Tabia hii ya mke wangu inaashiria nini?

Tabia hii ya mke wangu inaashiria nini?

Mkulima na Mfugaji

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2013
Posts
1,056
Reaction score
1,867
Mimi ni kijana ambaye niko kwenye ndoa naelekea mwaka wa pili sasa. Kama kawaida kwenye ndoa kuna milima na mabonde ya kupitia, na pia kwenye ndoa kuna Raha na karaha. Ila kwa Mke wangu kila anaponikwaza adhabu ambayo inamtesa nikimpa ni kususia chakula,na kumtenga kitandani yaani adhabu hizi huwa zinampa sana Tabu adhabu hii.

Alishawahi kuniambia kwamba hata kama unakasirika ila kula chakula changu halafu endelea kununa, kuna siku aliniudhi usiku nikamtenga kitanda nilichukua mkeka nikatandika sebuleni, kuja kusituka usiku wa manane namuona pembeni yangu kalala ikabidi nimuamshe tukalale kitandani.

Sasa leo ameniuzi tokea asubuhi sijala na yeye pia tokea asubuhi mpaka jioni ya leo hajakula kitu na ananyonyesha. Je tabia hii ya mke wangu inaashiria nini?
 
Dah nimecheka sana broo kwanini ulikimbilia kuowa unaisi utamuowa mkamilifu raha ya kukosea ni kuelezana ukweli na kumkanya kumbuka makosa mkiwa mnaishi pamoja hayaishi kwaiyo kukanyana, kukumbushana, na kusamehana ndyo njiya ya kuzidi kutete ndoa yenu
 
Kususa na kununa ni tabia za asili za kike. Wanaume tabia zetu ni ubabe, utemi na kufanya maamuzi. Hivyo nakushauri mtoa mada uachane na hizo tabia zako, maana kuna siku utasusa kumshugulikia mkeo. Utakuja sikia analiwazwa na jemba ya jirani.
 
Asee mkuu, wife hatengwi wala kupewa silent treatment hizo. Mwanaume kuwa na kifua kikubwa na usikubali zinaisha siku mbili tatu una makwaruzano na wife afu umemnunia nunia, hiyo ni big NO kwa wanaume.

Wew ndo kichwa cha familia, muongoze mnayamaliza unampiga make-up sex safi then mnalala roho safi kma mmeoana jana sio kumtenga. Mana hapo yeye anaonekana ana busara zaidi despite kuzinguana bado anakuweka karibu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom