Tabia ya kuomba hela imekithiri

Tabia ya kuomba hela imekithiri

tamu 3

Member
Joined
Dec 11, 2024
Posts
88
Reaction score
216
Tabia ya watu KUOMBA HELA inakuja kwa kasi sana.

Sio kwenye undugu, sio kwenye Urafiki, kwenye Mapenzi ndio usiseme Sasa.

Utasikia, Oi! Kama una ten haina kazi nifanyie utaratibu, kuna mishe nasikilizia !

Eti ten haina kazi. Kwa maisha gani mwamba uwe na ten haina kazi? Acha utani!

Mwingine sasa utasikia Mzee huku maduka yamefungwa, em nitumie buku tano chap nijiunge bando, kesho mapema narekebisha

Bora hata huyu uongo wake siyo mkali sana kama huyu anayesema oi huku leo ATM zote hazifanyi kazi nirekebishie ten chap narudisha mapema!😄😄

Ukimnyima anakutishia kwamba kumbuka kuna kesho, we poa tu!

Zamani hii tabia ya kuombaomba tulijua ni ya dada zetu tu lakini siku hizi mpaka wanaume wamo

Maana siku hizi hata vijana wa kiume wanaomba zawadi, usipo waletea wananuna. Nyiee! Hii sijaipenda kabisa.


Kijana wa kiume hata kumtumia mwanaume mwenzako sms ya nipigie inashitua sana. Tena anaandika pg🫢🫢. Hapana bhana!

Siku hizi dada zetu wanalalamika sana kwamba vijana wa kiume mnawaomba sana hela. Hii kiafrika haikubaliki!

Tabia hii ya kuomba watu hela imetuharibia ule utamaduni wa kusalimiana na kujuliana hali tuliokuwa nao huko nyuma.

Siku hizi ni hatari kumjulia hali mtu. Kuna mtu ukimsalimia hapo hapo anakuomba hela.

Sasa ole wako umwambie ntakucheki, inageuka kuwa deni, zitapigwa simu mpaka ukome. Ndani ya siku moja utakuta missed calls mpaka 200. Atakuomba utadhani pesa zako ni zake.

Hata ule utamaduni wa kuaga ndugu, jamaa na masela wakati unasafiri ili wakutakie baraka tele umeondoka. Watu sasa wanaogopa kuaga wataombwa kurudi na vitu.

Kama unaenda Kigoma utaagizwa dagaa, mawese, migebuka na vitenge vya Congo as if kule unakwenda kuviokota mtoni. Maana mtoni ndiko kuna vya bure inasema methali ya waha

Kama unakwenda Mbeya jiandae kuagizwa mchele na maharage ya Soya maji mara moja.

Unakwenda Mwanza watakutuma Sangara na senti tano hawakupi. Sasa usiwaletee. Utanuniwa ukome.

Nimeona niyaseme haya kabla hujalala. Kama umenielewa naomba ukamwambie na jamaa yako naye aache hii tabia, anatukera sana.

Mwambie jamaa yako kuna watu siku hizi wakimuona mbele wanamkwepa ili asiwaombe hela.

🤡🤡
 
Tabia ya watu KUOMBA HELA inakuja kwa kasi sana.

Sio kwenye undugu, sio kwenye Urafiki, kwenye Mapenzi ndio usiseme Sasa.

Utasikia, Oi! Kama una ten haina kazi nifanyie utaratibu, kuna mishe nasikilizia !

Eti ten haina kazi. Kwa maisha gani mwamba uwe na ten haina kazi? Acha utani!

Mwingine sasa utasikia Mzee huku maduka yamefungwa, em nitumie buku tano chap nijiunge bando, kesho mapema narekebisha

Bora hata huyu uongo wake siyo mkali sana kama huyu anayesema oi huku leo ATM zote hazifanyi kazi nirekebishie ten chap narudisha mapema!😄😄

Ukimnyima anakutishia kwamba kumbuka kuna kesho, we poa tu!

Zamani hii tabia ya kuombaomba tulijua ni ya dada zetu tu lakini siku hizi mpaka wanaume wamo

Maana siku hizi hata vijana wa kiume wanaomba zawadi, usipo waletea wananuna. Nyiee! Hii sijaipenda kabisa.


Kijana wa kiume hata kumtumia mwanaume mwenzako sms ya nipigie inashitua sana. Tena anaandika pg🫢🫢. Hapana bhana!

Siku hizi dada zetu wanalalamika sana kwamba vijana wa kiume mnawaomba sana hela. Hii kiafrika haikubaliki!

Tabia hii ya kuomba watu hela imetuharibia ule utamaduni wa kusalimiana na kujuliana hali tuliokuwa nao huko nyuma.

Siku hizi ni hatari kumjulia hali mtu. Kuna mtu ukimsalimia hapo hapo anakuomba hela.

Sasa ole wako umwambie ntakucheki, inageuka kuwa deni, zitapigwa simu mpaka ukome. Ndani ya siku moja utakuta missed calls mpaka 200. Atakuomba utadhani pesa zako ni zake.

Hata ule utamaduni wa kuaga ndugu, jamaa na masela wakati unasafiri ili wakutakie baraka tele umeondoka. Watu sasa wanaogopa kuaga wataombwa kurudi na vitu.

Kama unaenda Kigoma utaagizwa dagaa, mawese, migebuka na vitenge vya Congo as if kule unakwenda kuviokota mtoni. Maana mtoni ndiko kuna vya bure inasema methali ya waha

Kama unakwenda Mbeya jiandae kuagizwa mchele na maharage ya Soya maji mara moja.

Unakwenda Mwanza watakutuma Sangara na senti tano hawakupi. Sasa usiwaletee. Utanuniwa ukome.

Nimeona niyaseme haya kabla hujalala. Kama umenielewa naomba ukamwambie na jamaa yako naye aache hii tabia, anatukera sana.

Mwambie jamaa yako kuna watu siku hizi wakimuona mbele wanamkwepa ili asiwaombe hela.

🤡🤡
Kuna jamaa angu ananikera simu ikingia ni hela tu afu anabet bac tu.
 
Hakuna kitu kibaya humu duniani kama shida,

Tatizo ni kukosa uaminifu....

Maisha ya kila mmoja wetu yapo kwa mikono ya mwingine...

Nakopa, naomba Ila narudisha.
 
Upo sahihi, wakaka na wababa wanaongoza kwa kuomba hela,
Juzi kuna libaba lilinipigia salamu ndeeefu mwisho wake ananiomba laki, nikaliambia "ungekua mdada sawa ila mbaba, pambana aiseee"
 
Tabia ya watu KUOMBA HELA inakuja kwa kasi sana.

Sio kwenye undugu, sio kwenye Urafiki, kwenye Mapenzi ndio usiseme Sasa.

Utasikia, Oi! Kama una ten haina kazi nifanyie utaratibu, kuna mishe nasikilizia !

Eti ten haina kazi. Kwa maisha gani mwamba uwe na ten haina kazi? Acha utani!

Mwingine sasa utasikia Mzee huku maduka yamefungwa, em nitumie buku tano chap nijiunge bando, kesho mapema narekebisha

Bora hata huyu uongo wake siyo mkali sana kama huyu anayesema oi huku leo ATM zote hazifanyi kazi nirekebishie ten chap narudisha mapema!😄😄

Ukimnyima anakutishia kwamba kumbuka kuna kesho, we poa tu!

Zamani hii tabia ya kuombaomba tulijua ni ya dada zetu tu lakini siku hizi mpaka wanaume wamo

Maana siku hizi hata vijana wa kiume wanaomba zawadi, usipo waletea wananuna. Nyiee! Hii sijaipenda kabisa.


Kijana wa kiume hata kumtumia mwanaume mwenzako sms ya nipigie inashitua sana. Tena anaandika pg🫢🫢. Hapana bhana!

Siku hizi dada zetu wanalalamika sana kwamba vijana wa kiume mnawaomba sana hela. Hii kiafrika haikubaliki!

Tabia hii ya kuomba watu hela imetuharibia ule utamaduni wa kusalimiana na kujuliana hali tuliokuwa nao huko nyuma.

Siku hizi ni hatari kumjulia hali mtu. Kuna mtu ukimsalimia hapo hapo anakuomba hela.

Sasa ole wako umwambie ntakucheki, inageuka kuwa deni, zitapigwa simu mpaka ukome. Ndani ya siku moja utakuta missed calls mpaka 200. Atakuomba utadhani pesa zako ni zake.

Hata ule utamaduni wa kuaga ndugu, jamaa na masela wakati unasafiri ili wakutakie baraka tele umeondoka. Watu sasa wanaogopa kuaga wataombwa kurudi na vitu.

Kama unaenda Kigoma utaagizwa dagaa, mawese, migebuka na vitenge vya Congo as if kule unakwenda kuviokota mtoni. Maana mtoni ndiko kuna vya bure inasema methali ya waha

Kama unakwenda Mbeya jiandae kuagizwa mchele na maharage ya Soya maji mara moja.

Unakwenda Mwanza watakutuma Sangara na senti tano hawakupi. Sasa usiwaletee. Utanuniwa ukome.

Nimeona niyaseme haya kabla hujalala. Kama umenielewa naomba ukamwambie na jamaa yako naye aache hii tabia, anatukera sana.

Mwambie jamaa yako kuna watu siku hizi wakimuona mbele wanamkwepa ili asiwaombe hela.

🤡🤡
Kama huwezi wapelekea walichoagiza si waambie tu mapema kwanini ujifanye unazo wakati huna, haya naomba Pesa🤭
 
Siku hizi kuna sehemu kibao za kukopa, kuanzia 50k kulingana na shida yako.

Mambo ya kwenda kulia shida kwa mtu then akusambaze huwa sipendi hata kidogo.
 
Hivi mnaanzaje kuomba mtu pesa mbona mimi nashindwa nipeni mbinu loh, sijui kuomba kukopa kujifanya mnyonge nakufa na shida zangu.
Nilikuwaga hivi ila 2016 mpaka 2019, nimemeuomba sana Maza na Bro hela , life lilikuwa tight kinoma. Sema nakuelewa mara nyingi nimekuwa nikiishi hivyo.
 
Makanisani pia, Kila jpili uandae chenji za buku buku za kutosha.
 
Back
Top Bottom