Sema Tanzania
JF-Expert Member
- May 18, 2016
- 251
- 465
Waswahili walisema, “Kuzaa sio kazi, kazi kulea mwana”. Kama mzazi ni jukumu lako kuhakikisha mwanao anakua katika mazingira mazuri na elekezi ili kumfanya awe ni mwenye hekima kuanzia mdogo mpaka kufikia utu uzima wake.
Kumkuza mtoto mdogo awe vile unavyotaka kupitia muonekano wako au mtazamo wako ni kitu kikubwa sana na kama unajiona uko hivyo ulivyo sasa kwa sababu ya wazazi wako washukuru sana, maana si kazi ndogo waliofanya.
Kuna vitu kadha wa kadha ambavyo vinaweza kuchangia katika ukuaji au malezi kwa namna moja au nyingine. Mfano mazingira unayoishi, hali ya kijamii na uchumi wa familia, na vile vile elimu ya wazazi wanaomlea mtoto. Ni vigumu kujua njia ipi ya malezi itakuwa sahihi, kwani uzoefu unaonesha kuwa kuna baadhi ya tabia za wazazi ambazo zinaweza kuathiri malezi ya mtoto kwa njia chanya ama hasi.
Zifuatazo ni tabia ambazo wazazi wengi wanazo ambazo hupelekea watoto wao wasifanikiwe maishani.
1. Wazazi wasio wahamasisha watoto wao kujitegemea/ kuwa huru. Wazazi wanashauriwa kuwahimiza watoto wao kuwa wenye kujitegemea kimawazo na kujiamini, hii inasaidia sana hata anapokutana na vishawishi katika rika lake, ajue lipi baya lipi zuri. Unapomuamulia kila kitu haumjengi. Unamjenga mtoto endapo utamfanya ajiamini na kujitegemea. Kumbuka kwamba hautaishi nae milele, jifunze sasa kumwacha huru katika maamuzi madogo atajiamini na kutatua matatizo yake binafsi.
2. Wazazi wanaokaripia watoto wao mara kwa mara. Unapokuwa unatumia maneno makali kila mara mtoto anapokosea kuna madhara ya muda mrefu. Kumkaripia mtoto, kumtukana, kumsema kwa kejeli humfanya mtoto awe kwanza muoga wa kila kitu au tuseme si mthubutu, hii peke yake imtarudisha nyuma katika makuzi yake na vile vile kama mzazi, jaribu kutafuta njia mbadala ya kumfunza mtoto, maana kuna usemi unasema ‘mtoto umleavyo ndivyo akuavyo’, mtaanza kufokeana ndani ya nyumba akifikia umri wa balehe na kumbe lilikua kosa lako.
3. Tabia ya mzazi utaka kujua kila kitu kinachoendelea katika maisha ya mtoto.
Sawa ni kitu kizuri kwa upande mwingine, unakua haukosei sehemu yoyote ya maisha ya mwanao lakini kuendesha kila kitu chake kutampelekea mtoto awe na wasiwasi na huzuni kupindukia. Hawezi kufanya uamuzi wowote ule katika maisha yake bila wewe kuwepo, unakuta mama au baba walitaka kuwa madaktari ikashindikana, wanalazimisha sasa ndoto zao zitimizwe na mtoto na yeye kwa uoga wa kuwasaliti anang’ang’ania fani ambayo wala haiwezi maskini, ni lazima tu atafeli, tena sio shule tu, anafeli hadi maisha. Maana muda wake mwingi anautumia kufanya kitu ambacho hakina manufaa kwake kwasababu tu mzazi alisema.
4. Kumuacha mtoto aamue mwenyewe muda wa kulala.
Wanasayansi wanasema ukuaji wa ubongo wa mtoto mdogo unahitaji fomula, mtoto hawezi kuamua mwenyewe alale saa mbili usiku kila siku, leo atalala saa 1 kama alichoka sana, kesho atalala saa 3 kama kwenye TV kulikua na kipindi anachopenda kukiangalia, na siku nyingine atalala hata saa 6 ukiamua umuache mwenyewe aamue. Mpangie muda wa kulala usiopungua masaa 9-10 usiku hili litamsaidia hata akiamka kuwa mwenye nguvu za kujifunza vitu vipya na ubongo wake utakua kwa nafasi.
5. Wazazi wanaotumia mabavu:
Mzazi anayetumia mabavu ni yule anayetoa amri moja, na usipoifuata utaona cha mtema kuni, mfano anaposema, ‘Ufaulu mtihani la sivyo ukifeli usirudi nyumbani’ . Kwa wakati mwingine mzazi mwenye mamlaka na mwenye kutaka aeleweke kwanini amesema hivyo ujumbe wake utatoka kwa namna tofauti, mfano ‘Inakulazimu ufaulu mtihani, maana watu wote waliofanya vizuri shuleni wana maisha mazuri baada ya kumaliza shule’. Hawa ni wazazi wawili tofauti. Ulezi wa kutumia mabavu haujengi hata kidogo, kwa mfano mtoto kafeli, halafu harudi nyumbani si ataishia kuwa mtoto wa mtaani au kibaya zaidi kuwa kibaka.
MUHIMU: Makala hii itaendelea juma lijalo....
Kumkuza mtoto mdogo awe vile unavyotaka kupitia muonekano wako au mtazamo wako ni kitu kikubwa sana na kama unajiona uko hivyo ulivyo sasa kwa sababu ya wazazi wako washukuru sana, maana si kazi ndogo waliofanya.
Kuna vitu kadha wa kadha ambavyo vinaweza kuchangia katika ukuaji au malezi kwa namna moja au nyingine. Mfano mazingira unayoishi, hali ya kijamii na uchumi wa familia, na vile vile elimu ya wazazi wanaomlea mtoto. Ni vigumu kujua njia ipi ya malezi itakuwa sahihi, kwani uzoefu unaonesha kuwa kuna baadhi ya tabia za wazazi ambazo zinaweza kuathiri malezi ya mtoto kwa njia chanya ama hasi.
Zifuatazo ni tabia ambazo wazazi wengi wanazo ambazo hupelekea watoto wao wasifanikiwe maishani.
1. Wazazi wasio wahamasisha watoto wao kujitegemea/ kuwa huru. Wazazi wanashauriwa kuwahimiza watoto wao kuwa wenye kujitegemea kimawazo na kujiamini, hii inasaidia sana hata anapokutana na vishawishi katika rika lake, ajue lipi baya lipi zuri. Unapomuamulia kila kitu haumjengi. Unamjenga mtoto endapo utamfanya ajiamini na kujitegemea. Kumbuka kwamba hautaishi nae milele, jifunze sasa kumwacha huru katika maamuzi madogo atajiamini na kutatua matatizo yake binafsi.
2. Wazazi wanaokaripia watoto wao mara kwa mara. Unapokuwa unatumia maneno makali kila mara mtoto anapokosea kuna madhara ya muda mrefu. Kumkaripia mtoto, kumtukana, kumsema kwa kejeli humfanya mtoto awe kwanza muoga wa kila kitu au tuseme si mthubutu, hii peke yake imtarudisha nyuma katika makuzi yake na vile vile kama mzazi, jaribu kutafuta njia mbadala ya kumfunza mtoto, maana kuna usemi unasema ‘mtoto umleavyo ndivyo akuavyo’, mtaanza kufokeana ndani ya nyumba akifikia umri wa balehe na kumbe lilikua kosa lako.
3. Tabia ya mzazi utaka kujua kila kitu kinachoendelea katika maisha ya mtoto.
Sawa ni kitu kizuri kwa upande mwingine, unakua haukosei sehemu yoyote ya maisha ya mwanao lakini kuendesha kila kitu chake kutampelekea mtoto awe na wasiwasi na huzuni kupindukia. Hawezi kufanya uamuzi wowote ule katika maisha yake bila wewe kuwepo, unakuta mama au baba walitaka kuwa madaktari ikashindikana, wanalazimisha sasa ndoto zao zitimizwe na mtoto na yeye kwa uoga wa kuwasaliti anang’ang’ania fani ambayo wala haiwezi maskini, ni lazima tu atafeli, tena sio shule tu, anafeli hadi maisha. Maana muda wake mwingi anautumia kufanya kitu ambacho hakina manufaa kwake kwasababu tu mzazi alisema.
4. Kumuacha mtoto aamue mwenyewe muda wa kulala.
Wanasayansi wanasema ukuaji wa ubongo wa mtoto mdogo unahitaji fomula, mtoto hawezi kuamua mwenyewe alale saa mbili usiku kila siku, leo atalala saa 1 kama alichoka sana, kesho atalala saa 3 kama kwenye TV kulikua na kipindi anachopenda kukiangalia, na siku nyingine atalala hata saa 6 ukiamua umuache mwenyewe aamue. Mpangie muda wa kulala usiopungua masaa 9-10 usiku hili litamsaidia hata akiamka kuwa mwenye nguvu za kujifunza vitu vipya na ubongo wake utakua kwa nafasi.
5. Wazazi wanaotumia mabavu:
Mzazi anayetumia mabavu ni yule anayetoa amri moja, na usipoifuata utaona cha mtema kuni, mfano anaposema, ‘Ufaulu mtihani la sivyo ukifeli usirudi nyumbani’ . Kwa wakati mwingine mzazi mwenye mamlaka na mwenye kutaka aeleweke kwanini amesema hivyo ujumbe wake utatoka kwa namna tofauti, mfano ‘Inakulazimu ufaulu mtihani, maana watu wote waliofanya vizuri shuleni wana maisha mazuri baada ya kumaliza shule’. Hawa ni wazazi wawili tofauti. Ulezi wa kutumia mabavu haujengi hata kidogo, kwa mfano mtoto kafeli, halafu harudi nyumbani si ataishia kuwa mtoto wa mtaani au kibaya zaidi kuwa kibaka.
MUHIMU: Makala hii itaendelea juma lijalo....