Influenza
JF-Expert Member
- Jul 1, 2018
- 1,445
- 3,403
Polisi mkoani Tabora inamshikilia mwalimu wa Shule ya Msingi Shila wilayani Nzega, Ferdinand Felix (33) kwa tuhuma za kujifanya polisi.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Emmanuel Nley amesema leo Jumatatu Mei 5, 2019 kuwa mwalimu huyo alikamatwa juzi saa 3:00 asubuhi katika baa na nyumba moja ya kulala wageni.
Amesema polisi walipata taarifa kuwa kuna tapeli anayedai kuwa ni askari kutoka Kituo cha Kasulu mkoani Kigoma na kwamba yupo likizo wilayani Nzega.
Nley amesema mtu huyo alipotakiwa kuonyesha kibali maalumu kinachomtambulisha maarufu kama movement order, alishindwa kukionyesha hivyo kudai kuwa yeye ni mwalimu.
Amesema uwapo wa soko la madini Nzega umevutia wahalifu na matapeli ambao wanataka kujipatia fedha kwa njia haramu.
Amewataka wakazi wa Nzega kuwa makini na matapeli hasa baada ya kuanzishwa soko la madini kwenye wilaya yao.
Diwani wa Nzega Mjini Mashariki, Frederick Ruhangisa, amesema matapeli wamekuwa wakisumbua hata kabla ya kuanzishwa soko la madini.
Amesema matapeli hao wamekuwa wakiwasumbua wananchi hasa katika mtaa wa Benki ya NMB na tayari wamejiwekea utaratibu wa kuwapa tahadhari wananchi kupitia mikutano ya hadhara.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Emmanuel Nley amesema leo Jumatatu Mei 5, 2019 kuwa mwalimu huyo alikamatwa juzi saa 3:00 asubuhi katika baa na nyumba moja ya kulala wageni.
Amesema polisi walipata taarifa kuwa kuna tapeli anayedai kuwa ni askari kutoka Kituo cha Kasulu mkoani Kigoma na kwamba yupo likizo wilayani Nzega.
Nley amesema mtu huyo alipotakiwa kuonyesha kibali maalumu kinachomtambulisha maarufu kama movement order, alishindwa kukionyesha hivyo kudai kuwa yeye ni mwalimu.
Amesema uwapo wa soko la madini Nzega umevutia wahalifu na matapeli ambao wanataka kujipatia fedha kwa njia haramu.
Amewataka wakazi wa Nzega kuwa makini na matapeli hasa baada ya kuanzishwa soko la madini kwenye wilaya yao.
Diwani wa Nzega Mjini Mashariki, Frederick Ruhangisa, amesema matapeli wamekuwa wakisumbua hata kabla ya kuanzishwa soko la madini.
Amesema matapeli hao wamekuwa wakiwasumbua wananchi hasa katika mtaa wa Benki ya NMB na tayari wamejiwekea utaratibu wa kuwapa tahadhari wananchi kupitia mikutano ya hadhara.