Taasisi za kiislamu tokeni hadharani mkemee kauli tata za mashehe

ngara23

JF-Expert Member
Joined
Aug 31, 2019
Posts
15,774
Reaction score
35,994
Hapa naziita taasisi zote za kiislamu kuanzia Bakwata, Sunni jamaat,shia n.k

Uislamu ni dini iliyojipambanua kama dininya haki na misimamo ya haki, kujali utu na heshima Kwa watu wote

Kumekuwepo mashehe wanaotoa matamko tata kuhusu masuala ya utawala Bora hapa nchi

Mfano Leo shehe Mawinda akimwakilisha mufti amesema "heri mtu akatwe kichwa" ila amani iwepo.
Hii ni kauli ya kipumbavu kutamkwa na mtu tunayemheshimu katika jamii, anabariki mtu akatwe kichwa badala ya kuishawishi kuchukuliwa Kwa sheria za nchi ikiwa ni pamoja na kuwakamata na kuwafikisha mahakamani wale wavunja amani

Shehe Mawinda amechafua taasisi kubwa kama Bakwata na uislam Kwa ujumla

Waislam wana mashehe wasomi wanaoweza kuongea mambo mema Kwa umma, Kwa Nini mkubali kuongozwa na mashehe wafedhuli kama mawinda
 
Nje ya mada
Mfano nimempa mimba mdada bahati mbaya nika muomba msamaha akakubali bado nitakuwa muhusika katika mimba ile?

Msinifokee mimi last born wenu
 
Nje ya mada
Mfano nimempa mimba mdada bahati mbaya nika muomba msamaha akakubali bado nitakuwa muhusika katika mimba ile?

Msinifokee mimi last born wenu
Vip ikiwa wewe itapigwa mimba?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…