Mei, 2025.
Uboreshaji wa Daftari awamu ya pili unafanyika sambamba na uwekaji wazi wa Daftari la Awali la Wapiga Kura kwenye mikoa ya Geita, Mara, Kagera, Shinyanga, Mwanza, Simiyu, Rukwa, Tabora, Katavi, Kigoma, Iringa, Ruvuma, Njombe, Mbeya na Songwe. Mazoezi hayo kwenye mikoa tajwa yatafanyika kwa siku saba kuanzia tarehe 01 Mei, 2025 hadi tarehe 07 Mei, 2025.