FRANCIS DA DON
JF-Expert Member
- Sep 4, 2013
- 40,799
- 46,917
Kuna katabia nimeka notice hasa huku sinza kwa mwaibula na maeneo ya jirani.., wenye maduka hutafuta vitoto vidogo vya miaka 12 hadi 14 ili vifanye kazi ya kuuza duka. obviously vitoto hivi vinadhulumiwa haki yao ya msingi ya kufurahia utoto na kupata elimu kwani huu muda ukipita haurudi tena. vile vile wanafanya kazi bila ujira wowote au ujira kidogo sana.Kuna wakati nilienda dukani saa saba usiku nikakakuta katoto kamoja kako dukani bado kanauza.., kalikuwa kanasinzia ila kalikuwa kanajikaza tuu.., nilimwonea huruma sana..,nilipomuuliza kwa nini hujafunga duka akaniambia hua hafungi duka.., yaan hakuna usingizi wa kueleweka.., ni kusinzia tu pale panapokua hakuna wateja. Serikali mpo..?!